HABARI YA KUJIFUNZA YA 16
WIMBO 87 Tunatiana Moyo ku Mikutano
Kukaribia Bandugu na Badada Yetu Ni Jambo ya Muzuri Kwetu!
“Angalia! Ni muzuri sana na inapendeza sana ndugu kukaa pamoja kwa umoja!”—ZB. 133:1.
WAZO KUBWA
Mambo yenye tunaweza kufanya juu ya kukaribia bandugu na badada yetu, na baraka zenye tutapata wakati tunafanya urafiki na waabudu wenzetu.
1-2. Yehova anahangaikia sana nini, na anapenda tufanye nini?
YEHOVA anahangaikia sana namna tunatendea waabudu wenzetu. Yesu alifundisha kama tunapaswa kupenda jirani yetu sawa vile tunajipenda siye wenyewe. (Mt. 22:37-39) Ni kusema tunapaswa kutendea muzuri hata batu benye habaamini mambo yenye tunaamini. Kama tunafanya vile, tunamuiga Yehova Mungu mwenye “anaangazia jua lake watu waovu na watu wazuri, tena ananyesha mvua juu ya wenye haki na wenye hawako wenye haki.”—Mt. 5:45.
2 Ni kweli kama Yehova anapenda banadamu bote, lakini anapenda sana benye banafanya mambo ya muzuri. (Yoh. 14:21) Anapenda tumuige. Anatuomba tuonyeshe bandugu na badada yetu “upendo mwingi” na “upendo wenye upole.” (1 Pe. 4:8; Ro. 12:10) Upendo wenye upole ni upendo wenye tunaonyeshaka batu ya familia ao rafiki wa karibu.
3. Tunapaswa kukumbuka nini juu ya upendo?
3 Sawa vile tunapaswa kuhangaikia mimea ya mu shamba yetu juu ikomale, tunapaswa kuendelea kujikaza juu upendo wetu kwa bandugu na badada uendelee kukomala. Mutume Paulo alishauria Wakristo hivi: “Upendo wenu wa kindugu uendelee.” (Ebr. 13:1) Yehova anapenda tuendelee kukomalisha upendo wetu kwa ajili ya bengine. Hii habari inaonyesha juu ya nini tunapaswa kukaribia waabudu wenzetu na namna tunaweza kuendelea kufanya vile.
JUU YA NINI TUNAPASWA KUKARIBIA BANDUGU NA BADADA YETU
4. Sawa vile Zaburi 133:1 inaonyesha, tunaweza kufanya nini juu tuendelee kuona umoja wetu kuwa jambo ya pekee? (Ona pia picha.)
4 Soma Zaburi 133:1. Mwenye aliandika hii zaburi alisema kama kufanya urafiki na benye banamupenda Yehova ni “muzuri” na “inapendeza.” Na siye tunakubaliana naye. Lakini, juu tunaonanaka sana na bandugu na badada yetu, pengine hata mara mingi ku juma, tunaweza kuanza kuona umoja wetu wa Kikristo kuwa jambo ya kawaida tu. Iko sawa vile mutu mwenye anazoea kuona muti ya kabambi na ya kushangaza sana. Juu anaionaka sana, anaweza kuanza kuona kuwa ni ya kawaida tu. Tunaweza kufanya nini juu ile isitufikie na tuendelee kuona bandugu yetu kuwa ba maana? Tunapaswa kufikiria namna kila mumoya wabo ni wa maana mu kutaniko na ni wa maana kwetu. Tukifanya vile upendo wetu kwao utaendelea kuongezeka.
Kamata kwa uzito umoja wetu wa Kikristo, usiuone kuwa kitu ya bure-bure (Ona fungu ya 4)
5. Kuonyesha bandugu na badada yetu upendo kunaweza kuwa na matokeo gani juu ya bengine?
5 Wakati batu fulani banafika ku mikutano yetu kwa mara ya kwanza banaguswa sana saa banaona upendo wenye tunaonyeshana. Ile tu inaweza kufanya baone kama bamepata kweli. Yesu alisema hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu—kama muko na upendo kati yenu.” (Yoh. 13:35) Ona mufano wa Chaithra, mwanafunzi ku masomo ya juu mwenye alikuwa najifunza Biblia pamoya na Mashahidi wa Yehova. Aliitika mualiko wa kuenda ku mukusanyiko wa eneo. Kisha kukusanyika siku ya kwanza ya mukusanyiko, aliambia hivi mwalimu wake wa Biblia: “Bazazi yangu habayanikumbatiaka hata siku moya. Lakini ku mukusanyiko wenu, mu siku moya tu balinikumbatia mara 52.” Chaithra alifanya maendeleo na alibatizwa mu 2024. Kwa kweli, wakati wapya wanaona matendo yetu ya muzuri, kwa mufano namna tunaonyeshana upendo, ile inabachochea bapende kumutumikia Yehova.—Mt. 5:16.
6. Namna gani kuwa karibu na bandugu na badada yetu kunatulinda?
6 Kukaribia bandugu na badada yetu kunaweza kutulinda. Paulo alishauria Wakristo wenzake hivi: “Muendelee kutiana moyo kila siku, . . . ili mutu yeyote kati yenu asifanywe kuwa mugumu kwa nguvu za udanganyifu za zambi.” (Ebr. 3:13) Kama tunavunjika moyo sana mupaka tunaanza kushindwa kufanya mambo ya muzuri, Yehova anaweza kutumikisha mutumishi wake fulani mwenye anatambua ile jambo juu atupatie musaada wenye tuko nao lazima. (Zb. 73:2, 17, 23) Na ile inaweza kutusaidia sana.
7. Namna gani upendo unafanya tukuwe na umoja? (Wakolosai 3:13, 14)
7 Bandugu na badada yetu banafanya yote yenye banaweza juu ya kuonyeshana upendo, na ile inatuletea baraka mingi. (1 Yo. 4:11) Kwa mufano, upendo unatuchochea ‘tuendelee kuvumiliana,’ na ile inafanya tukuwe na umoja. (Soma Wakolosai 3:13, 14; Efe. 4:2-6) Njo maana ku mikutano yetu kunakuwaka hali ya kufurahisha yenye hauwezi kupata fasi ingine mu dunia.
TUONYESHANE HESHIMA
8. Namna gani Yehova anatusaidia tukuwe na umoja?
8 Umoja wenye tuko nao mu dunia yote ni muujiza. Hata kama hatukamilike, Yehova anatuwezesha kuwa na umoja. (1 Ko. 12:25) Biblia inasema kama ‘tumefundishwa na Mungu kupendana.’ (1 Te. 4:9) Ni kusema, kupitia Maandiko, Yehova anatuonyesha mambo yenye tunapaswa kufanya juu tukaribiane. ‘Tunafundishwa na Mungu’ wakati tunachunguza kwa uangalifu mafundisho yake na kuitumikisha. (Ebr. 4:12; Yak. 1:25) Mashahidi wa Yehova wanajikazaka sana kufanya vile.
9. Waroma 12:9-13 inatufundisha nini juu ya namna ya kuonyeshana heshima?
9 Namna gani Neno ya Mungu inatufundisha kukaribiana? Ona mambo yenye mutume Paulo alisema juu ya ile mu Waroma 12:9-13. (Soma.) Maneno yenye tutakazia akili ni hii: “Katika kuonyeshana heshima, mukuwe wa kwanza.” Maana yake nini? Tunapaswa kukamata hatua ya kuonyesha bengine “upendo wenye upole” kwa kuwa tayari kusamehe, kuwa wakaribishaji-wageni, kuwa wakarimu, na mambo ingine. (Efe. 4:32) Usichunge ndugu yako ao dada yako njo akukaribie, ‘ukuwe wa kwanza’ kufanya vile. Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”—Mdo. 20:35.
10. Namna gani tunaweza kuonyesha bidii “katika kuonyeshana heshima”? (Ona pia picha.)
10 Kisha tu kusema kama tunapaswa kuwa wa kwanza kuonyesha bengine heshima, Paulo alitushauria ‘tukuwe wenye bidii, hapana wavivu.’ Mutu mwenye bidii ni mutu mwenye anatumikaka sana. Kama banamupatia kazi, anaifanya muzuri sana. Mezali 3:27, 28 inatushauria hivi: “Usiime mema wale wenye unapaswa kutendea mema kama uko na uwezo wa kusaidia.” Njo maana kama tunaona mutu iko na lazima ya musaada, tunafanya yetu yote juu ya kumusaidia. Hatujiambie kama tutamusaidia wakati ingine ao kuwaza kama mutu mwingine njo atamusaidia.—1 Yo. 3:17, 18.
Tunapaswa kukamata hatua ya kusaidia bandugu na badada yetu wakati biko na lazima ya musaada (Ona fungu ya 10)
11. Nini njo inaweza kutusaidia tukaribiane?
11 Njia ingine ya kuonyesha bengine heshima ni kuwa tayari kubasamehe wakati banatukosea. Waefeso 4:26 inasema: “Musitende zambi; jua lisishuke wakati mungali katika kasirani.” Juu ya nini? Mustari wa 27 unasema kama kufanya vile kunaweza ‘kumupatia Ibilisi nafasi.’ Yehova anatuambia tena na tena mu Neno yake tusameheane. Wakolosai 3:13 inatushauria ‘tuendelee . . . kusameheana kwa kupenda.’ Kuachilia makosa ya bandugu na badada yetu wakati banatukwaza ni kati ya mambo yenye inafanyaka tukaribiane sana. Wakati tunafanya vile, tunasaidia “kuendeleza umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Efe. 4:3) Kwa kifupi, kusamehe kunaletaka umoja na amani.
