UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | ZABURI 45-51
Yehova Hataachilia Mutu Mwenye Kuvunjika Moyot
Daudi aliandika zaburi ya 51 kisha nabii Nathani kumuonyesha zambi kubwa yenye alifanya na Bath-sheba. Zamiri ya Daudi ilimusumbua sana, kwa hiyo alitubu kwa unyenyekevu.—2Sam 12:1-14.
Daudi alifanya zambi lakini angeweza kurudilia tena hali muzuri ya kiroho
Mbele akubali na kutubu zambi zake, zamiri yake ilimufanya akose furaha
Aliumia sana kwa sababu hakukubaliwa tena na Mungu mupaka akajisikia kama mifupa yake imevunjwa-vunjwa
Alitamani kusamehewa, kuwa tena na hali muzuri ya kiroho, na kupata tena furaha yake
Alimuomba Yehova kwa unyenyekevu amupatie moyo wenye kuwa tayari kutii
Alikuwa hakika kama Yehova atamusamehe