Mwezi wa 10
Siku ya Tatu, 1 Mwezi wa 10
Hekima yenye inatoka juu ni . . . tayari kutii.—Yak. 3:17.
Wakati fulani inakuwaka nguvu kwako kutii? Ile ilimufikia Mufalme Daudi, njo maana alimuomba Yehova hivi: “Uchochee ndani yangu utayari wa kukutii.” (Zb. 51:12) Daudi alimupenda Yehova. Hata vile, wakati fulani ilikuwa nguvu kwake kutii, na ni vile mambo inakuwaka pia kwetu. Juu ya nini? Kwanza, tuliriti muelekeo wa kutotii. Pili, Shetani anaendelea kujaribu kutuchochea tuasi, sawa vile yeye alifanya. (2 Ko. 11:3) Tatu, mu hii dunia tunazungukwa na watu wenye kuwa na muelekeo wa kutotii, “roho yenye sasa inatenda katika wana wa kukosa kutii.” (Efe. 2:2) Tunapaswa kujikaza sana ili kupiganisha muelekeo wetu wa kufanya zambi, lakini pia tunapaswa kujikaza ili kupiganisha roho ya kukosa kutii yenye Shetani na huu ulimwengu wanachochea. Tunapaswa kufanya yetu yote ili kumutii Yehova na wale wenye amepatia mamlaka fulani. w23.10 6 fu. 1
Siku ya Ine, 2 Mwezi wa 10
Umeweka divai ya muzuri mupaka sasa.—Yoh. 2:10.
Muujiza wa Yesu wa kugeuza maji kuwa divai unatufundisha nini? Tunajifunza somo ya unyenyekevu. Yesu hakujisifu juu ya ule muujiza; na kusema kweli, hakuna hata siku moya yenye alijisifu juu ya mambo yenye alikuwa nafanya. Lakini, juu alikuwa munyenyekevu, kila mara alimupatia Baba yake utukufu na sifa yote. (Yoh. 5:19, 30; 8:28) Kama tunaiga Yesu kwa kuendelea kuwa wanyenyekevu, hatutajisifu wakati tunafanya mambo fulani ya muzuri. Tujisifu juu ya pendeleo yenye tuko nayo ya kumutumikia Mungu wetu wa ajabu, hapana kujisifu juu yetu siye wenyewe. (Yer. 9:23, 24) Yeye njo tunapaswa kupatia sifa yote. Zaidi ya ile, kuko jambo fulani yenye tunaweza kutimiza bila musaada wa Yehova? (1 Ko. 1:26-31) Kama tuko wanyenyekevu, hatutajisifu juu ya mambo ya muzuri yenye tunafanyia wengine. Tutafurahi kujua kama Yehova anaona na anasamini mambo yenye tunafanya. (Linganisha na Matayo 6:2-4; Ebr. 13:16.) Kusema kweli, tutamufurahisha Yehova kama tunamuiga Yesu kwa kuwa wanyenyekevu.—1 Pe. 5:6. w23.04 4 fu. 9; 5 fu. 11-12
Siku ya Tano, 3 Mwezi wa 10
Muendelee kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.—Flp. 2:4.
Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuonyesha kama Wakristo wanapaswa kutafuta faida za wengine. Tunaweza kufanya nini ili kutumikisha ile shauri ku mikutano? Kwa kukumbuka kama wengine pia wanapenda kutoa maelezo. Fikiria ile jambo mu hii njia. Wakati uko naongea na marafiki wako, utasema mingi sana mupaka wakose nafasi ya kusema? Hapana, juu unapenda nao pia waseme. Vilevile, tunapenda kuachia wengine nafasi ya kutoa maelezo ku mikutano kadiri inawezekana. Kusema kweli, njia moya kati ya njia za muzuri za kutia moyo ndugu na dada zetu ni kuwapatia nafasi ya kutoa maelezo yenye kuonyesha imani yao. (1 Ko. 10:24) Tutoe maelezo ya mufupi juu tupatie watu wengi zaidi nafasi ya kutoa pia maelezo. Hata wakati unatoa maelezo ya mufupi, epuka kuzungumuzia mawazo mingi sana. Kama unazungumuzia mawazo mingi sana yenye kuwa mu fungu, hakutabakia mambo mingi yenye wengine watasema. w23.04 22-23 fu. 11-13
Siku ya Posho, 4 Mwezi wa 10
Ninafanya mambo yote kwa ajili ya habari njema, ili niishiriki pamoja na wengine.—1 Ko. 9:23.
