HABARI YA KUJIFUNZA YA 21
Namna Yehova Anajibiaka Sala Zetu
“Tunajua kwamba tutapata mambo yenye tuliomba, kwa kuwa tumeyaomba kwake.”—1 YO. 5:15.
WIMBO 41 Tafazali, Sikia Sala Yangu
KIFUPI YA HABARIa
1-2. Tunaweza kujiuliza maulizo gani kuhusu sala zetu?
ULISHAKAJIULIZA ikiwa Yehova iko najibia sala zako ao hapana? Kama ni vile, hauko weye peke. Ndugu na dada wengi walishakajiuliza vile, zaidi sana wakati walikuwa mu magumu. Kama tuko nateseka, inaweza pia kuwa nguvu kwetu kuona namna Yehova iko najibia sala zetu.
2 Tuone juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova anajibiaka sala za waabudu wake. (1 Yo. 5:15) Tutaona pia hii maulizo: Juu ya nini wakati fulani inaweza kuonekana sawa vile Yehova hajibie sala zetu? Yehova anajibiaka sala mu njia gani leo?
PENGINE YEHOVA HATAJIBIA MU NJIA YENYE TUNATAZAMIA
3. Juu ya nini Yehova anapenda tusali kwake?
3 Maandiko inatuhakikishia kama Yehova anatupendaka sana na kama anatuona kuwa wa maana sana. (Hag. 2:7; 1 Yo. 4:10) Njo maana anatuambia tusali kwake ili kumuomba musaada. (1 Pe. 5:6, 7) Anapenda kutusaidia tumukaribie na tuvumilie magumu yenye tuko napata.
Yehova alijibia sala za Daudi kwa kumukomboa mu mikono ya maadui wake (Ona fungu ya 4)
4. Tunajua namna gani kama Yehova anajibiaka sala za waabudu wake? (Ona pia picha.)
4 Mu Biblia tunasomaka kama Yehova alikuwaka najibia sala za waabudu wake. Unakumbuka mufano fulani? Mufano moya ni wa Mufalme Daudi. Alikuwa na maadui wengi hatari mu maisha yake, na kila mara alikuwa namuomba Yehova musaada. Siku moya alisali hivi: “Ee Yehova, sikia sala yangu; sikiliza kilio changu cha kuomba musaada. Unijibu katika uaminifu wako na katika haki yako.” (Zb. 143:1) Yehova alijibia sala za Daudi kwa kumukomboa. (1 Sa. 19:10, 18-20; 2 Sa. 5:17-25) Njo maana Daudi alisema hivi kwa uhakika: “Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia.” Na siye pia tunaweza kuwa na ule uhakika.—Zb. 145:18.
Yehova alijibia sala za Paulo kwa kumupatia nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kuvumilia (Ona fungu ya 5)
5. Kila mara Yehova alikuwa najibia sala za waabudu wake wa zamani mu njia yenye walitazamia? Leta mufano. (Ona pia picha.)
5 Pengine Yehova hatajibia sala zetu mu njia yenye tunatazamia. Ile njo ilimufikia mutume Paulo. Alimuomba Mungu amutoshe “mwiba katika mwili.” Paulo alisali mara tatu juu ya ile magumu. Yehova alijibia sala zake? Ndiyo. Lakini, hakumujibia mu njia yenye alitazamia. Kuliko kutosha ile magumu, Yehova alimupatia nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili aendelee kumutumikia kwa uaminifu.—2 Ko. 12:7-10.
6. Juu ya nini wakati fulani inaweza kuonekana sawa vile Yehova hajibie sala zetu?
6 Wakati fulani, Yehova anaweza pia kujibia sala zetu mu njia yenye hatutazamie. Tuko hakika kama anajua njia ya muzuri zaidi ya kutusaidia. Anaweza hata “kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote yenye tunaomba ao yenye tunafikiri.” (Efe. 3:20) Njo maana, anaweza kujibia sala zetu wakati ao mu njia yenye hatutazamie.
7. Juu ya nini inaweza kuwa muzuri kubadilisha mambo yenye tuko namuomba Yehova? Leta mufano.
7 Tunaweza kubadilisha mambo yenye tuko namuomba Yehova wakati tunatambua waziwazi mapenzi yake. Fikiria mufano wa Martin Poetzinger. Kisha tu kuoa, alifungwa mu kambi ya mateso ya nazi. Ku mwanzo, alimuombaka Yehova amusaidie atoke mu ile kambi juu ahangaikie bibi yake na aanze tena kazi ya kuhubiri. Lakini, kisha majuma mbili hakuona jambo yoyote yenye ilionyesha kama Yehova atamusaidia atoke. Kwa hiyo alianza kusali hivi: “Yehova, tafazali unionyeshe mambo yenye unapenda nifanye.” Kisha alianza kufikiri juu ya magumu yenye ndugu wengine mu ile kambi walikuwa napata. Wengi kati yao walihangaika sana juu ya bibi zao na watoto wao. Kisha, alisali hivi: “Yehova, aksanti kwa kunipatia mugao wa mupya. Unisaidie ili nitie moyo ndugu zangu.” Alipitisha miaka kenda yenye ilifuata mu ile kambi na iko natia moyo ndugu zake!
8. Ni jambo gani ya maana yenye hatupaswe kusahau wakati tuko nasali?
8 Hatupaswe kusahau kama Yehova iko na kusudi, na ataitimiza kulingana na wakati wenye alishaweka. Ile kusudi yake ni kumaliza kabisa magumu yote yenye iko nafanya watu wateseke leo, sawa vile misiba ya asili, magonjwa na kifo. Yehova atatimiza ile kusudi kupitia Ufalme wake. (Da. 2:44; Ufu. 21:3, 4) Lakini, mbele ile wakati ifike anaruhusu Shetani atawale dunia.b (Yoh. 12:31; Ufu. 12:9) Kama Yehova anamaliza magumu yote ya wanadamu leo, itaonekana sawa vile Shetani iko natawala muzuri dunia. Lakini, hata kama tunapaswa kungoya Yehova atimize ahadi fulani, ile haimaanishe kama haiko natusaidia. Tuone basi njia fulani zenye Yehova anatumiaka ili kutusaidia.
NJIA ZENYE YEHOVA ANATUMIAKA ILI KUJIBIA SALA LEO
9. Yehova anatusaidiaka namna gani wakati tunataka kukamata maamuzi? Fasiria.
9 Anatupatiaka hekima. Yehova anaahidi kama atatupatia hekima yenye tuko nayo lazima ili tukamate maamuzi ya muzuri. Tuko kabisa na lazima ya hekima yenye kutoka kwa Mungu wakati tuko nakamata maamuzi yenye itakuwa na matokeo mu maisha yetu, sawa vile kuamua ikiwa tutafunga ndoa ao hapana. (Yak. 1:5) Fikiria mufano wa dada Maria mwenye hayaolewa.c Alikuwa natumika kwa furaha kazi ya upainia wa kawaida. Na ni mu ile wakati njo alikutana na ndugu fulani. Anasema hivi: “Kadiri urafiki wetu ulikuwa nakomala, ni vile tulivutiana. Nilijua kama nilipaswa kukamata uamuzi. Nilisali sana juu ya ile jambo. Nilikuwa na lazima ya muongozo wa Yehova, lakini, nilijua pia kama Yehova hatanikamatia uamuzi.” Aliona kama Yehova alijibia sala zake kwa kumupatia hekima. Namna gani? Wakati alitafuta habari mu vichapo vyetu, alipata habari zenye zilijibia maulizo yenye alikuwa nayo. Alisikiliza pia mashauri ya hekima ya mama yake mwenye alikuwa muaminifu. Ile mashauri ilimusaidia Maria achunguze hisia zake. Ku mwisho, alikamata uamuzi wa hekima.
Namna gani Yehova anatupatiaka nguvu ya kuvumilia? (Ona fungu ya 10)
10. Kulingana na Wafilipi 4:13, Yehova anafanyaka nini ili kusaidia waabudu wake? Leta mufano. (Ona pia picha.)
10 Anatupatiaka nguvu ya kuvumilia. Yehova atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia magumu yetu sawa vile tu alimusaidiaka mutume Paulo. (Soma Wafilipi 4:13.) Fikiria namna Yehova alimusaidiaka ndugu Benjamin kuvumilia magumu ya nguvu. Karibu ujana wake wote, yeye na familia yake, waliishi mu kambi za wakimbizi mu Afrika. Benjamin anasema hivi: “Nilimuomba Yehova bila kuacha anipatie nguvu ya kufanya mambo yenye itamufurahisha. Yehova alijibia sala zangu kwa kunipatia amani ya akili, uhodari wa kuendelea kuhubiri, na alinisaidia nipate vichapo vya kunisaidia niendelee kuwa nguvu kiroho.” Anasema tena hivi: “Kusoma habari juu ya Mashahidi wenzangu na kuona namna Yehova aliwasaidia kuvumilia, kulifanya niazimie kabisa kuendelea kuwa muaminifu.”
Yehova alishakakusaidia kupitia waamini wenzako? (Ona fungu ya 11-12)d
11-12. Ni mu njia gani Yehova anaweza kutumia ndugu na dada zetu ili kujibia sala zetu? (Ona pia picha.)
11 Anatumiaka ndugu na dada zetu. Usiku mbele Yesu atoe uzima wake, alisali sana. Alimuomba Yehova asiruhusu watu wamuhukumu kwa kusema kama alitukana Mungu. Yehova hakuzuia ile, lakini, alimusaidia Yesu kwa kumutumia malaika ili amutie nguvu. (Lu. 22:42, 43) Yehova anaweza pia kutusaidia kwa kutumia ndugu na dada zetu wenye wanaweza kututembelea ao kutuita ku telefone ili kututia moyo. Siye wote tunaweza kutafuta nafasi za kuambia waamini wenzetu “neno la muzuri”.—Mez. 12:25.
12 Fikiria mufano wa dada Miriam. Majuma fulani kisha bwana yake kufa, alibakia yeye peke na alikuwa na huzuni na mwenye kushuka moyo. Alikuwa tu nalia na alikuwa na lazima ya kuongea na mutu fulani. Anasema hivi: “Sikukuwa hata na nguvu ya kuita mutu yeyote ku telefone, kwa hiyo nilisali kwa Yehova. Wakati nilikuwa nalia na kusali, telefone yangu ililia. Ni muzee moya njo aliniita, alikuwa rafiki.” Ule muzee na bibi yake walimufariji Miriam. Alikuwa hakika kama Yehova njo alichochea ule muzee amuite.
Namna gani Yehova anaweza kuchochea wengine watusaidie? (Ona fungu ya 13-14)
13. Leta mufano wenye unaonyesha namna Yehova anaweza kutumia wale wenye hawamuabudu ili kujibia sala zetu?
13 Anaweza kutumia watu wenye hawamuabudu. (Mez. 21:1) Wakati fulani Yehova anajibiaka sala za waabudu wake kwa kuchochea watu wenye hawamuabudu ili wawasaidie. Kwa mufano, alichochea Mufalme Artashasta amupatie Nehemia ruhusa ya kurudia Yerusalemu ili kujenga upya ule muji. (Ne. 2:3-6) Leo pia, Yehova anaweza kuchochea hata wale wenye hawamuabudu ili watusaidie wakati tuko na lazima ya musaada.
14. Unafurahia nini mu habari ya Soo Hing? (Ona pia picha.)
14 Dada Soo Hing aliona kama Yehova alimusaidia kupitia munganga wake. Mutoto wake alikuwa na magonjwa mbalimbali ya akili. Wakati ule mutoto alifanya aksida ya nguvu yenye ilifanya agonjwe tena sana, Soo Hing na bwana yake waliacha kazi juu wamuhangaikie. Ile ilifanya ikuwe nguvu kwao kupata makuta. Soo Hing alisema kama ile magumu ilimufikisha kabisa ku mwisho. Alimufungulia Yehova moyo wake kwa kumuomba musaada. Ule munganga alifikiria namna ya kumusaidia yeye na familia yake. Ile ilifanya serikali iwapatie musaada na nyumba ya kulipia ya bei ya chini. Kisha, Soo Hing alisema hivi: “Tuliona mukono wa Yehova mu magumu yetu. Kwa kweli, yeye ni ‘Musikiaji wa sala.’”—Zb. 65:2.
INAOMBA IMANI ILI KUONA NA KUKUBALI JIBU YA YEHOVA
15. Nini njo ilisaidia dada moya aone kama Yehova alikuwa najibia sala zake?
15 Yehova hajibiake kila mara sala zetu mu njia ya ajabu. Lakini, majibu yenye anatupatiaka njo yenye tunakuwaka nayo lazima kabisa ili tuendelee kuwa washikamanifu kwake. Kwa hiyo, ujikaze kuona namna Yehova anajibiaka sala zako. Dada Yoko aliona kama Yehova hakukuwa najibia sala zake, lakini kisha, alianza kuandika mambo yenye alikuwa namuomba Yehova. Kisha wakati fulani kupita, aliangalia fasi kwenye aliandikaka ile mambo na aliona kama Yehova alikuwa amejibia mingi kati ya sala zake hata zile zenye alikuwa alishasahau. Kila mara, tunapaswa kutua na kufikiri juu ya namna Yehova iko najibia sala zetu.—Zb. 66:19, 20.
16. Tunaweza kuonyesha namna gani kama tuko na imani wakati tunasali? (Waebrania 11:6)
16 Tunaonyesha kama tuko na imani, hapana tu kwa kusali kwa Yehova, lakini pia kwa kukubali jibu yenye anatupatia hata ikuwe ya namna gani. (Soma Waebrania 11:6.) Fikiria mufano wa Mike na bibi yake, Chrissy. Walikuwa na muradi wa kutumika ku Beteli. Mike anasema hivi: “Tulijaza fomu mara mingi na tulimuomba Yehova tena na tena ili atusaidie kufikia ule muradi, lakini hatukualikwa.” Mike na Chrissy walikuwa hakika kama Yehova anajua njia ya muzuri sana ya kuwatumikisha mu utumishi wake. Walifanya yote yenye waliweza mu kazi ya upainia wa kawaida fasi kwenye kulikuwa lazima kubwa na walisaidia mu kazi ya ujenzi. Leo wako mu kazi ya muzunguko. Mike anasema hivi: “Yehova hakujibia sala zetu mu njia yenye tulitazamia, lakini alizijibia mu njia za muzuri zaidi kuliko vile tuliwazia.”
17-18. Kulingana na Zaburi 86:6, 7, tuko hakika na jambo gani?
17 Soma Zaburi 86:6, 7. Muandikaji wa zaburi Daudi alikuwa hakika kama Yehova alisikia na kujibia sala zake. Na weye ukuwe hakika kama Yehova atafanya vile. Mifano yenye tunazungumuzia mu hii habari inatuhakikishia kama Yehova anaweza kutupatia hekima na nguvu yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia. Anaweza kutumia ndugu na dada zetu ao hata wale wenye hawamuabudu kwa sasa ili kutusaidia mu njia fulani.
18 Pengine Yehova hatajibia sala zetu mu njia yenye tunatazamia, hata vile tunajua kama atazijibia. Atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima kabisa wakati wenye tuko nayo lazima. Kwa hiyo, uendelee kusali na kuamini kama Yehova atakusikia, ukuwe hakika kama atakuhangaikia sasa, na kama ‘atatimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima’ mu dunia mupya.—Zb. 145:16.
WIMBO 46 Aksanti Yehova
a Yehova anatuhakikishia kama atajibia sala zetu ikiwa zinapatana na mapenzi yake. Wakati tunapata magumu, tunaweza kuwa hakika kama atatusaidia ili tuendelee kuwa waaminifu kwake. Tuone basi namna Yehova anajibiaka sala zetu.
b Juu upate sababu zenye zinafanya Yehova aruhusu Shetani atawale dunia, soma habari “Kaza Macho Yako juu ya Jambo la Maana,” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 6, 2017.
c Majina fulani imebadilishwa.
d MAFASIRIO YA PICHA Ukurasa wa 11: Mama na mutoto wake mwanamuke wanafika mu inchi ingine na wanakuwa wakimbizi. Waamini wenzao wanawakaribisha kwa uchangamufu na wanawasaidia.