12. Namna gani Yehova anatusaidia juu tuweze kusamehe?
12 Kusema kweli, inaweza kuwa nguvu kusamehe wakati banatuumiza. Lakini kwa musaada wa roho ya Mungu, tutaweza. Kisha kutushauria ‘tukuwe na upendo wenye upole kwa mutu na mwenzake’ na ‘tukuwe wenye bidii,’ Maandiko inatuomba hivi: “Muwake roho.” Mutu mwenye ‘anawaka roho’ ni mutu mwenye roho ya Mungu inachochea akuwe na bidii mingi sana. (Ro. 12:11) Kwa hiyo, roho ya Mungu inaweza kutusaidia kuonyeshana upendo wenye upole na kusameheana kwa kupenda. Njo maana tunamuomba Yehova kwa moyo wote atupatie roho yake takatifu.—Lu. 11:13.
“KUSIKUWE MIGAWANYIKO KATI YENU”
13. Ni nini inaweza kuleta migawanyiko kati yetu?
13 Mu kutaniko muko “watu wa namna zote” wenye wanatoka mu desturi tofauti-tofauti. (1 Ti. 2:3, 4) Juu tuko tofauti tunaweza kukamata maamuzi tofauti mu mambo ya kipekee sawa vile mu namna ya kuvala na kujipamba, mu mambo ya matunzo, ao mu mambo ya kujifurahisha. Kama hatuko baangalifu, ile inaweza kuleta migawanyiko mu kutaniko. (Ro. 14:4; 1 Ko. 1:10) Juu Mungu ametufundisha kupendana, tunapaswa kuwa baangalifu juu tusionyeshe kama mambo yenye siye tunachagula njo ya muzuri zaidi kupita ya bengine.—Flp. 2:3.
14. Tunapaswa kujikaza kufanya nini, na juu ya nini?
14 Tunaweza pia kuepuka kuleta migawanyiko kama tunajikaza kutendea muzuri bengine mu kutaniko na kubatia moyo kila wakati. (1 Te. 5:11) Wakati batu benye habatende tena ao benye baliondolewa mu kutaniko banamurudilia Yehova, tunabakaribisha kwa furaha! (2 Ko. 2:8) Ona mambo yenye ilifikia dada moya mwenye alifika ku Jumba ya Ufalme kisha kufanya miaka 10 na hatende tena. Anasema hivi: “Balinisalimia kwa furaha na kunipatia mukono kwa uchangamufu.” (Mdo. 3:19) Ile matendo ya kidogo tu ilifanya ajisikie namna gani? Anasema hivi: “Ilifanya nijisikie sawa vile mukono wa Yehova ulikuwa naniongoza juu nikuwe tena na furaha.” Kama tunajikaza kutia bengine moyo, Yesu anaweza kututumikisha juu ya kusaidia “wenye kuteseka na wenye kulemewa na mizigo.”—Mt. 11:28, 29.
15. Nini ingine njo inasaidiaka kuendeleza umoja? (Ona pia picha.)
15 Maneno yetu inaweza pia kusaidia kuendeleza umoja. Yobu 12:11 inasema hivi: “Je, sikio halipime maneno kama vile ulimi unaonja chakula?” Mutu mwenye iko napiga chakula anaonjaka kwanza juu ahakikishe kama iko butamu mbele ya kuipatia bengine. Vilevile, ni muzuri kuwaza kwanza juu ya mambo yenye tunatafuta sema mbele ya kuisema. (Zb. 141:3) Kusudi yetu ni kutafuta kujua ikiwa mambo yenye tutasema itatia moyo na italetea ‘faida wale wenye wanaisikia.’—Efe. 4:29.
Fikiria mambo yenye utasema mbele ya kuisema (Ona fungu ya 15)
16. Ni ba nani njo banapaswa kuwa baangalifu sana juu ya maneno yabo?
16 Siye bote tunapaswa kuwa baangalifu juu ya mambo yenye tunasema, zaidi sana bwana na pia bazazi. Banapaswa kuwa baangalifu sana juu maneno yabo ikuwe ya kutia moyo. (Kol. 3:19, 21; Tit. 2:4) Bazee ni bachungaji ba kondoo wa Yehova, njo maana banapaswa pia kila mara kutumia maneno ya kutia moyo na yenye kufariji. (Isa. 32:1, 2; Gal. 6:1) Mezali moya ya Biblia inatukumbusha hivi: “Neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa—ni la muzuri sana!”—Mez. 15:23.
PENDA “KWA TENDO NA KWELI”
17. Tunaweza kufanya nini juu tupende bandugu na badada yetu kwa moyo wote?
17 Mutume Yohana anatutia moyo ‘tupendane, hapana kwa neno ao kwa ulimi, lakini kwa tendo na kweli.’ (1 Yo. 3:18) Tunapaswa kupenda bandugu na badada yetu kwa moyo wote. Tunaweza kufanya vile namna gani? Kupitisha wakati pamoya na ndugu na dada zetu kunafanya tukaribiane sana na tupendane sana. Kwa hiyo tafuta nafasi za kupitisha wakati na bengine ku mukutano na mu mahubiri. Tembelea bengine. Kama tunafanya vile, tunaonyesha kama ‘tumefundishwa na Mungu kupendana.’ (1 Te. 4:9) Na tutaendelea kujionea namna “ni muzuri sana na inapendeza sana ndugu kukaa pamoja kwa umoja!”—Zb. 133:1.
WIMBO 90 Tutiane Moyo