Tunapaswa kukumbuka kama ni jambo ya maana kuendelea kusaidia wengine, zaidi sana kwa kuhubiri habari njema.Tunapaswa kuwa na usawaziko mu mahubiri. Tunahubiriaka watu wenye kuwa na mawazo tofauti juu ya Mungu na wenye wanatoka fasi mbalimbali ao wa desturi mbalimbali. Tunaweza kumuiga Paulo, mwenye alikuwa anajipatanisha na hali. Yesu alimuweka Paulo kuwa “mutume kwa mataifa.” (Ro. 11:13) Kwa hiyo, Paulo alihubiria Wayahudi, Wagiriki, watu wenye elimu, watu wa mu vijiji, wakubwa wa serikali, na wafalme. Juu ya kugusa mioyo ya wale watu wote, Paulo alifikia “kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote.” (1 Ko. 9:19-22) Alifikiria kwa uangalifu fasi kwenye watu wenye alikuwa nazungumuza nao walitoka na mambo yenye waliamini; na ile ilimusaidia akuwe na usawaziko ili kuzungumuza na kila mumoja wao mu njia yenye ingemuvuta katika kweli. Siye pia tunaweza kupata matokeo ya muzuri mu mahubiri kama tuko na usawaziko na kama tuko najikaza kufikiria njia ya muzuri sana ya kusaidia kila mutu mwenye tunahubiria. w23.07 23 fu. 11-12
Siku ya Yenga, 5 Mwezi wa 10
Mutumwa wa Bwana hana lazima ya kupigana, lakini anapaswa kuwa mupole.—2 Ti. 2:24.
Mutu mupole haiko muzaifu, kwa sababu inaomba mutu akuwe na nguvu ya kujizuia ili abakie mwenye kutulia wakati anapambana na hali yenye inaweza kumufanya akasirike. Upole ni moja kati ya sifa za “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23) Neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa upole, ilikuwa natumiwa wakati fulani ili kuzungumuzia farasi mwenye amezoezwa ili aweze kutii. Fikiria farasi mwenye hayazoezwa mwenye kuwa na nguvu mingi. Kisha kuzoezwa anakuwa “mupole.” Ni mupole lakini angali tu na nguvu. Siye wanadamu, namna gani tunaweza kuwa wapole na wakati uleule kuwa wenye nguvu? Hatuwezi kufanya vile kwa nguvu yetu wenyewe. Tunapaswa kumuomba Mungu roho yake takatifu na kumuomba atusaidie tukomalishe ile sifa. Watu wengi wameweza kufanya vile. Mashahidi wengi walitenda kwa upole wakati walipambana na upinzani. Na ile ilifanya wengine wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova.—2 Ti. 2:24, 25. w23.09 15 fu. 3
Siku ya Kwanza, 6 Mwezi wa 10
Nilisali, . . . na Yehova akatimiza ombi langu lenye nilimuomba.—1 Sam. 1:27.
