Namna ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Broshua Mupya ili Kutusaidia Kuwaelekeza Wanafunzi wa Biblia Kwenye Tengenezo
1. Taja sababu tatu zilizofanya broshua Mapenzi ya Yehova ichapishwe.
1 Je, umeanza kutumia broshua mupya Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? Kusudi la broshua hiyo ni: (1) Kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wawajue Mashahidi wa Yehova, (2) kuwasaidia waelewe kazi zetu, na (3) kuwaonyesha namna tengenezo letu linavyotenda. Broshua Mapenzi ya Yehova ina habari moja kwenye kila ukurasa ambayo inaweza kuchunguzwa kwa muda wa dakika tano ao kumi mwishoni mwa kila funzo.
2. Eleza namna broshua hiyo inavyopangwa.
2 Namna Inavyopangwa: Broshua hiyo ina sehemu tatu, kila sehemu inazungumuzia mambo mbalimbali kuhusu tengenezo la Yehova kama inavyoelezwa hapa juu. Kichwa cha kila moja ya masomo 28 yaliyo ndani ni ulizo, na vichwa vidogovidogo vinavyofuata vinaandikwa na maandishi meusi mazito na vinajibu ulizo hilo. Broshua hiyo ina picha kutoka katika inchi zaidi ya 50, picha hizo zimeongezwa ili kuonyesha wanafunzi namna kazi yetu inavyoenea duniani pote. Masomo mengi yana visanduku “Ikiwa Unapenda Kujua Zaidi.” Visanduku hivyo vina mapendekezo mbalimbali; unaweza kumutia moyo mwanafunzi ayatumie.
3. Namna gani tunaweza kutumia broshua Mapenzi ya Yehova?
3 Namna Unavyoweza Kuitumia: Anza kwa kumuonyesha mwanafunzi ulizo linalofanyiza kichwa cha somo. Kisha, munaposoma habari iliyo katika somo hilo pamoja, kazia vichwa vidogovidogo vinavyoandikwa kwa maandishi meusi mazito. Mwishowe, zungumuzia maulizo ya kujikumbusha yaliyo chini ya ukurasa. Unaweza kusoma somo lote ao kusoma na kuzungumuzia sehemu baada ya ingine. Tumia akili unapoamua andiko linalopaswa kusomwa. Usisahau kuzungumuzia picha mbalimbali na visanduku “Ikiwa Unapenda Kujua Zaidi.” Kwa kawaida, utazungumuzia kila somo kwa kufuata utaratibu ulio katika broshua. Lakini, ikiwa kuna jambo ambalo mwanafunzi anataka kujua kwa haraka, ujisikie huru kuchagua somo linalozungumuzia jambo hilo. Kwa mufano, ikiwa karibuni mutakuwa na mukusanyiko wa muzunguko, wa pekee ao wa wilaya, unaweza kuchagua somo la 11.
4. Sababu gani wewe ni mwenye furaha kwa kuwa tuna broshua hiyo mupya?
4 Tunapojifunza Biblia na mutu, tunamusaidia afahamiane na Baba yetu wa mbinguni. Lakini, ni lazima tumufundishe pia kuhusu tengenezo la Yehova. (Met. 6:20) Sisi ni wenye furaha kabisa kwa kuwa tuna broshua hiyo inayofanya iwe rahisi kwetu kufanya hivyo!