HABARI JUU YA MAISHA YA WATU
Yehova Alitusaidia Tukomale Kwenye ‘Balitupanda’
“UKOMALE kwenye banakupanda” ile shauri inaweza kushangaza sana. Mats na bibi yake Ann-Catrin ba mu inchi ya Suede “balipandwa” mara mingi. Namna gani balitumikisha ile shauri, na ilibasaidia namna gani?
Mats na Ann-Catrin balisoma masomo ya Gileadi mu 1979, na kwa miaka mingi “bamepandwa” ni kusema bametumwa fasi mbalimbali. Balitumikia Iran, Maurice, Myanmar, Tanzania, Uganda, na Zaire. Ku Gileadi njo mwalimu moya, Jack Redford, alibapatiaka ile shauri yenye ilibasaidia wakati “balibapanda,” “bakabaongola,” na “kubapanda tena” mara mingi. Tuache batuelezee.
Mutuambie mulipata kweli namna gani.
Mats: Baba yangu aliishi Poland mu Vita ya Pili ya Ulimwengu na aliona unafiki wa kanisa ya Katoliki. Lakini alizoea kusema, “Kweli inapaswa tu kuwa fasi fulani!” Kisha wakati, niliamini kabisa kama alisema kweli. Niliuza bitabu bya mingi byenye bilikuwa bilishatumikishiwa. Mu bile bitabu mulikuwa kitabu moya ya rangi ya bleu yenye kichwa Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele. Kichwa ya ile kitabu ilinipatia hamu ya kuisoma, na nilisoma ile kitabu yote ileile busiku na kufikia asubui nilijua kama nimepata kweli!
Kuanzia Mwezi wa 4, 1972, nilisoma bitabu mingi bya Mashahidi wa Yehova na nilipata majibu ya maulizo yangu. Nilijisikia sawa vile ule mufanyabiashara mwenye Yesu alizungumuzia mu mufano wake. Kisha kupata lulu ya bei, aliuzisha kila kitu juu aiuze. Na miye “niliuzisha” mipango yangu yote, ni kusema niliachana na mipango yangu ya kusoma masomo ya kuwa munganga juu niuze “lulu,” ni kusema kweli yenye nilikuwa nimepata. (Mt. 13:45, 46) Nilibatizwa tarehe 10, Mwezi wa 12, 1972.
Mu mwaka moya tu, bazazi yangu na muloko yangu baliitika pia kweli na bakabatizwa. Mu Mwezi wa 7, 1973, nilianza utumishi wa wakati wote. Mu kutaniko yetu mulikuwa bapainia ba bidii sana, kati yabo kulikuwa dada moya wa kiyana na wa kiroho, jina yake ilikuwa Ann-Catrin. Tulipendana na tukaoana mu 1975. Miaka ine yenye ilifuata tuliishi mu muji wa Strömsund, mu inchi ya Suede. Ilikuwa fasi ya kupendeza, kwenye batu mingi balipenda kujua kweli.
Ann-Catrin: Baba yangu alijifunza kweli wakati alikuwa karibu kumaliza masomo ya juu mu muji wa Stockholm. Ile wakati nilikiwa tu na miezi tatu, lakini alikuwa naenda na miye ku mikutano na mu mahubiri. Mama yangu hakufurahi na alijaribu kuonyesha kama Mashahidi wa Yehova wanasemaka bongo. Lakini hakuweza. Kwa hiyo kisha wakati naye alibatizwa. Nilibatizwa wakati nilikuwa na miaka 13, na nilianza upainia wakati nilikuwa na miaka 16. Kisha kutumikia Umeå, kwenye kulikuwa lazima ya wahubiri, nikakuwa painia wa pekee.
Kisha miye na Mats kuoana, tulifurahi kusaidia batu mingi bajue kweli. Kati yabo kulikuwa kijana mwanamuke mwenye kuitwa Maivor. Maivor aliachana na muchezo fulani wenye alikuwa nafanya; aliuacha juu aweze kumutumikia Yehova zaidi. Alianza kufanya kazi ya upainia pamoya na muloko yangu mwanamuke. Maivor na muloko yangu balisoma masomo ya Gileadi mu 1984 na biko bamisionere mu Equateur.
Mu kazi yenu ya umisionere, namna gani mulifuata shauri ya ‘kukomala kwenye banabapanda’?
Mats: “Balitupanda” tena na tena mu migao ya mupya. Lakini tulifanya yetu yote juu mizizi yetu “ibakie” katika Yesu, ni kusema tulijikaza kumuiga Yesu, zaidi sana sifa yake ya unyenyekevu. (Kol. 2:6, 7) Kwa mufano, wakati balikuwa natutuma mu eneo fulani, hatukutazamia kama bandugu ba kule batafanya mambo vile siye tunazoea kufanya, lakini tulijikaza kuelewa namna yabo ya kufanya mambo. Tulipenda kuelewa namna yabo ya kuona mambo na desturi yabo. Vile tulimuiga Yesu, ni vile tulijisikia sawa vile ‘tunapandwa pembeni ya mito midogo ya maji’ juu tuweze kukomala fasi yote kwenye banatupanda.—Zb. 1:2, 3.
Tulikuwa nasafikiri sana saa tulikuwa Zaire
Ann-Catrin: Kama banaongola muti kisha banaipanda tena, ile muti iko na lazima ya jua. Sikuzote Yehova amekuwa “jua” kwetu. (Zb. 84:11) Yehova ametubariki kwa kutupatia familia ya bandugu na dada benye upendo. Kwa mufano, mu kutaniko yetu ya kidogo mu Tehran, mu inchi ya Iran, bandugu na dada balituonyesha ukarimu wa sana, sawa tu wenye kuzungumuziwa mu Biblia. Tulipenda tubakie Iran, lakini mu Mwezi wa 7, 1980, Mashahidi wa Yehova walikatazwa mu ile inchi, na bakubwa ya inchi balitupatia saa 48 juu tutoke kule. Tulitumwa Zaire (yenye inaitwa leo Congo) mu Afrika.
Tungali nakumbuka wakati ya muzuri yenye tulipitisha Zaire, 1982
Saa tu nilisikia kama tutaenda mu Afrika, nililia. Mambo yenye nilikuwaka nilishasikia juu ya manyoka na magonjwa mu Afrika, iliniogopesha. Lakini barafiki yetu bawili benye balitumikia mu Afrika kwa miaka mingi balituambia hivi: “Musiogope, hamuyafikaka mu Afrika! Lakini tunajua kama mutapapenda.” Na kweli tulipapenda! Bandugu na badada ba mu Afrika biko na upendo na ni bachangamufu. Tulitumikia mu Zaire kwa miaka sita lakini tulipaswa kuondoka juu kazi yetu ilikatazwa kule pia. Nilijicheka wakati nilitambua kama niko sasa nasali hivi kwa Yehova, “Tafazali, tusaidie tubakie mu Afrika.”
Mumepata baraka gani?
Mwenye tulikuwa nalala mu inchi ya Tanzania, 1988
Mats: Tumefanya burafiki na bamisionere ba mingi ba kutoka fasi mbalimbali. Tena, mu maeneo fulani, tulipata furaha ya kuongoza mafunzo mingi ya Biblia. Wakati fulani kila mumoya wetu alikuwa naongoza mafunzo 20 hivi! Kitu ingine yenye siwezi kusaabu ni upendo na ukarimu wa bandugu na dada ba mu Afrika. Wakati tulikuwa natembelea makutaniko mu Tanzania, bandugu balituonyesha ukarimu “kupita uwezo wao” wakati “tulikuwa nalala” mu gari yetu pembeni ya manyumba yabo. Balikuwa nahakikisha kama tuko na kila kitu ya lazima, hata kama balikuwa maskini sana. (2 Ko. 8:3) Wakati yenye tulifurahia sana ilikuwa wakati yenye tuliita “hadisi njo.” Ile wakati njo kila siku miye na Ann-Catrin tulikuwa naikala mangaribi na kuzungumuzia mambo yenye ilipitikana muchana na kumushukuru Yehova juu alikuwa pamoya na siye.
Ann-Catrin: Miye, nimefurahia sana kujuana na bandugu na badada ba mu inchi za mingi. Tulijifunza luga za mupya, sawa vile luga ya Farsi, Kifaransa, Kiganda, na Kiswahili. Tena, tumejifunza desturi mbalimbali. Tulisaidia kuzoeza bapya, tulipata marafiki wa kweli, na tulitumika “bega kwa bega” pamoya nabo mu kazi ya Yehova.—Sef. 3:9.
Tuliona pia mambo mingi ya muzuri mu uumbaji wa Yehova. Pia wakati tulifika mu mugao wa mupya, ni sawa vile tulikuwa mu safari pamoya na Yehova na yeye njo alikuwa natuongoza. Ametufundisha mambo yenye hatungejuaka siye peke.
Tuko nahubiri mu maeneo mbalimbali ya Tanzania
Mulipata magumu gani, na ni nini imebasaidia kuvumilia?
Mats: Wakati fulani tuligonjwa magonjwa mbalimbali sawa vile malaria. Ann-Catrin alifanyiwa upasuaji mbalimbali wenye hatukutazamia. Tulikuwa pia na wasiwasi juu ya bazazi yetu benye balikuwa nazeeka. Lakini tunashukuru baloko yetu benye balikuwa pale juu ya kubahangaikia. Balibahangaikia kwa uvumilivu, kwa furaha, na kwa upendo. (1 Ti. 5:4) Hata kama tulifanya yetu yote juu ya kubahangaikia na tuko mbali, wakati fulani tulijisikia mubaya juu tungependa kufanya mingi zaidi juu ya kubasaidia.
Ann-Catrin: Mu 1983, wakati tulikuwa natumikia mu Zaire, niligonjwa kolera. Munganga aliambia Mats hivi: “Leoleo umutoshe mu hii inchi!” Siku yenye ilifuata tuliingia mu avion ya mizigo na tukarudia Suede. Ile tu njo avion yenye ilipatikana.
Mats: Tulilia sana juu tuliwaza kama kazi yetu ya umisionere inaishia pale. Hata kama munganga alisemaka kama Ann-Catrin hatajisikia muzuri, Ann-Catrin alipona. Kisha mwaka moya, tulirudia Zaire. Sasa balitutuma mu kutaniko ya kidogo ya Kiswahili mu muji wa Lubumbashi.
Ann-Catrin: Wakati tulikuwa Lubumbashi, nilibeba mimba lakini ikatoka. Hata kama hatukukuwa napanga kuwa na batoto, nilihuzunika sana saa mutoto wetu alikufa. Lakini mu ile wakati ya huzuni, Yehova alitufariji mu njia yenye hatukutazamia. Tulipata mafunzo mingi ya Biblia kuliko wakati ingine. Mbele hata mwaka moya iishe, hesabu ya bahubiri mu kutaniko yetu ilitoka ku bahubiri 35 mupaka bahubiri 70, na hesabu ya batu benye balikuwa nafika ku mikutano ilitoka ku 40 mupaka 220. Tulikuwa nahubiri sana, na Yehova alitubariki. Ile ilifanya nijisikie muzuri. Lakini wakati fulani tunakumbukaka na kuzungumuzia mutoto wetu. Tunangoya kwa hamu wakati Yehova ataponyesha kabisa mioyo yetu mu dunia mupya.
Mats: Wakati fulani, Ann-Catrin alikuwa wa kuchoka sana juu banganga balinipata na kansere ya ku sehemu fulani ya butumbutumbu, na iliomba nifanyiwe upasuaji mukubwa. Leo nilishajisikia muzuri, na Ann-Catrin iko nafanya yenye anaweza juu ya kumutumikia Yehova.
Tumeelewa kama haiko siye peke tu njo tunapataka magumu. Kisha mauaji yenye ilitokea Rwanda mu 1994, tulitembelea bandugu na dada mu kambi za bakimbizi. Hata kama balikuwa mu hali ya nguvu, balikuwa na imani ya nguvu, balivumilia, na balikuwa bakarimu sana. Ile ilitufundisha kama Yehova iko na uwezo wa kutegemeza batu yake hata bakuwe mu magumu gani.—Zb. 55:22.
Ann-Catrin: Tulipata magumu ingine wakati tulienda Uganda mu 2007 juu ya kuhuzuria programe ya kutolea Yehova biro ya tawi ya Uganda. Kisha programe, tulianza safari ya kuenda Nairobi Kenya. Tulikuwa batu 25, bamisionere na Banabeteli. Mbele tufike ku mupaka ya Kenya na Uganda, camion moya yenye ilikuwa nakuya mbele yetu, iligonga bisi yetu. Shofere na barafiki yetu batano balikufa palepale; na dada umoya alikufia ku hopitale. Tunangoya kwa hamu kubaona tena!—Yob. 14:13-15.
Nililumia lakini nilifikia kupona. Ile aksida ilituachaka na boga miye, Mats, na bandugu fulani benye balikuwaka mu ile gari. Kwa mufano, juu ya boga nilikuwa nashituka na kulamuka busiku na moyo iko napiga-piga. Bilikuwa bya kuogopesha sana. Kitu yenye ilitusaidia tutulie ni kusali na kusoma maandiko fulani yenye kufariji yenye tunapendaka sana. Tulionana pia na banganga benye banajua namna ya kutunza batu benye banasumbuliwa na mahangaiko, na ile pia ilisaidia. Leo mahangaiko yetu ilishapunguka, na tunamuomba Yehova atusaidie kufariji bengine benye banasumbuliwa na mahangaiko.
Wakati mulikuwa nazungumuzia namna Yehova amebasaidia kuvumilia magumu, mulisema kama alibabeba “kama mayayi ya mubichi.” Mulimaanisha nini?
Mats: Mu Kiswahili banasemaka, “Tumebebwa kama mayai ya mubichi.” Sawa vile mutu anabebaka muzuri mayayi ya mubichi juu isipasuke, ni vile Yehova ametutegemeza mu kila mugao. Hatuyakosaka bya lazima, Yehova alitupatia mambo mingi kupita hata yenye tulikuwa nayo lazima. Njia moya yenye Yehova ametuonyesha upendo na kututegemeza ni kupitia Baraza Yenye Kuongoza yenye inajitiaka pa nafasi yetu.
Ann-Catrin: Ninapenda kuzungumuzia mufano moya yenye kuonyesha namna Yehova ametutegemeza kwa upendo. Siku moya balituita ku telefone na kutuambia kama baba yangu mwenye alikuwa Suede alikuwa mugonjwa sana. Mats alikuwa anatoka tu kugonjwa malaria. Na hatukukuwa na makuta ya kulipa avion juu tufike Suede, njo maana tuliamua kama tutauzisha gari yetu. Kisha telefone ikalia ingine mara mbili. Ya kwanza ilikuwa ndugu fulani na bibi yake benye balisikia juu ya hali yetu na balipenda kulipia umoya wetu avion. Ya pili ilikuwa dada fulani mwenye kuzeeka mwenye alikuwa anaweka makuta pembeni “juu ya kusaidia mutu mwenye atakuwa mu uhitaji.” Mu dakika tu kidogo, tuliona namna Yehova alitusaidia!—Ebr. 13:6.
Mumejifunza mambo gani mu miaka 50 yenye mumepitisha mu utumishi wa wakati wote?
Mu mugao wetu wa mupya Myanmar
Ann-Catrin: Nimejifunza kama juu tukuwe na nguvu, tunapaswa ‘kuendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.’ Wakati tunamutegemea Yehova, anatupigania. (Isa. 30:15; 2 Nya. 20:15, 17) Juu tumetumikia Yehova kwa uwezo wetu wote mu kila mugao wenye ametupatia, tumepata baraka za mingi sana zenye hatungepataka mu njia ingine.
Mats: Jambo ya maana yenye nimejifunza ni kumutegemea Yehova mu kila hali na kuona vile atatenda kwa ajili yangu. (Zb. 37:5) Sikuzote anakuwaka tu tayari kutusaidia, sawa vile anaahidi kufanya. Na tunaendelea kujionea ile mu mugao wetu wa leo ku Beteli ya Myanmar.
Tunatumaini kama vijana benye banapenda kupanua utumishi wabo, batajionea pia upendo mushikamanifu wenye Yehova ametuonyesha. Tuko hakika kama batajionea ile kama tu banaacha Yehova abasaidie bakomale fasi yote kwenye banabapanda.