Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 12
“Tunawatembelea watu ili kuzungumuza nao juu ya habari inayoweza kusaidia familia yao. Wazazi wengi wanataka watoto wao wamupende Mungu. Unawaza wazazi ndio wanapaswa kufundisha watoto wao kumupenda Mungu, ao watoto wanapaswa kujifunza peke yao?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 12, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo lenye linafuata.
Munara wa Mulinzi 01/12
“Tunawatembelea watu ili kuzungumuza nao kwa muda mufupi juu ya Mungu. Tunajua kwamba watu wana mawazo tofauti juu ya Mungu. Unafikiri watu wengi wanamuona kuwa nguvu tu ao rafiki anayewahangaikia? [Acha mutu ajibu.] Andiko hili linaonyesha kwamba Mungu anapenda tuwe marafiki wake. [Soma Yakobo 4:8a.] Gazeti hili linaonyesha mambo tatu ambayo tunapaswa kufanya ili tumukaribie Mungu.”
Amuka! Mwezi wa 12
“Tunatembelea watu ili kuzungumuza nao kwa muda mufupi juu ya tatizo la afya ambalo linasumbua watu wengi. Shirika la Afya Duniani Pote (OMS) limeonyesha kwamba mutu mumoja kati ya watu ine atapatwa na magonjwa ya akili, kama vile kushuka moyo, wakati fulani katika maisha yake. Unawaza magonjwa ya akili yanaendelea kuwapata watu wengi zaidi? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatuahidi kwamba wakati unaokuja watu hawatapatwa tena na magonjwa wala maumivu. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Gazeti hili linazungumuzia mambo fulani ambayo kila mutu anapaswa kujua juu ya magonjwa ya akili.”