Tujitayarishe kwa Furaha kwa Ajili ya Ukumbusho
1. Kipindi cha Ukumbusho kinatutolea nafasi gani ya pekee?
1 Ukumbusho tutakaofanya Siku ya Pili tarehe 26 Mwezi wa 3, utatutolea nafasi nzuri ya kufurahia mipango ambayo Mungu alifanya ili kutukomboa. (Isa. 61:10) Hata mbele siku hiyo ifike, tukiwa na furaha tutajitayarisha vizuri kwa ajili ya siku hiyo. Namna gani?
2. Sababu gani tunatayarisha vizuri ukumbusho?
2 Kutayarisha Ukumbusho: Chakula cha Jioni cha Bwana ni mwazimisho mwepesi, lakini wa maana sana. Hata hivyo, inaomba kufanya mipango kwa ajili ya mwazimisho huo mbele ya wakati ili mambo madogomadogo ya maana yasipuuzwe. (Met. 21:5) Inaomba kupanga wakati unaofaa na kutayarisha mahali panapofaa. Inaomba kutayarisha mukate na divai. Mahali pa kufanyia mwazimisho huo panapaswa kuwa safi na kutayarishwa vizuri. Ndugu atakayetoa hotuba ya Ukumbusho anapaswa kujitayarisha vizuri, na ndugu watakaosaidia kupitisha mukate na divai na wakaribishaji wanapaswa kufuata maagizo waliyopewa. Bila shaka mengi ya mambo hayo yamekwisha kutayarishwa. Tunatayarisha vizuri Ukumbusho ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya zabihu ya ukombozi.—1 Pet. 1:8, 9.
3. Namna gani tutatayarisha moyo wetu kwa ajili ya Chakula cha Jioni cha Bwana?
3 Kutayarisha Moyo: Ni lazima pia tutayarishe moyo wetu ili tuelewe kabisa sababu gani tunaazimisha Ukumbusho. (Ezra 7:10) Kwa kusudi hilo, tunapaswa kuchukua wakati wa kuchunguza maandiko ya Biblia yanayopendekezwa kwa ajili ya Ukumbusho, na kutafakari juu ya siku za mwisho za maisha ya Yesu duniani. Kutafakari juu ya roho ya kujitoa ya Yesu kutatuchochea kumuiga.—Gal. 2:20.
4. Ni faida gani inayotokana na zabihu ya ukombozi inayokufurahisha zaidi?
4 Kifo cha Yesu kinatetea haki ya Yehova ya kutawala. Kinatukomboa kutoka zambi na kifo. (1 Yoh. 2:2) Kinatuwezesha kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Mungu na kinafungua njia ya kupata uzima wa milele. (Kol. 1:21, 22) Tena, tunapotafakari juu ya kifo cha Yesu, hilo linatusaidia kutia nguvu azimio letu la kuishi kulingana na naziri yetu kwa Yehova na kuendelea kumufuata Yesu. (Mt. 16:24) Unapojitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho unaokuja na pia utakapouhuzuria, furaha yako na iendelee kuongezeka!