PENDEKEZO JUU YA MAMBO YA KUJIFUNZA
Watu Waaminifu Wanatimizaka Naziri Zao
Soma Waamuzi 11:30-40 juu uone mambo yenye mufano wa Yefta na mutoto wake mwanamuke inaweza kukufundisha kuhusu kutimiza naziri.
Chunguza habari yote. Waisraeli waaminifu waliona namna gani naziri zenye walimutolea Yehova? (Hes. 30:2) Namna gani Yefta na mutoto wake mwanamuke walionyesha kama walikuwa na imani kwa Yehova?—Amu. 11:9-11, 19-24, 36.
Ujifunze mambo mingi zaidi. Inawezekana Yefta alikuwa nafikiria nini wakati alifanya naziri? (w16.04 7 fu. 12) Yefta na mutoto wake walijiima mambo gani juu ya kutimiza naziri? (w16.04 7-8 fu. 14-16) Leo Wakristo wanaweza kufanya naziri gani?—w17.04 5-8 fu. 10-19.
Umejifunza nini? Ujiulize hivi:
‘Ni nini inaweza kunisaidia niendelee kutimiza naziri yangu ya kujitoa kwa Mungu?’ (w20.03 13 fu. 20)
‘Ninaweza kujiima mambo gani juu ya kumutumikia Yehova zaidi?’
‘Nini inaweza kunisaidia niendelee kuheshimia naziri yangu ya ndoa?’ (Mt. 19:5, 6; Efe. 5:28-33)