MAISHA YA MUKRISTO
Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuhubiri Kupitia Kamera ao Enterfone
JUU YA NINI NI LAZIMA KUFANYA VILE: Maendeleo ya teknolojia na kuongezeka kwa mambo ya kuuana, vinafanya watu fulani watie kamera ao enterfone mu manyumba yao ili wakuwe wanazungumuza na watu wenye kuwa inje. Pengine unaweza kuogopa kuhubiria mutu mwenye hauone lakini yeye iko anakuona. Mambo yenye kufuata inaweza kutusaidia tufanye vile bila wasiwasi. Ni vile pia tunaweza kufanya wakati tuko nahubiri kupitia telefone.
NAMNA YA KUFANYA VILE:
Usiwaze kama watu hawatakusikiliza. Watu mingi wenye kuwa na kamera ao enterfone wanapendaka kuzungumuza na siye
Ujue kama kamera fulani zinaweza kukurekodi mbele hata upige kengele ya mulango, na mutu anaweza kukuona na kusikia mambo yenye uko nasema wakati tu unakuwa karibu na mulango
Wakati mutu anajibia, usemee ku ile enterfone ao ku kamera sawa vile tu uko nasema naye uso kwa uso. Unaweza kucheka na kufanya ishara kama kawaida. Sema tu namna ungesema kama angekuwa mbele yako. Sura yako isikuwe karibu sana na kamera wakati uko nasema. Kama mutu hajibie usimuachie ujumbe wenye kurekodiwa
Hata kisha kumaliza kuzungumuza naye, usisahau kama anaweza kuendelea kukuona na kusikia mambo yenye uko nasema