Mu maono yenye kushangaza, mutume Yohana aliona wazee 24 mbinguni na wako namuabudu Yehova. Walimusifu na kusema kama anastahili kupokea “utukufu na heshima na nguvu.” (Ufu. 4:10, 11) Malaika waaminifu wako apia na sababu mingi za kumusifu na kumuheshimia Yehova. Wako mbinguni pamoya naye na wamefikia kumujua muzuri. Wanaona sifa zake kupitia mambo yenye anafanya. Wakati wanaona namna Yehova iko natenda, ile inawachochea kumusifu. (Yob. 38:4-7) Siye pia tunapenda kumusifu Yehova mu sala zetu, kuonyesha mambo yenye tunapenda na mambo yenye tunafurahiaka kwake. Wakati unasoma na kujifunza Biblia, ujikaze kujua sifa za Yehova zenye unapendaka sana. (Yob. 37:23; Ro. 11:33) Kisha, umuambie namna unajisikiaka juu ya zile sifa. Tunaweza pia kumusifu juu anatusaidiaka na juu anasaidiaka pia ndugu na dada zetu Wakristo.—1 Sa. 2:1, 2. w23.05 3-4 fu. 6-7
Siku ya Pili, 7 Mwezi wa 10
Mutembee kwa namna yenye kumustahili Yehova.—Kol. 1:10.
Mu 1919, Babiloni Mukubwa haikukuwa tena na mamlaka juu ya watu wa Mungu. Mu ile mwaka, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” alianza kufanya kazi juu ya kusaidia watu wenye kuwa na mioyo ya muzuri waanze kutembea mu “Njia ya Utakatifu.” (Mt. 24:45-47; Isa. 35:8) Kazi ya “kutayarisha barabara” yenye ilifanywa zamani ilisaidia wale wenye walianza kutembea mu njia kubwa wamujue Yehova muzuri zaidi na makusudi yake. (Mez. 4:18) Walianza pia kuishi kulingana na mapenzi ya Yehova. Lakini, Yehova hakutazamia watu wake wafanye mabadiliko yote mara moya. Kuliko kufanya vile, alianza kuwasafisha pole kwa pole. Wazia namna siye wote tutakuwa na furaha wakati tutamufurahisha Mungu mu mambo yote! Juu barabara iendelee kuwa muzuri, inaombaka kuitengeneza kila mara. Kuanzia 1919, kazi yenye kufanywa mu “Njia ya Utakatifu” ingali inaendelea juu ya kusaidia watu wengi kadiri inawezekana watoke mu Babiloni Mukubwa. w23.05 17 fu. 15; 19 fu. 16
Siku ya Tatu, 8 Mwezi wa 10
Sitakuacha hata kidogo.—Ebr. 13:5.
Baraza Yenye Kuongoza iko nazoeza moja kwa moja wasaidizi wa mu halmashauri mbalimbali za Baraza Yenye Kuongoza. Leo wale wasaidizi wako nashugulikia madaraka makubwa mu tengenezo. Wametayarishwa muzuri ili waendeleze kazi ya kuhangaikia kondoo wa Kristo. Wakati mutiwa-mafuta wa mwisho ataenda mbinguni karibu na mwisho wa taabu kubwa, ibada safi itaendelea ku dunia. Chini ya uongozi wa Yesu Kristo, waabudu wa Yehova wataendelea kumutumikia. Ni kweli kwamba, ile wakati, tutashambuliwa na Gogu wa Magogu, muungano wa mataifa wenye kutuchukia. (Eze. 38:18-20) Lakini ile shambulio ya muda mufupi haitakuwa na matokeo; haitazuia watu wa Mungu kumuabudu Yehova. Bila shaka atawakomboa! Mu maono, mutume Yohana aliona “kundi kubwa” ya kondoo wengine wa Kristo. Yohana aliambiwa kama wale wenye kuwa mu ile “kundi kubwa” wanatoka “katika ile taabu kubwa.” (Ufu. 7:9, 14) Kwa kweli, tunajua kama Yehova atawaokoa! w24.02 5-6 fu. 13-14
Siku ya Ine, 9 Mwezi wa 10
Musizimishe moto wa roho.—1 Te. 5:19.
Tunapaswa kufanya nini ili tupate roho takatifu? Tunapaswa kumuomba Mungu atupatie ile roho, kujifunza Neno yake, na kujiunga na tengenezo yake yenye kuongozwa na roho. Kufanya vile kutatusaidia tuonyeshe “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23) Mungu anapatiaka tu roho takatifu wale wenye wanaendelea kuwa na mawazo na mwenendo muzuri. Hataendelea kupatia roho yake takatifu mutu mwenye iko na mawazo ya mubaya na mwenye iko na mwenendo mubaya. (1 Te. 4:7, 8) Juu Mungu aendelee kutupatia roho takatifu, tunapaswa pia kuepuka “kuzarau maneno ya unabii.” (1 Te. 5:20) Mu hii andiko, neno “unabii” maana yake ujumbe mbalimbali wenye Yehova anatupatia kupitia roho yake takatifu, kutia ndani mambo yenye inahusu siku yake na namna tunaweza kutenda kwa uharaka leo. Tusiwaze kama siku ya Yehova ao Armagedoni itakuyaka wakati tutakuwa tulishakufa. Kuliko kuwaza vile, tunaonyesha kama tunatazamia kuwa itakuya hivi karibuni ao tunaichunga kabisa mu akili yetu kwa kuendelea kuwa na “vitendo vya ushikamanifu kwa Munguna kwa kuendelea kuwa na mwenendo muzuri.”—2 Pe. 3:11, 12. w23.06 12 fu. 13-14
Siku ya Tano, 10 Mwezi wa 10
Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima.—Mez. 9:10.
Mukristo anapaswa kufanya nini kama anaona picha ya pornografia bila kutazamia? Anapaswa kuacha kuiagalia palepale. Jambo yenye inaweza kutusaidia kufanya vile ni kukumbuka kama urafiki wetu pamoya na Yehova njo jambo ya maana sana. Vilevile, hata picha fulani zenye zinaweza kuonekana sawa vile hazifanane picha za pornografia, zinaweza kulamusha tamaa ya kufanya uasherati. Juu ya nini tunapaswa kuziepuka? Juu hatupendi hata kidogo kufanya uzinifu mu moyo wetu. (Mt. 5:28, 29) David, muzee wa mu Tailandi anasema hivi: “Najiulizaka hivi: ‘Hata kama hizi picha hazifanane picha za pornografia, Yehova atafurahi kama naendelea kuziangalia?’ Kujiuliza vile kunanisaidiaka nitende kwa hekima.” Kuogopa kufanya jambo yoyote yenye itamuhuzunisha Yehova kutatusaidia tutende kwa hekima. Kumuogopa Mungu njo “mwanzo” ao musingi “wa hekima.” w23.06 23 fu. 12-13
Siku ya Posho, 11 Mwezi wa 10
Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani.—Isa. 26:20.
‘Vyumba vya ndani’ vinaweza kumaanisha makutaniko. Wakati wa taabu kubwa, tutapata ulinzi wenye Yehova anatuahidi kama tunaendelea kuungana na waamini wenzetu. Njo maana, kwa sasa, tunapaswa kujikaza sana kuvumilia ndugu na dada zetu lakini pia kuwapenda. Ile njo inaweza kufanya tuokoke! “Ile siku kubwa ya Yehova” itakuwa kipindi ya nguvu sana kwa wanadamu wote. (Sef. 1:14, 15) Watu wa Yehova watakuwa pia na magumu. Lakini, kama tunajitayarisha sasa, tutakuwa wenye kutulia na tutasaidia wengine. Tutavumilia magumu yote yenye tutakutana nayo. Wakati ndugu na dada zetu wanateseka, tutafanya yote yenye tunaweza ili kuwasaidia kwa kuwaonyesha huruma na kuwatolea musaada wenye wako nayo lazima. Na kama tunajifunza kupenda ndugu na dada zetu leo, tutaendelea kuwapenda hata wakati wenye kuya. Na ku mwisho, Yehova atatubariki kwa kutupatia uzima wa milele ku dunia kwenye misiba yote na taabu yote itakuwa ilishasahauliwa.—Isa. 65:17. w23.07 7 fu. 16-17
Siku ya Yenga, 12 Mwezi wa 10
[Yehova] atawafanya kuwa imara, atawatia nguvu, atawafanya ninyi musitikisike.—1 Pe. 5:10.
Mara mingi wakati Neno ya Mungu inazungumuzia watu waaminifu wa zamani, inasema kama walikuwa wenye nguvu. Lakini wakati fulani hata wenye nguvu zaidi kati yao, hawakujisikia kuwa na nguvu. Kwa mufano, wakati fulani Mufalme Daudi alijisikia kuwa “imara kama mulima,” lakini wakati mwingine “aliogopa sana.” (Zb. 30:7) Hata kama Samsoni alikuwa na nguvu mingi sana wakati alikuwa naongozwa na roho ya Mungu, alisema kama bila nguvu yenye kutoka kwa Mungu “atakuwa muzaifu na kuwa kama wanadamu wengine wote.” (Amu. 14:5, 6; 16:17) Wale wanaume waaminifu walikuwa wenye nguvu kwa sababu tu Yehova aliwapatia nguvu. Mutume Paulo alikubali kama alikuwa na lazima ya nguvu kutoka kwa Yehova. (2 Ko. 12:9, 10) Alipambana na magumu ya afya. (Gal. 4:13, 14) Wakati fulani, ilikuwa nguvu kwake kufanya mambo ya muzuri. (Ro. 7:18, 19) Na wakati ingine alikuwa na mahangaiko na hakujua ni nini itamufikia. (2 Ko. 1:8, 9) Hata vile, wakati Paulo alikuwa muzaifu, njo wakati alikuwa mwenye nguvu. Namna gani? Yehova alimupatia Paulo nguvu yenye alikuwa nayo lazima. Alimutia nguvu. w23.10 12 fu. 1-2
Siku ya Kwanza, 13 Mwezi wa 10
Yehova anaona ndani ya moyo.—1 Sa. 16:7.
Ikiwa wakati fulani tunajiona kuwa watu wa bure, tukumbuke kama ni Yehova njo alituvuta kwake. (Yoh. 6:44) Anaona jambo fulani ya muzuri ndani yetu, jambo fulani yenye pengine siye wenyewe hatuone, na anajua moyo wetu. (2 Ny. 6:30) Kwa hiyo tunaweza kumuamini wakati anasema kama tuko wa maana. (1 Yo. 3:19, 20) Mbele ya kujifunza kweli, wamoja kati yetu walifanya mambo yenye pengine wanaendelea kuhuzunikia mupaka leo. (1 Pe. 4:3) Hata Wakristo waaminifu wanapiganisha muelekeo wa kufanya zambi. Moyo wako uko nakuhukumu? Kama ni vile, usivunjike moyo. Ujue kama hata watumishi fulani wa Yehova walijisikia vile. Kwa mufano, mutume Paulo alijiona kuwa wa bure wakati alifikiria uzaifu wake. (Ro. 7:24) Kwa kweli, Paulo alikuwa ametubu zambi zake na kubatizwa. Lakini, aliendelea kujiona kuwa “mudogo zaidi kati ya mitume” na mutenda-zambi “wa kwanza kabisa.”—1 Ko. 15:9; 1 Ti. 1:15. w24.03 27 fu. 5-6
Siku ya Pili, 14 Mwezi wa 10
Wakaacha nyumba ya Yehova Mungu.—2 Ny. 24:18.
