Namna Mbalimbali ya Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 5
“Je, unaona kama dini inachochea watu kupendana na kuishi kwa amani na wengine ao kuchukiana na kutendeana kwa jeuri? [Acha mutu ajibu.] Acha nikuonyeshe jambo fulani lenye kupendeza juu ya habari hii.” Umuonyeshe musikilizaji wako Mnara wa Mlinzi wa tarehe 01/05, na muzungumuzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na umusomee hata andiko moja kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umutolee mutu magazeti na ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/05/12
“Watu wengi wanawaza kama ni vizuri dini ijiingize katika mambo ya politike, lakini wengine wanawaza kama ni vibaya kufanya hivyo. Wewe unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Ona namna Yesu alivyofanya alipokuwa duniani wakati watu walitaka kumufanya kuwa mufalme. [Soma Yohana 6:15.] Gazeti hili linaeleza kwa nini Yesu hakukubali na pia linazungumuzia njia nzuri zaidi ambayo Wakristo wanaweza kutumia ili kusaidia watu kuliko kuingia katika mambo ya politike.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Karibu kila mumoja wetu amekwisha kutendewa isivyo haki wakati fulani. Unafikiri kuna mutawala fulani anayeweza kumaliza ukosefu wa haki? [Acha mutu ajibu.] Ona unabii wa Biblia unaozungumuzia mutawala atakayemaliza ukosefu wa haki. [Soma Zaburi 72:11-14.] Biblia inaahidi kwamba wakati ujao kutakuwa na haki. Gazeti hili linazungumuzia jambo hilo.”