Tumia Adresi Yetu ya Internete ili Kuwafundisha Watoto Wako
1. Kwenye adresi yetu ya Internete, sehemu yenye kichwa “Watoto” imetayarishwa kwa kusudi gani?
1 Adresi yetu ya Internete, jw.org, imetayarishwa ili iwapendeze watu wa kila umri. Kwenye adresi yetu, sehemu yenye kichwa “Watoto” (fungua maneno Mafundisho ya Biblia, kisha fungua neno Watoto) inasaidia watoto wadogo na wazazi wao wakaribiane, na pia wamukaribie Yehova. (Kum. 6:6, 7) Namna gani unaweza kutumia sehemu hiyo ili kuwafundisha watoto wako?
2. Namna gani unaweza kuchagua habari ya kujifunza na watoto wako kulingana na umri wao?
2 Patanisha Mafundisho na Miaka ya Watoto: Kila mutoto ana mahitaji yake. (1 Kor. 13:11) Namna gani basi unaweza kuchagua habari ya kujifunza na watoto wako kulingana na umri wao? Ujiulize: ‘Ni habari gani itakayowapendeza watoto wangu? Wataelewa habari hiyo kwa kadiri gani? Wanaweza kuendelea kukaza akili kwa muda gani?’ Kuhusu watoto wenye miaka mitatu ao chini ya miaka hiyo, unaweza kuzungumuzia habari zinazopatikana chini ya kichwa “Ninajifunza Biblia.” Familia zingine zinachunguza hadisi za Biblia zinazopatikana katika sehemu “Uwafundishe Watoto Wako.” Pia, chunguza sehemu zifuatazo.
3. Namna gani wazazi wanaweza kutumia hadisi na mazoezi chini ya kichwa “Miradi ya Ibada ya Familia”?
3 Miradi ya Ibada ya Familia: Sehemu hizo zinawasaidia wazazi kujifunza na watoto wao. Ili kujifunza namna ya kutumia hadisi na mazoezi, finyanga alama ya kupakua, kisha usome sehemu “Mwongozo kwa Wazazi” kuhusu kila muradi. Tumia mazoezi ya picha, kama vile ukurasa wa kupaka rangi, ili kuwafundisha watoto wadogo. Uwasaidie watoto wenye kukomaa wamalize mazoezi ya kujifunza. Mazoezi yaliyo katika kila sehemu yanazungumuzia hadisi ao somo lilelile la Biblia. Kwa hiyo, watoto wa kila umri wanaweza kushiriki katika muradi uleule wa ibada ya familia.
4. Ni habari gani inayopatikana katika sehemu “Uwe Rafiki ya Yehova”?
4 Uwe Rafiki ya Yehova: Video, nyimbo, na mazoezi katika sehemu hii ya adresi yetu ya Internete vinasaidia wazazi kukazia Neno la Mungu katika mioyo ya watoto wao wadogo. (Kum. 31:12) Kila video fupi inafundisha somo la maana. Kwa kufungua neno Mazoezi utapata sehemu zinazokazia maana ya masomo hayo. Kwa kawaida watoto wanapenda kuimba, na pia, nyimbo zinawasaidia kukumbuka mambo ambayo wamejifunza, kwa hiyo, nyimbo za Ufalme na nyimbo zilizotayarishwa hasa kwa ajili ya watoto zinatiwa kwa ukawaida kwenye adresi yetu ya Internete.
5. Sababu gani wazazi wanapaswa kumuomba Yehova awasaidie kuwafundisha watoto wao kweli?
5 Wazazi, Yehova anataka mupate matokeo mazuri munapowafundisha watoto. Kwa hiyo, mumuombe awasaidie kuwafundisha watoto wenu kweli. (Amu. 13:8) Kwa musaada wa Yehova, munaweza kuwazoeza watoto wenu ili wawe ‘wenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.’—2 Tim. 3:15; Met. 4:1-4.