Jambo moya yenye uamuzi mubaya wa Mufalme Yehoashi unaweza kutufundisha ni kama tunapaswa kuchagua marafiki wenye watatuchochea kufanya mambo ya muzuri; marafiki wenye wanamupenda Yehova na wenye wanapenda kumufurahisha. Haiko lazima marafiki wetu wakuwe tu wa miaka yetu. Kumbuka kama Yehoashi alikuwa mudogo sana kuliko rafiki yake Yehoyada. Fikiria marafiki wenye uko nao kisha ujiulize hii maulizo: ‘Wananisaidia ili imani yangu kwa Yehova ikuwe nguvu zaidi? Wananitia moyo nitumikishe kanuni za Mungu mu maisha yangu? Wanazungumuzia kuhusu Yehova na kweli za Biblia? Wanaheshimia kanuni za Mungu? Wananiambia tu mambo yenye ninapenda kusikia ao wako tayari kunirekebisha kama ninafanya makosa?’ (Mez. 27:5, 6, 17) Kusema kweli, hauna lazima ya marafiki wenye hawamupendi Yehova. Lakini kama uko na marafiki wenye wanamupenda Yehova, ushikamane nao; watakusaidia sana!—Mez. 13:20. w23.09 9-10 fu. 6-7
Siku ya Tatu, 15 Mwezi wa 10
Mimi ndiye Alfa na Omega.—Ufu. 1:8.
Alfa njo herufi ya kwanza mu alfabeti ya Kigiriki na omega njo herufi ya mwisho. Kwa kutumia maneno “Alfa na Omega,” Yehova anaonyesha kama wakati anaanza jambo fulani anaendelea nayo mupaka ifikie mwisho kabisa. Kisha Yehova kuumba Adamu na Eva akawaambia: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.” (Mwa. 1:28) Ile wakati ni sawa vile Yehova alisema “Alfa.” Alionyesha waziwazi kusudi yake: Kutakuwa wakati wenye wazao wa Adamu na Eva wenye kuwa wakamilifu na watiifu watajaza dunia na kuifanya kuwa Paradiso. Wakati ile itatimia ni sawa vile atasema “Omega.” Kisha kumaliza kuumba “mbingu na dunia pamoja na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake,” Yehova alisema jambo fulani yenye ilihakikisha kama kusudi yake itatimia kabisa. Yehova alitoa uhakikisho kama bila shaka angetimiza kusudi yake kwa wanadamu na dunia. Ingetimia kabisa ku mwisho wa siku ya saba.—Mwa. 2:1-3. w23.11 5 fu. 13-14
Siku ya Ine, 16 Mwezi wa 10
Mufungue njia ya Yehova! Mufanye njia kubwa yenye kunyooka katika jangwa kwa ajili ya Mungu wetu.—Isa. 40:3.
Safari ya kutoka Babiloni kuenda Israeli haikukuwa mwepesi, na ingekamata karibu miezi ine. Lakini, Yehova aliahidi kama atatosha vizuizi vyote vyenye vingefanya Waisraeli wasirudie muzuri. Wayahudi waaminifu walijua kama ikiwa wanajikaza kabisa kurudia mu Israeli wangepata baraka mingi sana. Baraka kubwa sana yenye wangepata ni kurudisha ibada safi. Hamukukuwa hata hekalu moya ya Yehova mu Babiloni. Na hamukukuwa hata mazabahu kwenye Waisraeli wangetolea zabihu zenye Sheria ya Musa iliomba na hamukukuwa makuhani wenye walipaswa kutoa zile zabihu. Zaidi ya ile, mu ule muji, watu wenye walikuwa naabudu miungu ya uongo walikuwa wengi sana kuliko wale wenye walitii Yehova ao kanuni zake. Kwa hiyo, maelfu ya Wayahudi wenye walikuwa namuogopa Mungu walikuwa natazamia kwa hamu kurudia mu inchi yao ili warudishe ibada safi. w23.05 14-15 fu. 3-4
Siku ya Tano, 17 Mwezi wa 10
Muendelee kutembea kama watoto wa mwangaza.—Efe. 5:8.
