MAISHA YA MUKRISTO
Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kurudilia Watu
SABABU GANI NI LAZIMA: Watu wengi wenye wanapendezwa na ujumbe wa Ufalme wanatafuta kujua kweli juu ya Mungu. (Isa 55:6) Ili kuwafundisha, tunapaswa kuendelea kuwarudilia. Watu wanapata matatizo mbalimbali; kwa hiyo, tunapaswa kubadilisha namna ya kuchochea kupendezwa kwao. Lakini tunaweza kupata matokeo ya muzuri kama tunajitayarisha muzuri, na kama tuko na mupango wa kuanzisha funzo la Biblia kila mara wakati tunarudilia mutu.
NAMNA YA KUFANYA:
Ujikaze ili usikawie kuwarudilia watu. —Mt 13:19
Ukuwe mwenye urafiki na mwenye heshima. Ujikaze kutulia
Anza kwa kusalimia mutu kwa furaha. Umuite kwa jina lake. Umukumbushe sababu gani umemurudilia; pengine ni juu ya kujibia ulizo fulani, kumuletea gazeti la mupya, kumuonyesha adresi yetu ya Internete, kumuonyesha video fulani, ao kumuonyesha namna tunajifunzaka Biblia na watu. Kama musikilizaji anapenda muzungumuzie habari ingine, ubadilishe habari yako.—Flp 2:4
Muangia maji mbegu ya kweli yenye imepandwa katika moyo wake kwa kumusomea andiko ao kwa kumuachia kichapo fulani. (1Kor 3:6) Ujikaze ili muelewane naye
Umutayarishe ili kumutembelea tena