Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 15/10 uku. 3-8
  • Unaona Mukono wa Mungu Katika Maisha Yako?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unaona Mukono wa Mungu Katika Maisha Yako?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • WALIKATAA KUONA MUKONO WA MUNGU
  • WALIONA MUKONO WA YEHOVA
  • TUNAONA MUKONO WA MUNGU LEO
  • UNAONA MUKONO WA YEHOVA KATIKA MAISHA YAKO?
  • Alivumilia Ukosefu wa Haki
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Alikesha, na pia Alingojea
    Tuige Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Namna Yehova Anajibiaka Sala Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 15/10 uku. 3-8
Wakati mwanamuke huyu angali anasali katika nyumba yake, Mashahidi wa Yehova wanagonga kwenye mulango wake

Unaona Mukono wa Mungu Katika Maisha Yako?

‘Mukono wa Yehova utajulishwa kwa watumishi wake.’—ISAYA 66:14.

NYIMBO: 65, 26

UNAWEZA KUELEZA?

  • Watu fulani wanaona mukono wa Mungu katika maisha yao, lakini wengine hawauone. Sababu gani?

  • Ni mambo gani yenye kuonyesha kwamba Yehova anatuhangaikia leo?

  • Namna gani tunaweza kuona wazi-wazi mukono wa Mungu katika maisha yetu?

1, 2. Watu fulani wako na mawazo gani juu ya Mungu?

WATU wengi wanaamini kwamba Mungu hahangaikie mambo yenye wanafanya. Wanawaza kwamba Mungu hahangaikie hata kidogo magumu yenye wanapata katika maisha yao. Kwa mufano, katika Mwezi wa 11, 2013 kimbunga ao upepo mukubwa uliharibu sehemu kubwa ya inchi ya Ufilipino. Kisha upepo huo, kiongozi wa muji fulani mukubwa alisema hivi: “Inawezekana Mungu haiko tena pamoja na sisi.”

2 Watu wengine wanawaza kwamba Mungu hawezi kuona mambo yenye wanafanya. (Isaya 26:10, 11; 3 Yohana 11) Wakati wa mutume Paulo, watu fulani walikuwa na mawazo kama hayo. Mutume Paulo alisema kwamba ‘hawakukubali kumujua Mungu.’ Walikuwa wenye kukosa haki, wenye pupa ao tamaa nyingi, na wabaya.—Waroma 1:28, 29.

3.(a) Tunapaswa kujiuliza maulizo gani? (b) Katika Biblia, mara nyingi maneno ‘mukono wa Mungu’ inamaanisha nini?

3 Sisi tuko na mawazo gani? Tunajua kwamba Yehova anaona mambo yote yenye tunafanya. Lakini, tunaamini kwamba Yehova anatuhangaikia kabisa? Tunaona namna mukono wake unatusaidia katika maisha yetu? Katika Biblia, mara nyingi maneno ‘mukono wa Mungu’ inamaanisha nguvu zake. Anatumia nguvu zake ili kusaidia watumishi wake na kupata ushindi juu ya maadui wake. (Soma Kumbukumbu la Torati 26:8.) Yesu alisema kwamba watu fulani ‘watamuona Mungu.’ (Mathayo 5:8) Tuko kati ya watu hao? Namna gani tunaweza ‘kumuona Mungu’? Acha sasa tuzungumuzie mifano yenye kupatikana katika Biblia ya watu wenye waliona mukono wa Mungu katika maisha yao, na wale wenye hawakuona mukono huo. Tutajifunza pia namna imani inatusaidia tuone mukono wa Mungu.

WALIKATAA KUONA MUKONO WA MUNGU

4. Sababu gani maadui wa Waisraeli walikataa kuona mukono wa Mungu?

4 Zamani, watu wengi walikuwa na nafasi ya kuona ao kusikia namna Mungu alisaidia taifa la Israeli. Yehova alitumia miujiza ili kukomboa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri na kupata ushindi juu ya wafalme wengi katika Inchi ya Ahadi. (Yoshua 9:3, 9, 10) Wafalme wengine waliona ao kusikia namna Yehova alikomboa watu wake, lakini ‘walianza kukusanyika pamoja ili kupigana vita na Yoshua na Israeli.’ (Yoshua 9:1, 2) Wakati wafalme hao walipigana na Waisraeli, walikuwa na nafasi ya kuona mukono wa Mungu. Kwa musaada wa nguvu kubwa za Yehova, ‘jua likasimama, mwezi nao ukasimama, mupaka taifa hilo lilipokuwa limelipiza kisasi juu ya maadui wake.’ (Yoshua 10:13) Lakini Yehova aliacha mioyo ya maadui wa Waisraeli ‘ikuwe migumu,’ ili wapigane na taifa hilo. (Yoshua 11:20) Maadui hao walishindwa kwa sababu walikataa kukubali kwamba ni Yehova ndiye alikuwa anapigania watu wake.

