Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 56
  • Je, Shetani Anaweza Kuwatawala Wanadamu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Shetani Anaweza Kuwatawala Wanadamu?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Je, Shetani Iko Kabisa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Umupinge Ibilisi
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 56

Je, Shetani Anaweza Kuwatawala Wanadamu?

Jibu la Biblia

Shetani na mashetani wanaongoza watu wafanye mabaya sana. Kwa hiyo Biblia inasema: ‘Yule Muovu anautawala ulimwengu wote.’ (1 Yohana 5:​19, New Century Version) Biblia inaonyesha njia ambazo Shetani anatumia ili kuwatawala watu.

  • Ujanja. Biblia inatia Wakristo moyo ‘wapambane na ujanja wa Shetani.’ (Waefeso 6:​11, NCV) Njia moja ya ujanja ambayo anatumia ni kuwafanya watu waamini kwamba watu wake ni watumishi wa Mungu.​—2 Wakorintho 11:13-​15.

  • Kupashana habari na mashetani. Shetani anadanganya watu kupitia wachawi, watu wa kutabiri mambo, na wote wanaotumia uaguzi ao wale wanaochunguza nyota. (Kumbukumbu 18:10-​12) Matumizi ya dawa za kulewesha, kulalisha usingizi, njia zingine za kupoteza akili zinafanya pia mutu aongozwe na mashetani.​—Luka 11:24-​26.

  • Dini ya uongo. Dini zinazofundisha mambo ya uongo zinawafanya watu wasimutii Mungu. (1 Wakorintho 10:20) Biblia inaita mambo hayo ya uongo kuwa “mafundisho ya roho waovu.”​—1 Timotheo 4:1.

  • Kuingia katika watu. Biblia inasimulia habari za roho waovu wanaoingia katika watu na kuwaongoza. Wakati mwengine mashetani yanafanya watu kuwa vipofu ao mabubu na hata kuwafanya wajiumize.​—Mathayo 12:22; Marko 5:​2-5.

Namna ya kuepuka kuongozwa na Shetani

Usiogope mashetani, kwa kuwa Biblia inaonyesha namna unavyoweza kumupinga kabisa Shetani:

  • Jifunze njia za Shetani ili ‘usikose kujua mbinu zake.’​—2 Wakorintho 2:​11.

  • Jifunze Biblia na kisha utumie mambo unayojifunza. Tumia kanuni za Biblia ili zikuepushe na uvutano mubaya wa Shetani.​—Waefeso 6:​11-​18.

  • Achana kabisa na kila kitu kinachoweza kukuunganisha na mashetani. (Matendo 19:19) Hiyo inatia ndani, muziki, vitabu, magazeti, picha, na video zinazohusu kupashana habari na mashetani.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine