Unajitayarisha kwa Ajili ya Ukumbusho?
Ilikuwa tarehe 13, Mwezi wa Nisani Mwaka wa 33. Yesu alijua kwamba alibakia na mangaribi moja tu ya kupitisha na mitume wake. Angefanya nao Pasaka yake ya mwisho na kuanzisha jambo jipya, ni kusema Chakula cha Bwana cha Mangaribi. Kwa sababu tukio la maana kama hilo linaomba kujitayarisha muzuri, Yesu aliwatuma Petro na Yohana ili watayarishe mambo. (Luka 22:7-13) Kuanzia siku hiyo, ni lazima sana kila mwaka wakristo wenye wanapenda kufanya Ukumbusho wajitayarishe kwa ajili ya tukio hilo. (Luka 22:19) Ni mambo gani ya lazima tunapaswa kutayarisha kwa ajili ya Ukumbusho wenye tutafanya tarehe 3, Mwezi wa 4?
Namna wahubiri wanapaswa kujitayarisha:
Wafanye mipango ili kuhubiri sana wakati wa kampanye ya kuwatolea watu mialiko ya Ukumbusho.
Waandike majina ya wanafunzi wao wa Biblia, watu wa jamaa yao, wanafunzi ao wafanyakazi wenzao na watu wengine wenye wanajuana nao ili wawaalike kwenye Ukumbusho.
Wasome na kufikiri sana juu ya maandiko ya Biblia kwa ajili ya Ukumbusho.
Wakuje kwenye Ukumbusho na wako tayari kukaribisha wageni.