UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 10-11
Musa na Haruni Wanaonyesha Uhodari Mukubwa
Musa na Haruni walionyesha uhodari mukubwa wakati walikuwa wanaongea na Farao, mutu mwenye alikuwa na mamlaka zaidi katika dunia ile wakati. Nini njo iliwasaidia kufanya vile? Biblia inasema hivi kuhusu Musa: “Kwa imani alitoka Misri, lakini bila kuogopa kasirani ya mufalme, kwa maana aliendelea kuwa imara kama mutu mwenye anamuona Ule mwenye haonekane.” (Ebr 11:27) Musa na Haruni walikuwa na imani yenye nguvu katika Yehova na walimutegemea.
Ni hali gani zenye zinaomba kuonyesha uhodari ili kutetea imani yako bila woga mbele ya mutu fulani mwenye kuwa na mamlaka?