Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 12 uku. 8-13
  • Namna Kitabu ya Yobu Inaweza Kutusaidia Wakati Tunatoa Mashauri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Kitabu ya Yobu Inaweza Kutusaidia Wakati Tunatoa Mashauri
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MASHAURI YA BARAFIKI TATU BA YOBU
  • NAMNA ELIHU ALIMUSHAURIA YOBU
  • TUENDELEE KUJIFUNZA MAMBO MINGI KUTOKA MU KITABU YA YOBU
  • Kitabu ya Yobu Inaweza Kukusaidia Wakati Uko Nateseka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Rafiki wa Kweli Anatoa Mashauri Yenye Kujenga
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • “Sitaacha Uaminifu-Mushikamanifu Wangu!”
    Tuige Imani Yao
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 12 uku. 8-13

HABARI YA KUJIFUNZA YA 49

WIMBO 44 Sala ya Mutu wa Hali ya Chini

Namna Kitabu ya Yobu Inaweza Kutusaidia Wakati Tunatoa Mashauri

“Lakini sasa, Yobu, tafazali sikia maneno yangu.”—YOB. 33:1.

WAZO KUBWA

Namna kitabu ya Yobu inatufundisha kutoa mashauri ya muzuri.

1-2. Ni daraka gani ya buzito yenye barafiki tatu ba Yobu na Elihu balikuwa nayo?

BILA kukawia batu yote ba mu eneo ya Mashariki balijua habari ya Yobu. Balijua vile alipoteza kila kitu yenye alikuwa nayo. Wakati barafiki yake tatu, Elifazi, Bildadi, na Sofari, balisikia juu ya mambo yenye ilimufikia, balifunga safari ya kuenda Usi juu ya kumufariji. Lakini saa balimuona Yobu baliishiwa. Habakuwazia kama hali yake ilikuwa mubaya sana vile.

2 Pima kuwazia hali ya Yobu: Alipoteza bitu byote byenye alikuwa nabyo. Wanyama wake waliibiwa, na wengine wakakufa. Batumishi yake ba mingi balikufa na nyumba ikaangukia batoto yake bote, nabo bakakufa. Zaidi ya ile Yobu aligonjwa sana; majipu ilimutoka mwili yote. Wakati barafiki tatu ba Yobu balimuona kwa mbali anaikala mu majivu, balifanya nini? Hata kama baliona maumivu yenye Yobu alikuwa nayo, balibakia kimya kwa siku saba hivi, habakumusemesha. (Yob. 2:​12, 13) Kisha kijana mwenye kuitwa Elihu alikuya na kuikala pembeni yabo. Ku mwisho, Yobu akaamua kusema. Alilaani siku yenye alizaliwa na akasema ingekuwa hata muzuri akufe. (Yob. 3:​1-3, 11) Ni kweli, Yobu alikuwa na lazima ya musaada! Maneno yenye bale banaume bangesema na namna bangeisema ingeonyesha kama kweli ni barafiki yake na kama banamuhangaikia kabisa.

3. Tutazungumuzia sasa nini?

3 Yehova aliongoza Musa aandike mambo yenye barafiki tatu ba Yobu na Elihu balisema na kufanya. Inawezekana mambo fulani yenye Elifazi alisema, iliongozwa na roho muovu. Lakini ni Yehova njo aliongoza Elihu aseme maneno yenye alisema. (Yob. 4:​12-16; 33:​24, 25) Njo maana haishangaze kuona kama mu kitabu ya Yobu muko mashauri fulani ya muzuri sana, lakini muko pia mashauri fulani ya mubaya sana. Kwa hiyo kitabu ya Yobu inaweza kutusaidia wakati tunapenda kutoa mashauri. Kwanza, tutaona mufano mubaya wa barafiki tatu ba Yobu. Kisha, tutaona mufano muzuri wa Elihu. Mu kila hali, tutaona namna kitabu ya Yobu ingesaidia Baisraeli na namna inaweza kutusaidia leo.

