HABARI YA KUJIFUNZA YA 48
WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia
Kitabu ya Yobu Inaweza Kukusaidia Wakati Uko Nateseka
“Kwa kweli, Mungu hawezi kutenda uovu.”—YOB. 34:12.
WAZO KUBWA
Mambo yenye kitabu ya Yobu inaweza kutufundisha juu ya sababu zenye zinafanya Mungu aruhusu mateso, na namna tunaweza kuvumilia wakati tunateseka.
1-2. Juu ya nini ni muzuri tusome kitabu ya Yobu?
KUMEPITA masiku mingi tangu usome kitabu ya Yobu? Kitabu ya Yobu iliandikwa kumepita miaka 3 500 hivi, na batu mingi bameona kama ni kati ya bitabu byenye kuandikwa muzuri sana. Batu banasifu mwenye aliandika ile kitabu, juu alitumikisha maneno yenye iko mwepesi kuelewa, ya kupendeza, na ya kugusa sana. Ni Musa njo aliandika ile kitabu ya maana, lakini mwenye alimuambia bya kuandika ni Yehova Mungu.—2 Ti. 3:16.
2 Kitabu ya Yobu ni kitabu ya maana sana mu Biblia. Juu ya nini? Kwanza ni juu inazungumuzia kutakaswa kwa jina ya Yehova. Ile ni jambo ya maana sana yenye inahusu viumbe vyote vyenye akili. Tena kitabu ya Yobu inatufundisha juu ya sifa za ajabu za Yehova sawa vile upendo, hekima, haki, na nguvu. Kwa mufano, ni mu kitabu ya Yobu njo Yehova anaitwa mara mingi sana “Mweza-Yote;” mu ile kitabu Yehova anaitwa vile mara 31. Pia kitabu ya Yobu inajibia maulizo yenye batu mingi banajiulizaka juu ya maisha. Kati ya ile maulizo kuko hii ulizo yenye inahangaishaka batu mingi: Juu ya nini Mungu anaacha batu bateseke?
3. Tutajifunza nini kama tunasoma kitabu ya Yobu?
3 Sawa vile tunaonaka muzuri mambo yenye inatuzunguruka wakati tuko yulu ya mulima, ni vile tunaelewa muzuri mawazo ya Yehova juu ya mateso wakati tunasoma kitabu ya Yobu. Tuone basi namna kitabu ya Yobu inaweza kutusaidia wakati tuko nateseka. Tutaona pia namna habari ya Yobu ingeweza kusaidia Baisraeli na namna inaweza kutusaidia leo. Tena tutaona namna tunaweza kutumikisha habari ya Yobu juu ya kusaidia bengine.
MUNGU ANAACHA YOBU ATESEKE
4. Kulikuwa tofauti gani kati ya Yobu na Baisraeli benye balikuwa Misri?
4 Wakati Baisraeli balikuwa batumwa Misri, mwanaume mwenye kuitwa Yobu alikuwa naishi mu inchi ya Usi. Inawezekana Usi ilikuwa mashariki ya Inchi ya Ahadi karibu na Arabia. Baisraeli fulani balikuwa balishaanza kuabudu sanamu mu Misri, lakini Yobu yeye alikuwa namutumikia Yehova kwa uaminifu. (Yos. 24:14; Eze. 20:8) Yehova alisema hivi juu ya Yobu: “Hakuna mutu kama yeye juu ya dunia.”a (Yob. 1:8) Yobu alikuwa tajiri sana, alijulikana sana, na batu balimuheshimia sana kupita batu bote ba mu ile sehemu ya dunia. (Yob. 1:3) Bila shaka Shetani hakufurahi kuona mutu mwenye kujulikana na kuheshimiwa sana vile iko namutumikia Mungu kwa uaminifu!
5. Juu ya nini Yehova aliacha Yobu ateseke? (Yobu 1:20-22; 2:9, 10)
5 Shetani alisema kama Yobu akipata mateso ataacha kumutumikia Yehova. (Yob. 1:7-11; 2:2-5) Yehova alimupenda sana Yobu, lakini mashitaka yenye Shetani alileta ilikuwa ya buzito sana. Njo maana Yehova alimuacha Shetani aonyeshe ikiwa alisema kweli ao hapana. (Yob. 1:12-19; 2:6-8) Shetani alifanya Yobu apoteze wanyama wake wote, aliua batoto yake kumi, na akamuletea ugonjwa wa mubaya sana, majipu ilimuyala mwili muzima. Lakini ile magumu yote haikumufanya Yobu aache kumutumikia Yehova kwa uaminifu. (Soma Yobu 1:20-22; 2:9, 10.) Kisha wakati, Yehova alimurudishia Yobu afya ya muzuri, utajiri, na heshima yenye alipoteza, na Yobu alipata batoto bengine 10. Tena kwa muujiza Yehova alimuongezea miaka ingine 140 ya kuishi. Kwa hiyo, Yobu aliweza kuona bajukuu ya bajukuu yake. (Yob. 42:10-13,16) Namna gani habari ya Yobu ingesaidia batumishi ba Yehova ba zamani, na namna gani inaweza kutusaidia leo?
6. Kujua juu ya nini Yehova aliacha Yobu ateseke kungesaidia namna gani Baisraeli? (Ona pia picha.)
6 Namna habari ya Yobu ingesaidia Baisraeli. Maisha ya Baisraeli haikukuwa mwepesi wakati balikuwa naishi Misri. Kwa mufano, Yoshua na Kalebu balipitisha ujana wao wote mu butumwa. Kisha balipitisha ingine miaka 40 mu jangwa juu tu Baisraeli bengine balikosa kumutii Yehova. Kama Baisraeli balijua mateso ya Yobu na baraka zenye alipata ku mwisho, bila shaka ile ilibasaidia na ilisaidia pia vizazi vyenye vilifuata kuelewa ni nani njo analetaka mateso. Tena bangeelewa juu ya nini Mungu anaacha batu bateseke na kama Yehova anapenda sana batu benye banabakia baaminifu kwake na anababariki.
Baisraeli benye balikuwa batumwa kwa miaka mingi mu Misri, ku mwisho bangefikia kujua habari ya Yobu na ile ingebasaidia (Ona fungu ya 6)
7-8. Namna gani kitabu ya Yobu inaweza kusaidia benye biko nateseka? Leta mufano.
7 Namna habari ya Yobu inatusaidia. Inahuzunisha kuona kama leo batu mingi banaacha kumuamini Mungu juu habaelewe juu ya nini mambo ya mubaya inafikiaka batu bazuri. Fikiria mufano wa mwanamuke moya mwenye kuitwa Hazelb wa mu inchi ya Rwanda. Wakati alikuwa mutoto aliamini Mungu. Lakini mambo ilibadilika. Bazazi yake baliachana, kisha mama yake akaolewa na bwana mwingine. Ule bwana alikuwa namutendea Hazel mubaya. Na wakati Hazel alikuwa kijana, balimubaka. Wakati Hazel alienda ku kanisa yabo juu ya kupata faraja, hakuipata. Kisha, aliandikia Mungu barua. Mu ile barua alisema hivi: “Mungu, nilisali kwako, nilijikaza kufanya mambo ya muzuri, nilifanya bizuri lakini weye ukanilipa bibaya. Sasa ninaamua kukuacha, na kuanzia hapa nitafanya byote byenye binanifurahisha.” Tunasikia huzuni sana kuona vile batu mingi, sawa vile Hazel, banafundishwa kama ni Mungu njo anabaleteaka mateso!
8 Lakini, kitabu ya Yobu imetufundisha kama haiko Mungu njo analeteaka batu mateso, ni Shetani! Tena tumejifunza kama hatupaswe kuwaza kama benye biko nateseka balifanya mambo fulani ya mubaya. Biblia inatuambia kama “wakati na matukio yenye hayatazamiwe” inaweza kupata mutu yeyote wakati wowote. (Muh. 9:11; Yob. 4:1, 8) Tumejifunza pia kama wakati tunavumilia majaribu kwa uaminifu tunapatia Yehova nafasi ya kujibia Shetani mwenye anamuchokoza, na tunaonyesha kama Shetani ni muongo. (Yob. 2:3; Mez. 27:11) Tuko benye shukrani juu tunajua ile mambo yenye Biblia inafundisha. Ile mambo inatusaidia kuelewa juu ya nini siye na batu benye tunapendaka tunapata mateso. Hazel mwenye tulizungumuzia alianza kujifunza Biblia pamoya na Mashahidi wa Yehova na alifikia kuelewa kama haiko Mungu njo alimuletea mateso. Hazel alisema hivi: “Nilisali tena kwa Mungu kwa moyo wote. Nilimuambia Yehova kama wakati nilisema kama ninamuacha, kusema kweli sikumuacha juu sikukuwa hata namujua. Sasa ninaelewa kama Yehova ananipenda, na niko na furaha.” Tuko wenye shukrani sana juu tunajua juu ya nini Mungu anaacha batu bateseke! Tuone sasa namna habari ya Yobu inaweza kutusaidia wakati tuko na magumu.
