Siku ya Kwanza, 13 Mwezi wa 10
Yehova anaona ndani ya moyo.—1 Sa. 16:7.
Ikiwa wakati fulani tunajiona kuwa watu wa bure, tukumbuke kama ni Yehova njo alituvuta kwake. (Yoh. 6:44) Anaona jambo fulani ya muzuri ndani yetu, jambo fulani yenye pengine siye wenyewe hatuone, na anajua moyo wetu. (2 Ny. 6:30) Kwa hiyo tunaweza kumuamini wakati anasema kama tuko wa maana. (1 Yo. 3:19, 20) Mbele ya kujifunza kweli, wamoja kati yetu walifanya mambo yenye pengine wanaendelea kuhuzunikia mupaka leo. (1 Pe. 4:3) Hata Wakristo waaminifu wanapiganisha muelekeo wa kufanya zambi. Moyo wako uko nakuhukumu? Kama ni vile, usivunjike moyo. Ujue kama hata watumishi fulani wa Yehova walijisikia vile. Kwa mufano, mutume Paulo alijiona kuwa wa bure wakati alifikiria uzaifu wake. (Ro. 7:24) Kwa kweli, Paulo alikuwa ametubu zambi zake na kubatizwa. Lakini, aliendelea kujiona kuwa “mudogo zaidi kati ya mitume” na mutenda-zambi “wa kwanza kabisa.”—1 Ko. 15:9; 1 Ti. 1:15. w24.03 27 fu. 5-6
Siku ya Pili, 14 Mwezi wa 10
Wakaacha nyumba ya Yehova Mungu.—2 Ny. 24:18.
Jambo moya yenye uamuzi mubaya wa Mufalme Yehoashi unaweza kutufundisha ni kama tunapaswa kuchagua marafiki wenye watatuchochea kufanya mambo ya muzuri; marafiki wenye wanamupenda Yehova na wenye wanapenda kumufurahisha. Haiko lazima marafiki wetu wakuwe tu wa miaka yetu. Kumbuka kama Yehoashi alikuwa mudogo sana kuliko rafiki yake Yehoyada. Fikiria marafiki wenye uko nao kisha ujiulize hii maulizo: ‘Wananisaidia ili imani yangu kwa Yehova ikuwe nguvu zaidi? Wananitia moyo nitumikishe kanuni za Mungu mu maisha yangu? Wanazungumuzia kuhusu Yehova na kweli za Biblia? Wanaheshimia kanuni za Mungu? Wananiambia tu mambo yenye ninapenda kusikia ao wako tayari kunirekebisha kama ninafanya makosa?’ (Mez. 27:5, 6, 17) Kusema kweli, hauna lazima ya marafiki wenye hawamupendi Yehova. Lakini kama uko na marafiki wenye wanamupenda Yehova, ushikamane nao; watakusaidia sana!—Mez. 13:20. w23.09 9-10 fu. 6-7
Siku ya Tatu, 15 Mwezi wa 10
Mimi ndiye Alfa na Omega.—Ufu. 1:8.
Alfa njo herufi ya kwanza mu alfabeti ya Kigiriki na omega njo herufi ya mwisho. Kwa kutumia maneno “Alfa na Omega,” Yehova anaonyesha kama wakati anaanza jambo fulani anaendelea nayo mupaka ifikie mwisho kabisa. Kisha Yehova kuumba Adamu na Eva akawaambia: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.” (Mwa. 1:28) Ile wakati ni sawa vile Yehova alisema “Alfa.” Alionyesha waziwazi kusudi yake: Kutakuwa wakati wenye wazao wa Adamu na Eva wenye kuwa wakamilifu na watiifu watajaza dunia na kuifanya kuwa Paradiso. Wakati ile itatimia ni sawa vile atasema “Omega.” Kisha kumaliza kuumba “mbingu na dunia pamoja na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake,” Yehova alisema jambo fulani yenye ilihakikisha kama kusudi yake itatimia kabisa. Yehova alitoa uhakikisho kama bila shaka angetimiza kusudi yake kwa wanadamu na dunia. Ingetimia kabisa ku mwisho wa siku ya saba.—Mwa. 2:1-3. w23.11 5 fu. 13-14