MASHAURI YA BARAFIKI TATU BA YOBU

4. Juu ya nini barafiki tatu ba Yobu balishindwa kumufariji? (Ona pia picha.)

4 Biblia inasema kama barafiki tatu ba Yobu balienda “kumupatia Yobu pole na kumufariji” kisha kusikia mambo yenye ilimupata. (Yob. 2:11) Lakini balishindwa kumufariji. Juu ya nini? Kuko sababu tatu. Kwanza, balimuhukumu bila kumusikiliza. Kwa mufano, balisema kama mambo yenye ilimupata Yobu ilikuwa malipizi ya zambi zenye alifanya.a (Yob. 4:7; 11:14) Pili, mashauri ya mingi yenye balipatia Yobu haikumusaidia, haikukuwa ya upendo, na ilikuwa ya kuumiza. Kwa mufano, bale banaume bote tatu balisema maneno yenye ilionekana sawa vile ni ya muzuri, lakini haikukuwa ya kweli. (Yob. 13:12) Bildadi alisema mara mbili kama Yobu alikuwa nasema mingi. (Yob. 8:2; 18:2) Na bila huruma Sofari alisema kama Yobu alikuwa “mupumbavu.” (Yob. 11:12) Hata kama habakumufokea Yobu, mambo yenye balisema na namna baliisema haikuonyesha upendo, heshima, na ilifanya Yobu ajihukumu. (Yob. 15:​7-11) Bale banaume balipenda sana kuonyesha kama Yobu alikosea kuliko kumutia moyo na kutia nguvu imani yake.

Rafiki mumoya wa Yobu iko nazungumuza naye kwa ukali wakati bengine bawili biko naangalia. Yobu mwenye anayala majipu mwili yote iko nasikiliza mashauri yake wakati anaikala chini.

Wakati uko natoa mashauri, ujikaze kusema kwa upole. Kusudi yako inapaswa kuwa kusaidia mutu (Ona fungu ya 4)


5. Mashauri yenye bale barafiki tatu ba Yobu balitoa ilikuwa na matokeo gani?

5 Haishangaze kuona kama mashauri yenye barafiki tatu ba Yobu balitoa haikuleta matokeo ya muzuri. Maneno yabo ilifanya Yobu ajisikie mubaya zaidi. (Yob. 19:2) Tunaelewa juu ya nini Yobu alianza kujitetea na kusema mambo yenye hakupaswa kusema. (Yob. 6:​3, 26) Mawazo ya bale barafiki yake tatu haikupatana na mawazo ya Yehova, na habakutendea Yobu kwa huruma. Matokeo ilikuwa nini? Shetani aliweza kubatumikisha juu ya kuvunja Yobu moyo. (Yob. 2:​4, 6) Namna gani hii habari ingeweza kusaidia Baisraeli ba zamani, na namna gani inaweza kutusaidia leo?

6. Mufano mubaya wa barafiki tatu ba Yobu ungefundisha nini bazee ba Israeli?

6 Namna hii habari ingesaidia Baisraeli. Kisha Yehova kuanzisha taifa ya Israeli, aliweka banaume benye kustahili, ni kusema bazee, juu bahukumu taifa kwa kufuata kanuni zake zenye haki. (Kum. 1:​15-18; 27:1) Bale banaume balipaswa kusikiliza kwa uangalifu mbele ya kutoa mashauri ao mbele ya kuhukumu. (2 Ny. 19:6) Balipaswa pia kuuliza maulizo kuliko kuwaza kama banajua mambo yote. (Kum. 19:18) Balipaswa kuepuka kutumia maneno makali. Juu ya nini? Juu ile ingevunja mutu moyo na kumuzuia kusema mambo yenye iko nayo ku moyo. (Kut. 22:​22-24) Ile ni mambo fulani tu yenye habari ya Yobu ingefundisha bale bazee ba Israeli.

7. Zaidi ya bazee ba Israeli, ni nani bengine bangeweza kutoa mashauri, na namna gani habari ya Yobu ingebasaidia? (Mezali 27:9)

7 Bila shaka, haiko bazee tu njo bangeweza kutoa mashauri mu Israeli. Mwisraeli yeyote, ikuwe kijana ao muzee, mwanaume ao mwanamuke, angeweza kutolea mwenzake mashauri yenye ingemusaidia mu ibada yake kwa Yehova, ao ya kumusaidia aachane na tabia fulani ya mubaya. (Zb. 141:5) Kusema kweli, barafiki ba kweli banashaurianaka. (Soma Mezali 27:9.) Mufano mubaya wa barafiki tatu ba Yobu ungesaidia Baisraeli ba zamani bajue mambo yenye habakupaswa kusema na yenye habakupaswa kufanya wakati biko natoa shauri.

8. Tunapaswa kuepuka nini wakati tuko natoa mashauri? (Ona pia picha.)

8 Namna habari ya Yobu inaweza kutusaidia. Siye Bakristo tunapenda kusaidia bandugu na badada yetu wakati biko mu magumu. Lakini, juu tuweze kufanya vile, tunapaswa kuepuka mambo yenye barafiki tatu ba Yobu balifanyaka. Kwanza, hatupaswe kuhukumu mutu haraka-haraka, tunapaswa kuhakikisha kama tunajua mambo yote muzuri mbele ya kusema. Pili, tusikuwe sawa Elifazi, siye mashauri yetu inapaswa kutegemea Neno ya Mungu, hapana mawazo yetu ao mambo yenye tunajua. (Yob. 4:8; 5:​3, 27) Tatu, tunapaswa kuepuka kutumia maneno ya makali ao ya kukosa upendo. Kuko mambo fulani ya kweli yenye Elifazi na benzake balisema, na hata Paulo alitaya mambo fulani yenye balisema. (Linganisha Yobu 5:13 na 1 Wakorinto 3:19.) Lakini, mambo mingi yenye balisema juu ya Mungu haikukuwa ya kweli na iliumiza Yobu. Njo maana Yehova alisema kama habakusema kweli. (Yob. 42:​7, 8) Mashauri yetu haipaswe kufanya ionekane sawa vile Yehova hana usawaziko na haipaswe kufanya mutu aone sawa vile Yehova hamupendi. Tuone sasa mambo yenye mufano wa Elihu unaweza kutufundisha.

Picha: Ndugu iko nashauria kwa upendo ndugu mwenye iko na huzuni. 1. Ndugu iko nasikiliza kwa uvumilivu wakati ndugu mwenye iko na huzuni iko najieleza, banaikala inje na ku meza kuko binywaji. 2. Ndugu mwenye iko nasikiliza anafungula Biblia. 3. Kwa upendo ule ndugu anasoma shauri ya mu Biblia na ule ndugu mwingine iko nasikiliza kwa utulivu.

Wakati uko natoa mashauri, (1) uhakikishe kama unajua mambo muzuri, (2) utumikishe Neno ya Mungu, na (3) uzungumuze kwa upendo (Ona fungu ya 8)


NAMNA ELIHU ALIMUSHAURIA YOBU

9. Fasiria juu ya nini Yobu alikuwa na lazima ya musaada kisha barafiki yake tatu kuacha kusema, na namna Yehova alimusaidia.

9 Yobu na barafiki yake tatu balibishana wakati murefu. Maneno yabo inakamata sura 28 za kitabu ya Yobu, na ilionyesha kama balikuwa balishasirika. Tunaelewa juu ya nini Yobu aliendelea kuvunjika moyo! Alikuwa tu angali na lazima ya mutu wa kumufariji na kumusaidia abadilishe mawazo yake. Namna gani Yehova alimusaidia? Alitumikisha Elihu. Juu ya nini Elihu alingoya mbele ya kusema? Elihu alisema hivi: “Mimi ni kijana, na ninyi ni wazee. Kwa hiyo, kwa heshima, nilijizuia.” (Yob. 32:​6, 7) Elihu alielewa hii jambo yenye batu mingi balishaelewa leo: Batu benye kuzeeka bameishi miaka mingi na bamejifunza mambo mingi, kwa hiyo biko na hekima na uzoefu wenye mara mingi vijana hawana. Lakini kisha kusikiliza kwa uvumilivu Yobu na barafiki yake, Elihu hakuendelea kubakia kimya. Alisema hivi: “Haiko kuishi miaka mingi tu ndiko kunamufanya mutu akuwe na hekima, na haiko wazee peke yao ndio wanaelewa mambo yenye kuwa sawa.” (Yob. 32:9) Elihu alisema nini kisha pale, na aliisema namna gani?

10. Elihu alifanya nini mbele ashaurie Yobu? (Yobu 33:​6, 7)

10 Mbele Elihu ashaurie Yobu, alifanya Yobu atulie na ajisikie muzuri juu akuwe tayari kumusikiliza. Alifanya vile namna gani? Biblia inasema kama Elihu naye alikuwa alishasirika, kwa hiyo alitulia kwanza. (Yob. 32:​2-5) Ile ilimusaidia asiseme maneno yenye ingemukasirisha Yobu ao kumuumiza, lakini aseme maneno ya kumutia moyo. Kwa mufano, aliambia hivi Yobu: “Angalia! Mimi niko tu kama wewe mbele ya Mungu wa kweli.” (Soma Yobu 33:​6, 7.) Na juu ya kuonyesha kama alisikiliza Yobu kwa uangalifu, alirudilia mawazo makubwa ya maneno ya Yobu. (Yob. 32:11; 33:​8-11) Alifanya tena vile wakati alishauria Yobu mara ingine.—Yob. 34:​5, 6, 9; 35:​1-4.

11. Elihu alishauria Yobu namna gani? (Yobu 33:1)

11 Wakati Elihu alishauria Yobu, alionyesha kama anaheshimia ule mwanaume muaminifu. Kwa mufano, alimuita ku jina yake, jambo yenye inaonekana bale barafiki yake tatu habakufanya. (Soma Yobu 33:1.) Na pengine alikumbuka vile alikuwa na hamu sana ya kusema wakati Yobu na barafiki yake balikuwa nabishana, njo maana alipatia Yobu nafasi ya kujibia kisha yeye kumushauria. (Yob. 32:4; 33:32) Tena alionya Yobu waziwazi juu ya mawazo yenye haifae yenye alikuwa nayo, na kwa upole alimukumbusha juu ya hekima, nguvu, haki na upendo mushikamanifu wa Yehova. (Yob. 36:​18, 21-26; 37:​23, 24) Bila shaka, mashauri ya muzuri ya Elihu ilisaidia Yobu akuwe tayari kusikiliza mashauri ingine kutoka kwa Muumbaji wake. (Yob. 38:​1-3) Namna gani mufano wa Elihu ungesaidia Baisraeli ba zamani na namna gani unaweza kutusaidia leo?

12. Namna gani Yehova alitumia manabii juu ya kusaidia batu yake, na namna gani mufano muzuri wa Elihu ungeweza kusaidia Baisraeli?

12 Namna hii habari ingesaidia Baisraeli. Mara mingi Yehova alitumikisha manabii juu ya kufundisha Baisraeli na kubasaidia baachane na njia ya mubaya. Kwa mufano, mu wakati wa baamuzi, Yehova alitumia Debora juu ya kutolea taifa muongozo. Na alitumia Samweli hata wakati alikuwa kijana, juu ya kufundisha batu. (Amu. 4:​4-7; 5:7; 1 Sa. 3:​19, 20) Na wakati wa Wafalme, Yehova aliendelea kutumikisha manabii juu basaidie batu yake baendelee kumuabudu mu njia yenye kufaa, na juu babatolee mashauri wakati habakumutii. (2 Sa. 12:​1-4; Mdo. 3:24) Mufano wa Elihu wenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Yobu ungesaidia bale banaume na banamuke baaminifu bajue mambo ya kusema wakati biko natoa shauri na namna ya kuisema.

