Faida ya Kuwa na Eneo lako Mwenyewe
1. Sababu gani ni vizuri kufikiria kuwa na eneo lako mwenyewe?
1 Sababu gani ni vizuri kufikiria kuwa na eneo lako mwenyewe? Ikiwa kutaniko lenu lina eneo kubwa, unaweza kuwa na eneo lako, labda karibu na mahali unapoishi. Kitabu Tengenezo kwenye ukurasa wa 103, kinasema hivi: ‘Kuwa na eneo lako karibu kutakuwezesha kutumia vizuri wakati wako katika mahubiri. Unaweza kumuambia muhubiri mwengine ili akusindikize katika eneo lako.’
2. Namna gani kuwa na eneo lako mwenyewe kunakutolea nafasi ya kuhubiri zaidi?
2 Usisahau Kutegemeza Kikundi Chenu cha Mahubiri: Ikiwa una eneo lako karibu na mahali pako pa kazi, unaweza kuhubiri humo wakati wa mapumuziko ao mbele ya kurudi nyumbani, labda pamoja na muhubiri mwengine anayetumikia karibu na hapo. Ikiwa una eneo karibu na nyumba yako, inaweza kuwa rahisi kwako na familia yako kuhubiri katika eneo hilo wakati wa mangaribi. Ikiwa hamuhuzurie mukutano kwa ajili ya mahubiri, itakuwa vizuri mbele ya kuanza kuhubiri mumuombe Yehova awape muongozo. (Flp. 4:6) Tena, haupaswe kuhubiri katika eneo lako tu; unapaswa pia kujiunga na kikundi chenu cha mahubiri. Zaidi sana Siku ya Posho na Siku ya Yenga, ni vizuri zaidi kutegemeza kikundi chenu cha mahubiri kwa kuwa vikundi vingi vya mahubiri vinapanga mikutano kwa ajili ya mahubiri siku hizo.
3. Unaweza kupata faida gani kwa kuwa na eneo lako mwenyewe?
3 Faida: Ikiwa una eneo lako, una mahali pa kuhubiri wakati wowote kulingana na programu yako. Haupitishe wakati mwingi ili kuenda kwenye eneo, kwa hiyo unakuwa na wakati mwingi wa kuhubiri. Hilo linasaidia wahubiri fulani kuwa mapainia wasaidizi ao mapainia wa kawaida. Kwa kuwa watu unaohubiria ni majirani wako, itakuwa rahisi kuwarudilia na kuongoza mafunzo ya Biblia. Wahubiri wengi wanaona kama kuhubiri katika maeneo yao wenyewe kunawasaidia wajuane na watu wa maeneo hayo, na pia kunasaidia watu hao wawaaminie, zaidi sana ikiwa maeneo hayo yanaweza kuhubiriwa zaidi ya mara moja mbele ya kupewa wahubiri wengine. Kuhubiri katika eneo lako kunakusaidia wewe na familia yako mutimize kwa ukamili huduma yenu, sivyo?—2 Tim. 4:5.