Tuko na lazima ya roho takatifu ya Mungu ili tuendelea kujiendesha “kama watoto wa mwangaza.” Juu ya nini? Juu ni nguvu sana kuendelea kuwa safi mu huu ulimwengu wenye kujaa mwenendo muchafu. (1 Te. 4:3-5, 7, 8) Roho takatifu inaweza kutusaidia tupiganishe mawazo ya ulimwengu, ni kusema filozofia ya ulimwengu na mawazo yenye kupingana na mawazo ya Mungu. Roho takatifu inaweza pia kutusaidia tuonyeshe “kila namna ya wema, na haki.” (Efe. 5:9) Njia moya ya kupata roho takatifu ni kuomba Yehova atupatie ile roho. Yesu alisema kama Yehova anawapatia “roho yake takatifu wale wenye kumuomba.” (Lu. 11:13) Pia wakati tunamusifu Yehova pamoya ku mikutano, tunapata roho takatifu. (Efe. 5:19, 20) Utendaji wa roho takatifu mu maisha yetu utatusaidia kuishi mu njia yenye inamufurahisha Mungu. w24.03 23-24 fu. 13-15
Siku ya Posho, 18 Mwezi wa 10
Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata; muendelee kupiga hodi, na watawafungulia.—Lu. 11:9.
Uko na lazima ya kuwa na uvumilivu zaidi? Kama ni vile, muombe Yehova akusaidie. Uvumilivu ni sehemu ya tunda ya roho. (Gal. 5:22, 23) Tunapaswa kumuomba Yehova atupatie roho yake takatifu na kumuomba atusaidie tukomalishe tunda ya ile roho. Kama tunajikuta mu hali yenye inatuomba tuonyeshe uvumilivu, tunapaswa “kuendelea kumuomba” Yehova roho takatifu ili tuonyeshe uvumilivu. (Lu. 11:13) Tunapaswa pia kumuomba atusaidie tuone mambo vile yeye anaiona. Na kisha kusali, tunapaswa kufanya yetu yote juu tuendelee kuwa wavumilivu kila siku. Kama tunaendelea kumuomba Yehova atusaidie tukuwe na uvumilivu na kama tunaendelea kufanya yetu yote juu ya kuonyesha ile sifa, atatusaidia tukuwe na uvumilivu zaidi hata kama hatukukuwaka na ile sifa zamani. Kutafakari juu ya mifano yenye kuwa mu Biblia kunaweza pia kusaidia. Mu Biblia muko mifano mingi ya watu wenye walikuwa na uvumilivu. Kama tunatafakari juu ya ile mifano, tunaweza kujifunza njia mbalimbali za kuonyesha uvumilivu. w23.08 22 fu. 10-11
Siku ya Yenga, 19 Mwezi wa 10
Mushushe nyavu zenu, muvue samaki.—Lu. 5:4.
Yesu alimuhakikishia mutume Petro kama Yehova atamuhangaikia. Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa, alisaidia Petro na mitume wengine kukamata tena samaki kwa njia ya muujiza. (Yoh. 21:4-6) Bila shaka ule muujiza ulimuhakikishia Petro kama ni mwepesi kwa Yehova kumutolea vitu vya kimwili vyenye alikuwa navyo lazima. Pengine Petro alikumbuka namna Yesu alisemaka kama Yehova atatimiza mahitaji ya wale wenye “kutafuta kwanza Ufalme.” (Mt. 6:33) lle ilifanya Petro atie kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, hapana kazi ya kuvua samaki. Kisha pale alitoa ushahidi kwa uhodari siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., na akasaidia maelfu ya watu wakubali habari njema. (Mdo. 2:14, 37-41) Na kisha alisaidia Wasamaria na Watu wa Mataifa wakubali Kristo. (Mdo. 8:14-17; 10:44-48) Ni wazi kama Yehova alitumia Petro ili kuleta watu wa namna zote mu kutaniko. w23.09 20 fu. 1; 23 fu. 11
Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 10
Kama hamunijulishe ndoto hiyo, pamoja na maana yake, mutakatwa vipande-vipande.—Da. 2:5.
