Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Mwezi wa 3 uku. 4
  • Ayubu Aliendelea Kuwa Mushikamanifu Wakati Alijaribiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ayubu Aliendelea Kuwa Mushikamanifu Wakati Alijaribiwa
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Sitaacha Uaminifu-Mushikamanifu Wangu!”
    Tuige Imani Yao
  • Yobu Anaendelea Kuwa Mushikamanifu
    Biblia—Iko na Habari Gani?
  • Endelea Kuwa Muaminifu-Mushikamanifu!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • “Umutumainie Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
mwb16 Mwezi wa 3 uku. 4

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | AYUBU 1-5

Ayubu Aliendelea Kuwa Mushikamanifu Wakati Alijaribiwa

Kutoka mbinguni, Shetani anaangalia Ayubu

Ayubu aliishi katika inchi ya Usi wakati Waisraeli walikuwa watumwa katika inchi ya Misri. Hata kama hakukuwa Muisraeli, Ayubu alikuwa muabudu muaminifu wa Yehova. Alikuwa na familia kubwa, mali nyingi, na aliheshimiwa sana katika eneo lake. Alijulikana kuwa mushauri mukubwa na mwenye kuhukumu pasipo upendeleo. Alisaidia masikini na watu wenye walikuwa katika uhitaji. Ayubu alikuwa mwanaume mushikamanifu.

Ayubu alionyesha wazi-wazi kwamba Yehova alikuwa Mutu wa maana sana katika maisha yake

1:8-11, 22; 2:2-5

  • Shetani alitambua ushikamanifu wa Ayubu. Shetani hakukataa kwamba Ayubu ni mwaminifu kwa Yehova; lakini, alitilia shaka nia ao sababu yenye ilimusukuma Ayubu kuwa mwaminifu kwa Mungu

  • Shetani alisema kwamba Ayubu alimutumikia Yehova kwa sababu ya faida yake mwenyewe

  • Ili kujibu mashitaka ya Shetani, Yehova alimuruhusu Shetani amujaribu mwanaume huyo muaminifu. Shetani alishambulia Ayubu katika kila jambo

  • Wakati Shetani aliona kwamba Ayubu aliendelea kuwa mushikamanifu, alitilia shaka ushikamanifu wa kila mutu

  • Ayubu hakutenda zambi ao kusema kwamba Mungu alifanya jambo la mubaya

Ayubu anapambana na magumu katika nyumba yake
    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine