Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 6
Soma Isaya 42:8. Kisha sema hivi: “Kulingana na andiko hili, Mungu ana jina. Unawaza ni lazima tutumie jina la Mungu? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo gazeti hili linasema.” Umuonyeshe mutu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 mwezi wa 6, na muzungumuzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/06/12
“Ningependa kujua mawazo yako juu ya habari moja ya lazima. [Fungua ukurasa wa 3, na umuonyeshe habari zilizo kwenye ukurasa huo.] Kati ya mawazo yanayosemwa hapa, ni wazo gani linaloambatana na mawazo yako? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema yenyewe. [Soma Waroma 15:4.] Gazeti hili linazungumuzia sababu tano zinazofanya Biblia iwe kitabu cha pekee na linaonyesha namna Biblia inavyoweza kutufaidi.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Kila mwaka mamilioni ya watu duniani pote wanagonjwa kwa sababu ya chakula chenye kuharibika. Wewe unawaza chakula tunachotumia katika eneo letu ni kizuri ao ni chenye kuharibika? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha njia ine zinazoweza kutusaidia tulinde familia yetu. Linazungumuzia pia ahadi ya Biblia ya kwamba karibuni kila mutu atafurahia chakula kizuri kwa uwingi.” Soma Zaburi 104:14, 15.