13. Namna gani Bakristo leo banaweza kutia moyo baabudu benzabo?

13 Namna hii habari inaweza kutusaidia. Na siye Bakristo tunaambiaka batu mapenzi ya Mungu yenye kuwa mu Neno yake Biblia. Pia tunatumikishaka maneno ya muzuri juu ya kujenga na kutia moyo baabudu benzetu. (1 Ko. 14:3) Bazee banapaswa kujikaza hata zaidi “kusema kwa namna yenye kufariji” wakati biko nazungumuza na bandugu na badada yabo, hata benye balishasirika ao benye biko na “mazungumuzo ya ovyoovyo.”—1 Te. 5:14; Yob. 6:3.

14-15. Leta mufano wenye kuonyesha namna muzee anaweza kuiga mufano wa Elihu wakati iko natoa mashauri.

14 Wazia hii hali: Muzee anapata habari kama dada fulani mu kutaniko alishavunjika moyo. Yeye na ndugu mwingine banaenda kumutembelea juu ya kumutia moyo. Wakati biko kule, ule dada anabaambia kama hata kama iko nakusanyika na iko naesnda mu mahubiri, hana furaha. Ule muzee atafanya nini juu ya kumusaidia?

15 Kwanza, inawezekana atajikaza kuelewa juu ya nini ule dada iko najisikia vile. Na juu aelewe, itaomba amusikilize kwa uvumilivu. Muzee anaweza kujiuliza hivi: Huyu dada alishavunjika moyo juu anawaza kama hastahili upendo wa Yehova? Ao ni “mahangaiko ya maisha” njo inafanya avunjike moyo? (Lu. 21:34) Pili, ule muzee atajikaza kupongeza ule dada juu iko naendelea kukusanyika na kuhubiri hata kama alishavunjika moyo. Tatu, kisha ule muzee kuelewa hali na kuelewa mambo yenye iko nafanya ule dada avunjike moyo, atatumikisha Biblia juu ya kumusaidia akuwe hakika kama Yehova anamupenda.—Gal. 2:20.

TUENDELEE KUJIFUNZA MAMBO MINGI KUTOKA MU KITABU YA YOBU

16. Tunaweza kufanya nini juu tuendelee kujifunza mambo mingi kutoka mu kitabu ya Yobu?

16 Kuchunguza kitabu ya Yobu kumetusaidia sana! Mu habari yenye ilitangulia, kitabu ya Yobu ilitusaidia kuelewa juu ya nini Mungu anaacha batu bateseke na namna tunaweza kuvumilia mateso. Na mu hii habari, tunaona kama siye bote tunaweza kutoa mashauri ya muzuri kama tunaepuka mufano mubaya wa barafiki tatu ba Yobu na kufuata mufano muzuri wa Elihu. Mu siku zenye ziko nakuya kama inaomba utoe shauri, itakuwa muzuri uchunguze kwanza mambo yenye tunajifunza mu kitabu ya Yobu. Na kama kulishapita wakati mingi tangu usome kitabu ya Yobu, ni muzuri ujitilie muradi wa kuisoma tena. Kama unafanya vile, utajifunza mambo ingine ya mingi yenye inaweza kukusaidia.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Mufano wa barafiki tatu ba Yobu unatusaidia kuepuka nini wakati tuko natoa mashauri?

  • Namna gani Elihu alionyesha hekima wakati alimutolea Yobu mashauri?

  • Tunaweza kufanya nini juu kitabu ya Yobu iendelee kutusaidia?

WIMBO 125 “Wenye Furaha Ni Wale Wenye Rehema!”

a Inaonekana kama ni roho muovu njo aliongoza Elifazi aseme kama hakuna mwanadamu mwenye Yehova anaona kuwa mwenye haki na hakuna mwanadamu mwenye anaweza kumufurahisha Mungu. Elifazi aliamini kabisa ile mawazo ya bongo, na aliirudilia kila wakati alizungumuza na Yobu.—Yob. 4:17; 15:​15, 16; 22:2.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine