Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp22 na. 1 uku. 10-11
  • 3 | Utoshe Mawazo ya Chuki mu Akili Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 3 | Utoshe Mawazo ya Chuki mu Akili Yako
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fundisho ya Biblia:
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya:
  • Stefano​—“Akiwa Amekubaliwa na Mungu na Akiwa Amejaa Nguvu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Namna ya Kuachana na Chuki
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Tunaweza Kuachana na Chuki!
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Juu ya Nini Chuki Iko Naendelea?
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
wp22 na. 1 uku. 10-11
Mwanaume mumoya iko najiwazia namna iko nasalimiana na mutu wa rangi ingine. Kwenye kivuli yao wako nabishana na wanakamata alama zenye kuonyesha kama wanapinga mawazo fulani.

NAMNA YA KUACHANA NA CHUKI

3 | Utoshe Mawazo Ya Chuki Mu Akili Yako

Fundisho ya Biblia:

“Mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.”​—WAROMA 12:2.

Ile Iko na Maana Gani?

Mungu anahangaikiaka mawazo yetu. (Yeremia 17:10) Ni kweli kwamba tunapaswa kuepuka kusema ao kufanya jambo fulani yenye inachochea chuki, lakini hatupaswe kuishia pale. Juu chuki inaanziaka mu akili na mu moyo wa mutu, tunapaswa kabisa kutosha mawazo ya chuki mu akili na mu moyo wetu. Ni ile tu njo itatusaidia ‘tugeuzwe,’ ni kusema tubadilike na tuachane kabisa na chuki.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya:

Ujichunguze sana ili uone kama uko na mawazo gani juu ya watu wengine, zaidi sana watu wa rangi ingine ya ngozi na wa inchi ingine. Ujiulize hivi: ‘Ninawaonaka namna gani? Mawazo yangu inachochewa na mambo yenye ninajua kuwahusu, ao mambo yenye watu wanasemaka kuwahusu?’ Epuka site za Enternete za kupashana habari, filme, ao mambo ya kujifurahisha yenye inachochea chuki na jeuri.

Neno ya Mungu inaweza kutusaidia tutoshe mawazo ya chuki mu akili yetu na mu moyo wetu

Haikuwake mwepesi kila mara kuchunguza mawazo yetu kwa kusudi ya kubadilika. Lakini Neno ya Mungu inaweza kutusaidia “kutambua mawazo na makusudio ya moyo.” (Waebrania 4:12) Kwa hiyo, endelea kujifunza Biblia. Ulinganishe mawazo ya Biblia na mawazo yako, na kisha ujikaze kabisa kupatanisha mawazo yako na mambo yenye Biblia inafundisha. Neno ya Mungu inaweza kutusaidia tuachane na chuki, hata yenye ‘ilishatia mizizi kabisa’ mu akili na mu moyo wetu.​—2 Wakorinto 10:4, 5.

Habari ya Kweli​—STEPHEN

Alibadilisha Mawazo Yake

Stephen.

Stephen na watu wa familia yake walikuwaka nachukiwa na wazungu. Ile ilifanya ajiunge na kikundi moya ya politike yenye ilikuwa napigania haki za wanadamu. Wakati fulani, yeye mwenyewe alikuwa natendea watu mubaya juu aliwachukia. Stephen anasema hivi: “Siku moya, miye na marafiki wangu tulionaka filme yenye inaonyesha mateso ya watumwa wa Afrika, wenye walipelekwaka Amerika. Tulikasirika sana na tulianza kupiga vijana wazungu wenye walikuwa mu ile jumba ya kuonyeshea filme. Kisha tulienda mu manyumba ya wazungu, yenye ilikuwa pale karibu, juu ya kutafuta watu wengine wenye tungepiga.”

Mawazo ya Stephen ilibadilika kabisa wakati alianza kujifunza Biblia pamoya na Mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Juu nilizoea kuona namna watu wako nabagua watu wa rangi ingine ya ngozi, nilishangala sana kuona namna Mashahidi wa Yehova walikuwa natendeana. Kwa mufano, wakati Shahidi moya muzungu alisafiri, aliacha watoto wake mu familia ya watu weusi juu wawachunge. Tena, familia moya ya wazungu ilibebaka mutoto moya mweusi mwenye hakukuwa na fasi ya kuishi, na wakaanza kuishi naye.” Stephen alifikia kuwa hakika kabisa kama Mashahidi wa Yehova njo Wakristo wa kweli. Juu wako na upendo kati yao, sawa vile Yesu alisemaka.​—Yohana 13:35.

Ni nini ilimusaidia Stephen aache kuchukia watu na kuwatendea mubaya? Ni andiko ya Waroma 12:2. Anasema hivi: “Nilianza kutambua kama nilipaswa kubadilisha mawazo yangu. Iliomba nifanye vile juu niishi kwa amani pamoya na watu, lakini pia juu njo ilikuwa namna ya muzuri sana ya kuishi.” Kwa zaidi ya miaka 40 sasa, Stephen hakuwake tena nachukia watu.

Ukipenda kujua mambo mingi juu ya Stephen, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 7, 2015, ukurasa wa 10-11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine