Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwfq habari 18
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?
  • Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mawazo ya watu wengi
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?
  • Juu ya nini mutu akubali kuchukiwa juu tu ya kukatala kusherehekea Noeli?
  • Shuguli za Watu Wakati wa Noeli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Noeli ni ya Wakristo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
ijwfq habari 18
Wazazi wako naongea na mutoto wao kijana wakati iko nafungula zawadi fulani.

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?

Mawazo ya watu wengi

Uongo: Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Noeli juu hawamuamini Yesu.

Ukweli: Tuko Wakristo. Tunaamini kama wokovu unapatikana kupitia tu Yesu Kristo.—Matendo 4:12.

Uongo: Munagawanya familia kwa kufundisha watu wasisherehekee Noeli.

Ukweli: Tunahangaikia sana familia na tunatumia Biblia juu ya kuzisaidia zikuwe nguvu.

Uongo: Munakosaka mambo ya muzuri ya mu “Noeli”, sawa vile kuonyesha ukarimu, kutakia watu amani mu dunia na kutendea watu mambo ya muzuri.

Ukweli: Tunajikazaka kuwa wakarimu na wenye kufanya amani kila siku. (Mezali 11:25; Waroma 12:18) Kwa mufano, namna yetu ya kuongoza mikutano na kuhubiri inapatana na hii agizo ya Yesu: “Mulipokea bure, mutoe bure.” (Matayo 10:8) Zaidi ya ile, tunaelewa kama Ufalme wa Mungu tu njo utaleta amani ku dunia.​—Matayo 10:7.

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?

  • Yesu alitupatia amri ya kukumbuka kifo yake, hapana kuzaliwa kwake.​—Luka 22:19, 20.

  • Mitume na wanafunzi wa kwanza wa Yesu, hawakukuwa nasherehekea Noeli. Kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema kama “watu walianza kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu mu 243 [K.K.Y.],” karne moya kisha mutume wa mwisho kufa.

  • Hakuna ushuhuda wenye kuonyesha kama Yesu alizaliwa tarehe 25, Mwezi wa 12; tarehe yake ya kuzaliwa haiandikwe mu Biblia.

  • Tunaamini kama Mungu hakubali Noeli juu inatokana na desturi za kipagani.​—2 Wakorinto 6:17.

Juu ya nini mutu akubali kuchukiwa juu tu ya kukatala kusherehekea Noeli?

Watu wengi wanaendelea kusherehekea Noeli hata kama wanajua kwamba inatokana na desturi za kipagani na haitegemezwe na Biblia. Wale watu wanaweza kujiuliza: Juu ya nini wakristo wanakubali kuchukiwa juu tu ya kukatala kusherehekea Noeli?

Biblia inatutia moyo tufikiri, tutumie ‘nguvu zetu za kufikiri’. (Waroma 12:1, 2) Inatufundisha kuisamini kweli. (Yohana 4:23, 24) Ni kweli tunahangaikiaka namna watu wanatuona, lakini tunajikaza kushikamana na kanuni za Biblia hata kama ile inaweza kufanya wengine watuchukie.

Hata kama hatusherehekeake Noeli, tunaheshimia haki ya kila mutu ya kujiamulia ikiwa ataisherehekea ao hapana. Hatuzuie wengine kuisherehekea.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine