Siku ya Posho, 13 Mwezi wa 9
Wewe ni mutu mwenye samani sana.—Da. 9:23.
Wakati nabii Danieli alikuwa angali kijana, Wababiloni walimufunga na kumupeleka mu muji wao wenye ulikuwa mbali na Yerusalemu. Lakini, Danieli alishangaza wale wenye walimufunga. Waliona “kile chenye [kinaonekana] kwa macho,” ni kusema, waliona kama Danieli “hakukuwa na kasoro yoyote, alikuwa na sura ya muzuri,” na kama alitoka mu familia yenye kuheshimiwa. (1 Sa. 16:7) Njo maana, Wababiloni walimuzoeza ili aanze kutumika mu nyumba ya Kifalme. (Da. 1:3, 4, 6) Yehova alimupenda Danieli juu alichagua kuwa mushikamanifu kwake. Kwa kweli, inawezekana Danieli alikuwa tu na miaka 20 hivi wakati Yehova alimuona kuwa mwenye haki, sawa vile Noa na Yobu, wanaume wenye walimutumikia kwa uaminifu kwa miaka mingi. (Mwa. 5:32; 6:9, 10; Yob. 42:16, 17; Eze. 14:14) Na Yehova aliendelea kumupenda Danieli mu maisha yake yote yenye ilikuwa ya murefu na ya maana.—Da. 10:11, 19. w23.08 2 fu. 1-2
Siku ya Yenga, 14 Mwezi wa 9
Elewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini.—Efe. 3:18.
Wakati unataka kuamua ikiwa utauza nyumba fulani ao hapana. Itakuwa lazima uchunguze kila sehemu ya nyumba yenye unapenda kuuza. Hapana kupitia video lakini kwa kufika mahali kwenye kuko ile nyumba. Tunaweza pia kufanya vile wakati tuko nasoma na kujifunza Biblia. Kama unaisoma mbiombio pengine utajifunza tu kweli za musingi, ni kusema “mambo ya musingi ya maneno matakatifu ya Mungu.” (Ebr. 5:12) Kuliko kufanya vile, sawa vile mutu anaweza kufanya kuhusu nyumba, ingia “ndani” ili uchunguze mambo yote ya maana. Njia ya muzuri ya kujifunza Biblia ni kuona namna sehemu zake mbalimbali zinapatana. Usitafute tu kujua ni kweli gani unaamini, lakini pia juu ya nini unaziamini. Ili kuelewa Neno ya Mungu kwa undani kabisa, unapaswa kujifunza mafundisho mazito ya Biblia. Mutume Paulo alitia moyo ndugu na dada zake wajifunze Neno ya Mungu kwa uangalifu ili waweze “kuelewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini” wa kweli. Na ile ingefanya wafikie kuwa “na mizizi na kufanywa imara” katika imani yao. (Efe. 3:14-19) Siye pia tunapaswa kufanya vile. w23.10 18 fu. 1-3
Siku ya Kwanza, 15 Mwezi wa 9
Ndugu, kuhusu kuvumulia uovu na kuwa wavumilivu, mufuate mufano wa wale manabii wenye walisema katika jina la Yehova.—Yak. 5:10.
Biblia iko na mifano mingi ya watu wenye walikuwaka na uvumilivu. Hauone kama ni jambo ya muzuri kama unajiwekea muradi wa kujifunza ile mifano? Kwa mufano, hata kama Daudi alitiwa mafuta wakati alikuwa angali kijana sana ili akuwe mufalme wa Israeli, alipaswa kungoya miaka mingi mbele akuwe mufalme. Simeoni na Ana walimuabudu Yehova kwa uaminifu wakati walikuwa nangoya Masiya mwenye aliahidiwa. (Lu. 2:25, 36-38) Wakati utakuwa najifunza ile mifano, tafuta majibu ya hii maulizo: Pengine ni nini ilisaidia huyu mutu aonyeshe uvumilivu? Alipata faida gani juu alikuwa na uvumilivu? Namna gani naweza kumuiga? Unaweza pia kupata faida kwa kujifunza kuhusu wale wenye hawakuonyesha uvumilivu. (1 Sa. 13:8-14) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Nini njo ilifanya wale watu washindwe kuonyesha uvumilivu? Ni matokeo gani ya mubaya yenye walipata juu hawakukuwa na uvumilivu?’ w23.08 25 fu. 15