NAMNA HABARI YA YOBU INATUSAIDIA KUVUMILIA
9. Yobu alitenda namna gani wakati alikuwa nateseka? (Yakobo 5:11)
9 Pima kuwazia hali ya Yobu: Anaikala yeye peke mu majifu, mwili yake inayala majipu na iko na maumivu ya mingi. Ngozi yake ilishaharibika sana juu ya ule ugonjwa na anagonda sana. Hana nguvu ya kufanya kitu, iko tu najipalula na kipande ya chombo ya budongo, na iko nanungunika juu ya maumivu yenye iko nayo. Lakini Yobu iko navumilia, haiko naishi tu juu ya kuishi. (Soma Yakobo 5:11.) Ni nini ilimusaidia avumilie?
10. Yobu alikuwa na uhusiano gani pamoya na Yehova? Fasiria.
10 Yobu alimuambia Yehova mambo yote yenye ilikuwa ku moyo wake. (Yob. 10:1, 2; 16:20) Kwa mufano, sura ya 3 ya kitabu ya Yobu inaonyesha namna Yobu alihuzunika sana juu ya mambo yenye ilimufikia, na namna aliwaza kama ni Yehova njo alimuletea ile mateso. Kisha, wakati barafiki yake batatu balimuambia kama mateso yenye iko napata ni malipizi kutoka kwa Mungu juu ya zambi zenye alifanya, Yobu aliendelea kujitetea na kuonyesha kama ni muaminifu. Maneno ya Yobu inaonyesha kama kwa wakati fulani alijiona kuwa mwenye haki kupita Mungu. (Yob. 10:1-3; 32:1, 2; 35:1, 2) Lakini alifikia kuitika kama wakati fulani alikuwa na “mazungumuzo ya ovyoovyo” saa alikuwa najikaza kutetea uaminifu wake. (Yob. 6:3, 26) Mu sura ya 31, Yobu anasema kama hastahili malipizi na anaomba Yehova amufasirie juu ya nini ile mambo iko namupata. (Yob. 31:35) Kusema kweli, Yobu hakukuwa na sheria ya kuomba Yehova amufasirie juu ya nini ile mambo yote iko namupata.
11. Yehova alijibia namna gani maneno ya Yobu ya kujitetea?
11 Tunaelewa sasa juu ya nini Yobu alijisikia huru kuzungumuza na Yehova. Ni juu alikuwa na urafiki wa nguvu pamoya naye na alikuwa hakika kama Yehova atamutendea kwa haki. Wakati Yehova alimujibia Yobu mu upepo mukali, hakumufasiria juu ya nini alikuwa nateseka, na hakumulaumu juu alikuwa nanungunika ao juu alikuwa natetea uaminifu wake. Lakini alimufundisha sawa vile baba anafundishaka mutoto wake. Na ile ilikuwa njia ya muzuri ya kumusaidia. Matokeo ilikuwa nini? Kwa unyenyekevu Yobu alikubali kama hajue kitu, na akatubu juu alizungumuza bila kuwaza. (Yob. 31:6; 40:4, 5; 42:1-6) Namna gani hii habari ingeweza kusaidia batumishi ba Yehova ba zamani, na namna gani inaweza kutusaidia leo?
12. Namna gani habari ya Yobu ingesaidia Baisraeli?
12 Namna habari ya Yobu ingesaidia Baisraeli. Mambo yenye ilifikia Yobu ingefundisha Baisraeli mambo ya maana. Fikiria mufano wa Musa. Alivumilia magumu ya mingi wakati alikuwa naongoza taifa ya Israeli. Mara mingi Baisraeli balikatala kumutii Yehova, na ile ilimuvunja Musa moyo. Baisraeli balimunungunikia Yehova tena na tena wakati mambo haikukuwa muzuri, lakini Musa yeye alielezea Yehova mahangaiko yake. (Kut. 16:6-8; Hes. 11:10-14; 14:1-4, 11; 16:41, 49; 17:5) Pia Musa alivumilia wakati Yehova alimukaripia. Kwa mufano, wakati Baisraeli balikuwa napiga kambi Kadeshi, mbele tu baingie mu Inchi ya Ahadi, Musa alizungumuza “bila kufikiri kupitia midomo yake” na alishindwa kutukuza jina ya Yehova. (Zb. 106:32, 33) Matokeo ilikuwa nini? Yehova hakuruhusu Musa aingie mu Inchi ya Ahadi. (Kum. 32:50-52) Bila shaka ile nizamu ilihuzunisha sana Musa, lakini aliikubali juu alikuwa munyenyekevu. Habari ya Yobu ingesaidia pia Baisraeli benye bangeisha kisha pale bavumilie magumu yenye bangepata. Kutafakari juu ya habari ya Yobu kungesaidia Baisraeli baaminifu bajifunze namna ya kufungulia Yehova moyo wao na kuepuka kujitetea mbele yake. Tena bangejifunza namna ya kuitika nizamu ya Yehova kwa unyenyekevu.
13. Namna gani habari ya Yobu inaweza kutusaidia tuvumilie? (Waebrania 10:36)
13 Namna habari ya Yobu inatusaidia. Siye Bakristo tuko na lazima ya kuvumilia. (Soma Waebrania 10:36.) Pengine tuko bagonjwa, tunashuka moyo, tuko na magumu mu familia, mupendwa wetu alikufa, ao tuko na magumu ingine ya nguvu. Na wakati fulani, maneno na matendo ya bengine inaweza kufanya ikuwe nguvu zaidi kuvumilia hali yetu. (Mez. 12:18) Lakini, kitabu ya Yobu inatufundisha kama tunaweza kuambia Yehova vile tuko najisikia kabisa, na kuwa hakika kama atatusikiliza. (1 Yo. 5:14) Na ikiwa saa tuko nazungumuza na Yehova wakati fulani tunakuwa na “mazungumuzo ya ovyoovyo” sawa Yobu, Yehova hatatulaumu. Lakini atatupatia nguvu na hekima yenye tuko nayo lazima juu ya kuvumilia. (2 Ny. 16:9; Yak. 1:5) Pia anaweza kuturekebisha kama ni lazima, sawa vile alimurekebisha Yobu. Kitabu ya Yobu inatufundisha tena namna tunaweza kuvumilia kama tunapata mashauri ao nizamu kutoka mu Neno ya Yehova, kutoka mu tengenezo yake, ao kutoka kwa barafiki benye kukomala kiroho. (Ebr. 12:5-7) Kwa unyenyekevu Yobu alikubali kurekebishwa na alipata faida, na siye tutapata faida kama tunakubali mashauri. (2 Ko. 13:11) Kwa kweli kitabu ya Yobu inatufundisha mambo ya maana sana! Tuone sasa vile tunaweza kutumikisha habari ya Yobu juu ya kusaidia bengine.
TUMIKISHA KITABU YA YOBU JUU YA KUSAIDIA BENGINE
14. Tunaweza kusema nini mu mahubiri juu ya kufasiria juu ya nini kuko mateso?
14 Mu mahubiri, mutu alishakakuuliza juu ya nini kuko mateso? Ulimujibiaka nini? Pengine ulimufasiriaka mambo yenye Biblia inazungumuzia yenye ilipitikanaka mu bustani ya Edeni. Pengine ulimuambiaka kwanza kama Shetani, malaika mubaya, alidanganya bazazi yetu ya kwanza na akabachochea bakose kumutii Mungu. (Mwa. 3:1-6) Kisha pengine ulimuambiaka kama kisha Adamu na Eva kukosa kumutii Mungu, batu balianza kuteseka na kufa. (Ro. 5:12) Ku mwisho, pengine ulimufasiriaka kama Mungu anaacha wakati ipite juu ya kuonyesha kama Shetani alisema bongo, na juu habari njema itangazwe kusudi batu yote bajue kama karibuni atatosha mateso yote na banadamu batakuwa tena bakamilifu. (Ufu. 21:3, 4) Ile ni njia ya muzuri ya kujibia ile ulizo, na inaweza kuwa na matokeo ya muzuri.
15. Namna gani unaweza kutumia kitabu ya Yobu juu ya kujibia mutu mwenye anauliza juu ya nini kuko mateso? (Ona pia picha.)
15 Njia ingine ya kujibia mutu mwenye anauliza juu ya nini kuko mateso ni kutumia kitabu ya Yobu. Kwanza unaweza kumupongeza juu ya ile ulizo ya maana. Kisha, unaweza kumuambia kama Yobu mwanaume muaminifu mwenye alitesekaka sana, naye aliulizaka juu ya nini iko nateseka. Na hata aliwaza kama Mungu njo alikuwa namuletea ile mateso. (Yob. 7:17-21) Mutu mwenye uko nazungumuza naye anaweza kushangala kusikia kama tangu zamani batu banajiulizaka ile ulizo. Kisha, unaweza kumufasiria kama ni Shetani njo aliletea Yobu ile mateso hapana Mungu. Shetani alifanya vile juu ya kujaribu kuonyesha kama banadamu banamutumikiaka Mungu juu tu ya bitu byenye Mungu anabapatia, haiko juu banamupenda. Unaweza pia kuongeza kama juu Mungu aliruhusu Yobu ateseke, ile inaonyesha kama anatumainia banadamu baaminifu; njo maana anabapatia nafasi ya kuonyesha kama Shetani ni musema-bongo. Ku mwisho, unaweza kumufasiria kama Mungu alibariki Yobu juu aliendelea kuwa muaminifu. Kwa hiyo, tunaweza kutia bengine moyo kwa kubahakikishia kama haiko Yehova njo analetaka mateso.
Namna gani unaweza kutumia kitabu ya Yobu juu ya kuhakikishia bengine kama haiko Mungu njo analetaka mambo ya mubaya? (Ona fungu ya 15)
16. Leta mufano wenye unaonyesha namna kitabu ya Yobu inaweza kusaidia mutu mwenye iko nateseka.
16 Ona vile kitabu ya Yobu ilisaidia Mario. Siku moya mu 2021, dada fulani alikuwa nahubiri ku telefone. Wakati aliita Mario kwa mara ya kwanza alisoma naye andiko ya Biblia na akamufasiria kama Mungu anasikilizaka sala zetu, na wakati wenye kuya atatufanyia mambo ya muzuri. Wakati ule dada alimuuliza mawazo yake juu ya ile andiko, Mario alimuambia kama wakati alimuita alikuwa naandika barua ya kulaga familia yake juu alitaka kujiua. Mario alisema hivi: “Ninaamini Mungu, lakini asubui nilikuwa najiuliza ikiwa alishaniacha.” Wakati ule dada alimuita tena ku telefone, balizungumuzia mateso ya Yobu, na Mario aliamua kusoma kitabu yote ya Yobu. Kwa hiyo ule dada alimutumia lien ya Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Matokeo ilikuwa nini? Mario alikubali kujifunza Biblia na alifurahi kujifunza mambo mingi juu ya Mungu mwenye upendo mwenye alionyesha kama anamuhangaikia.
17. Juu ya nini uko mwenye shukrani juu Yehova alitia kitabu ya Yobu mu Neno yake Biblia? (Yobu 34:12)
17 Ni wazi kama Neno ya Mungu iko na nguvu ya kusaidia batu, hata batu benye kuteseka. (Ebr. 4:12) Tuko benye shukrani juu Yehova aliandikisha habari ya Yobu mu Neno yake! (Yob. 19:23, 24) Kitabu ya Yobu inatuhakikishia kama “Mungu hawezi kutenda uovu.” (Soma Yobu 34:12.) Inatuonyesha pia juu ya nini Mungu anaacha mateso na namna tunaweza kuvumilia mateso. Na inatusaidia kujua namna tunaweza kufariji benye kuteseka. Mu habari yenye kufuata tutaona namna kitabu ya Yobu inaweza kutusaidia wakati tuko natoa mashauri.
WIMBO 156 Kwa Imani
a Inaonekana Yobu aliishi mu kipindi kati ya kifo ya Yosefu (1657 M.K.Y.) na wakati wenye Musa aliwekwa juu aongoze taifa ya Israeli (1514 hivi M.K.Y.). Inawezekana mazungumuzo kati ya Yehova na Shetani na majaribu ya Yobu ilipitikana mu ile kipindi.
b Majina fulani imebadilishwa.