Unatafuta nafasi za kukusaidia uone mukono wa Mungu katika maisha yako?

5. Ahabu, Mufalme mubaya, alikataa kuamini nini?

5 Kisha miaka mingi, Ahabu, Mufalme mubaya, alikuwa na nafasi ya kuona mukono wa Mungu mara nyingi. Nabii Eliya alimuambia hivi: “Hakutakuwa na umande wala mvua, isipokuwa kwa agizo la neno langu!” (1 Wafalme 17:1) Ni mukono wa Mungu tu ndio ulizuia umande na mvua, lakini Ahabu alikataa kuamini jambo hilo. Kisha, nabii Eliya alisali kwa Yehova, naye alimujibu kwa kushusha moto kutoka mbinguni. Ahabu aliona namna moto huo unashuka. Kisha, nabii Eliya alimuambia Ahabu kwamba Yehova atamaliza kipwa na kufanya mvua kubwa inyeshe. (1 Wafalme 18:22-45) Ahabu alijionea miujiza hiyo yote, lakini aliendelea kukataa kukubali kwamba ilifanyika kwa nguvu za Yehova. Mifano hiyo inatufundisha nini? Tunapaswa kuona mukono wa Mungu katika maisha yetu.

WALIONA MUKONO WA YEHOVA

6, 7. Wagibeoni na Rahabu walitambua nini?

6 Wagibeoni walikuwa tofauti sana na mataifa mengine yenye ilikuwa pembeni yao. Waliona mukono wa Mungu. Kuliko kupigana na taifa la Israeli, Wagibeoni walifanya amani pamoja nao. Sababu gani? Walisema kwamba walisikia habari juu ya mambo yote yenye Yehova alikuwa amefanya. (Yoshua 9:3, 9, 10) Walifanya muzuri kutambua kwamba Yehova alikuwa anapigania taifa la Israeli.

7 Rahabu pia aliona mukono wa Yehova. Hakuwa Muisraeli, lakini alisikia habari juu ya namna Yehova alikomboa watu wake kutoka katika inchi ya Misri. Wakati wapelelezi wawili Waisraeli walifika kwake, aliwaambia hivi: ‘Ninajua kwamba Yehova atawapatia inchi hii.’ Rahabu alikuwa na imani kwamba Yehova angemuokoa na watu wa familia yake. Alionyesha imani katika Yehova hata kama alijua kwamba kufanya hivyo kungemuletea hatari.—Yoshua 2:9-13; 4:23, 24.

8. Namna gani Waisraeli fulani walitambua mukono wa Mungu?

8 Tofauti na Ahabu, Mufalme mubaya, Waisraeli fulani wenye waliona namna Yehova anajibu sala ya nabii Eliya kwa kushusha moto kutoka mbinguni, walitambua kwamba Mungu ndiye alifanya jambo hilo. Walisema hivi kwa sauti kubwa: “Yehova ndiye Mungu wa kweli!” (1 Wafalme 18:39) Walikuwa hakika kwamba walikuwa wameona nguvu za Mungu.

9. Namna gani tunaweza kumuona Yehova na kuona mukono wake leo?

9 Tumezungumuzia mifano ya muzuri na ya mubaya yenye kutusaidia tuelewe maana ya ‘kumuona Mungu’ ao kuona mukono wa Mungu. Wakati tunafikia kumujua Yehova na sifa zake, tunaona mukono wake kupitia ‘macho ya moyo wetu.’ (Waefeso 1:18) Hilo linatuchochea tuige watumishi waaminifu wa zamani na wa leo wenye wameona namna Yehova amewasaidia watu wake. Lakini, ni mambo gani inaonyesha kwamba Yehova anaendelea kuwasaidia watumishi wake leo?

TUNAONA MUKONO WA MUNGU LEO

10. Ni mambo gani inaonyesha kwamba Yehova anaendelea kuwasaidia watu leo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

10 Tuko na mambo mengi yenye kuonyesha kwamba Yehova anaendelea kuwasaidia watu leo. Mara nyingi, tunasikia habari za watu wenye walisali ili Mungu awasaidie katika maisha yao, na namna alijibu sala zao. (Zaburi 53:2) Kwa mufano, wakati ndugu Allan alikuwa anahubiri katika kisiwa fulani cha inchi ya Ufilipino, alikutana na mwanamuke moja. Mara moja mwanamuke huyo alianza kulia. Ndugu Allan anasema hivi: “Asubuhi hiyohiyo mwanamuke huyo alisali kwa Yehova ili Mashahidi wamutembelee.” Wakati alikuwa kijana, mwanamuke huyo alijifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, lakini kisha kuolewa alihamia kwenye kisiwa hicho, na hakuendelea tena kujifunza. Mungu alijibu palepale sala yake na hilo liligusa moyo wake. Kisha miezi fulani, alijitoa kwa Yehova na kubatizwa.

1. Mwanaume huyu anakataa tumbako; 2. Dada anahubiri katika eneo la kigeni; 3. Ndugu anajitetea kwenye tribinali

Unatafuta nafasi za kukusaidia uone mukono wa Mungu katika maisha yako?(Picha hizi zinapatana na fungu la 11-13)

11, 12.(a)Namna gani Yehova anaendelea kuwasaidia watumishi wake? (b) Eleza namna Yehova alimusaidia dada moja.

11 Watumishi wengi wa Yehova wamejionea namna mukono wake umewasaidia waache tabia mbaya zenye walikuwa nazo zamani kama vile, kuvuta tumbako, kutumia dawa za kulewesha, ao kuangalia pornografia. Wamoja kati yao wanasema kwamba walijikaza kuacha tabia hizo, lakini walishindwa. Hata hivyo, wakati walimuomba Yehova musaada, aliwapatia “nguvu zinazopita zile za kawaida,” na mwishowe walifikia kuachana kabisa na tabia hizo.—2 Wakorintho 4:7; Zaburi 37:23, 24.

Yehova anasaidia watumishi wake wavumilie magumu yenye wanapambana nayo

12 Yehova anasaidia pia watumishi wake wavumilie magumu yenye wanapambana nayo. Dada Amy alijionea jambo hilo. Alipewa mugawo wa kusaidia kujenga Jumba la Ufalme na nyumba ya wamisionere kwenye kisiwa kidogo katika Bahari ya Pasifiki. Hali ya maisha ya kule ilikuwa tofauti, ni kusema, mara nyingi hakukuwa umeme (courant) ao maji, barabara zilikuwa na maji mengi, aliendelea kukumbuka familia yake, na alikuwa anaishi katika chumba kidogo kwenye hoteli. Siku moja alitombokea dada moja mwenye walikuwa wanatumika pamoja naye. Jambo hilo lilimuhuzunisha sana. Wakati alirudia katika chumba chake chenye kuwa na giza, alisali kwa Yehova na kumuomba musaada. Kisha, wakati umeme ulirudia, alisoma katika Munara wa Mulinzi habari yenye kuzungumuzia wakati wanafunzi wa Gileadi wanapewa vyeti vyao. Habari hiyo ilizungumuzia magumu yenye alipaswa pia kuvumilia. Anasema hivi: “Nilijisikia kuwa Yehova alikuwa anazungumuza na mimi usiku huo. Habari hiyo ilinisaidia niendelee na ­mugawo wangu.”—Zaburi 44:25, 26; Isaya 41:10, 13.

13. Ni mambo gani inaonyesha kwamba Yehova amesaidia watumishi wake watetee haki yao ya kuhubiri?

13 Yehova amesaidia pia watumishi wake kutetea habari njema kulingana na sheria. (Wafilipi 1:7) Kwa mufano, wakati guvernema fulani zilijaribu kusimamisha kazi yetu ya kuhubiri, tulijitetea kwenye tribinali. Katika dunia yote, tumepata ushindi kwenye tribinali kubwa karibu mara 268, na tangu mwaka wa 2000, tumepata ushindi mara 24 kwenye Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya. Inaonekana wazi kwamba hakuna mutu mwenye anaweza kuzuia mukono wa Mungu!—Isaya 54:17; soma Isaya 59:1.

14. Ni mambo mengine gani yenye kuonyesha kwamba Mungu iko pamoja na watu wake?

14 Jambo lingine lenye kuonyesha kwamba mukono wa Mungu unatusaidia ni kazi ya kuhubiri habari njema yenye inafanywa katika dunia yote. (Mathayo 24:14; Matendo 1:8) Pia, ni kwa musaada wa Yehova tu ndiyo watumishi wake kutoka katika mataifa yote wanaishi kwa umoja. Umoja huo ni wa pekee sana! Hata watu wenye hawamuabudu Yehova wanakubali kwamba ‘kwa kweli Mungu iko katikati yetu.’ (1 Wakorintho 14:25) Kuna mambo mengi yenye kuonyesha kwamba Mungu iko pamoja na watu wake. (Soma Isaya 66:14.) Halafu wewe? Je, unaona mukono wa Yehova katika maisha yako?

UNAONA MUKONO WA YEHOVA KATIKA MAISHA YAKO?

15. Sababu gani wakati fulani tunaweza kukosa kuona mukono wa Yehova katika maisha yetu?

15 Wakati fulani, inawezekana tukose kuona mukono wa Mungu katika maisha yetu. Sababu gani? Kwa sababu wakati tunapatwa na magumu mengi, tunaweza kusahau kwamba Yehova ametusaidia mara nyingi zamani. Jambo hilo lilimufikia nabii Eliya. Alikuwa mwenye bidii, lakini wakati Malkia Yezebeli alitafuta kumuua, nabii Eliya aliogopa sana. Alisahau kwanza namna Yehova alikuwa amemusaidia zamani. Biblia inasema kwamba nabii Eliya aliomba akufe. (1 Wafalme 19:1-4) Ni nani angemusaidia ili akuwe na bidii tena? Alipaswa kumutegemea Yehova!—1 Wafalme 19:14-18.

16. Namna gani tunaweza kuona mukono wa Mungu wakati tunapatwa na magumu?

16 Ayubu alikaza sana akili juu ya magumu yake na hilo lilimufanya akose kuona hali yake namna Yehova alikuwa anaiona. (Ayubu 42:3-6) Wakati fulani, inaweza pia kuwa vigumu kwetu kuona mukono wa Mungu kwa sababu ya magumu yetu. Ni nini inaweza kutusaidia tuone mambo yenye Mungu anatufanyia? Tunapaswa kufikiri sana juu ya mambo yenye Biblia inasema juu ya magumu yetu. Kisha, tutamuona Yehova kuwa mutu wa kweli kabisa, na hilo litatusaidia pia tuweze kusema hivi: ‘Nimesikia habari zako, lakini sasa jicho langu mwenyewe linakuona wewe.’

Dada wawili wanahubiria mwanamuke moja katika barabara

Je, Yehova anakutumikisha ili usaidie wengine wamuone? (Picha hizi zinapatana na fungu la 17, 18)

17, 18. (a) Namna gani unaweza kuona mukono wa Yehova katika maisha yako? (b) Toa mufano wenye kuonyesha kwamba Mungu anaendelea kutusaidia leo.

17 Namna gani unaweza kuona mukono wa Yehova katika maisha yako? Acha sasa tufikirie mifano tano. Kwanza, unaweza kuelewa kwamba Yehova alikusaidia ujue kweli. Pili, pengine unakumbuka wakati ulienda kwenye mikutano, na kisha kusikiliza hotuba fulani, ulisema hivi; “Ni kama vile hotuba hii ilitayarishwa kabisa kwa ajili yangu!” Tatu, inawezekana umekwisha kuona namna Yehova anajibu moja kati ya sala zako. Ine, pengine ulipenda kufanya mengi katika kazi ya Yehova na uliona namna alikusaidia ufikie muradi wako. Tano, pengine uliacha kazi yako kwa sababu ilikuwa inakuzuia uendelee kumutumikia Yehova na kisha uliona namna anatimiza ahadi yake hii: “Sitakutupa hata kidogo.” (Waebrania 13:5) Wakati tuko na urafiki wa sana pamoja na Yehova, inaweza kuwa vyepesi kwetu kuona mukono wake katika maisha yetu.

18 Dada Sarah wa inchi ya Kenya, anasema hivi: “Nilisali kwa ajili ya mwanafunzi moja mwenye niliona kuwa hapendezwe na funzo la Biblia. Niliuliza Yehova ikiwa niache kujifunza naye. Kisha tu kusema ‘Amina’, telefone yangu ikalia. Mwanafunzi huyo wa Biblia aliniita ili kuniuliza ikiwa tunaweza kuenda naye kwenye mikutano! Nilishangaa sana!” Ikiwa tunafikiri sana juu ya mambo yenye Mungu anaendelea kutufanyia, tutaona namna mukono wake unaendelea kutusaidia. Dada Rhonna, mwenye kuishi Asia, anasema kwamba inaomba wakati ili kuona namna Yehova anatusaidia katika maisha yetu. Anaongezea hivi: “Kisha kutambua jambo hilo, utashangaa kuona kwamba anatuhangaikia sana!”

19. Ni jambo lingine gani lenye tunapaswa kufanya ili tuone mukono wa Mungu?

19 Yesu alisema kwamba wale ‘watamuona Mungu’ wanapaswa kuwa “safi moyoni.” (Mathayo 5:8) Hilo linamaanisha nini? Tunapaswa kuendelea kuwa na mawazo safi na kuacha kufanya mambo mabaya. (Soma 2 Wakorintho 4:2.) Katika habari hii, tumejifunza kwamba ili tuone mukono wa Mungu, tunapaswa kutia nguvu urafiki wetu pamoja naye. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna imani inaweza kutusaidia kuona waziwazi mukono wa Yehova katika maisha yetu.

MAFASIRIO YA MANENO FULANI

  • Tunaona mukono wa Mungu katika maisha yetu wakati tunatambua namna anajibu sala zetu na namna anatusaidia

  • Tunamuona Yehova kupitia macho ya moyo wakati tunafikia kabisa kumujua yeye na sifa zake

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine