UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 8-9
Farao Mwenye Kiburi Anasaidia Kutimiza Kusudi la Mungu Bila Kujua
Mafarao Wamisri walijiona kuwa miungu. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini Farao alikuwa na kiburi sana mupaka akakataa kusikiliza Musa na Haruni na hata makuhani wake wenye kufanya uchawi.
Unasikilizaka wakati wengine wanatoa mapendekezo? Unakuwaka mwenye Shukrani wakati mutu fulani anakupatia mashauri? Ao sikuzote unaonaka kama hauwezi kukosea? “Kiburi kinatangulia kuanguka.” (Mez 16:18) Kwa kweli, ni jambo la maana sana kuepuka kuwa na kiburi!