Miaka mbili hivi kisha Wababiloni kuharibu Yerusalemu. Nebukadneza, Mufalme wa Babiloni alilota ndoto yenye ilimuogopesha kuhusu sanamu kubwa sana. Alisema kama ataua wanaume wote wenye hekima, kutia ndani Danieli kama wanashindwa kumuambia ndoto yake na kama wanashindwa kuifasiria. (Da. 2:3-5) Danieli alipaswa kutenda haraka, juu kama hangefanya vile, watu wengi wangekufa. Njo maana “aliingia na kumuomba mufalme amupatie wakati ili amufasirie mufalme maana yake.” (Da. 2:16) Ile ilionyesha kama Danieli alikuwa na uhodari na imani. Juu ya nini tunasema vile? Juu mu Biblia hamuna andiko yenye inaonyesha kama Danieli alikuwaka nafasiria ndoto zamani. Aliomba marafiki wake “wasali ili wapate rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni juu ya siri hiyo.” (Da. 2:18) Yehova alijibia sala zao. Kwa musaada wa Mungu, Danieli alifasiria ndoto ya Nebukadneza. Kwa kufanya vile, aliokoa uzima wake na wa marafiki wake. w23.08 3 fu. 4
Siku ya Pili, 21 Mwezi wa 10
Ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.—Mt. 24:13.
Fikiria faida za kuwa na uvumilivu. Kama tuko na uvumilivu, tutakuwa na furaha zaidi na tutatulia zaidi. Kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuwa na afya ya muzuri kimwili na kiakili. Kama tunavumilia wengine, tutakuwa na uhusiano wa muzuri zaidi pamoya nao. Kutaniko yetu itakuwa na umoja zaidi. Kama hatukasirike haraka wakati mutu fulani anatuchokoza, ile itafanya hali isiharibike zaidi. (Zb. 37:8, maelezo ya chini; Mez. 14:29) Lakini, zaidi ya yote, tutamuiga Baba yetu wa mbinguni na tutamukaribia hata zaidi. Uvumilivu ni sifa ya muzuri kabisa yenye inatuleteaka siye wote faida! Kusema kweli, haiko mwepesi kila mara kuwa na uvumilivu, lakini kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuendelea kuonyesha ile sifa. Na vile tuko naendelea kungoya kwa uvumilivu dunia mupya, tuko hakika kama “jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa, wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 33:18) Tuazimie basi kuendelea kuvaa uvumilivu. w23.08 22 fu. 7; 25 fu. 16-17
Siku ya Tatu, 22 Mwezi wa 10
Imani yenyewe bila matendo imekufa.—Yak. 2:17.
Yakobo alionyesha kama mutu anaweza kusema kama iko na imani; lakini, je, matendo yake inaonyesha imani kabisa? (Yak. 2:1-5, 9) Yakobo anazungumuzia pia mutu mwenye anaona ‘ndugu ao dada anakosa nguo ao chakula’ lakini hamutolee musaada wenye iko nao lazima. Hata kama ule mutu anasema kama iko na imani, ile imani haionekane kupitia matendo; kwa hiyo, ile imani ni ya bure. (Yak. 2:14-16) Yakobo alizungumuzia Rahabu kuwa mufano muzuri wa kuonyesha imani kupitia matendo. (Yak. 2:25, 26) Rahabu alisikia habari kuhusu Yehova na akaamini kama ni Yehova njo alikuwa anategemeza Waisraeli. (Yos. 2:9-11) Alionyesha imani yake kupitia matendo. Alilinda wapelelezi wawili Waisraeli wakati uzima wao ulikuwa mu hatari. Ile ilikuwa na matokeo gani? Ule mwanamuke, mwenye hakamilike na mwenye hakukuwa Muisraeli, alionwa kuwa mwenye haki sawa vile tu Abrahamu. Mufano wake unaonyesha ulazima wa kuwa na imani yenye inaonekana kupitia matendo. w23.12 5-6 fu. 12-13
Siku ya Ine, 23 Mwezi wa 10
“Mukuwe na mizizi na kufanywa imara juu ya ule musingi.”—Efe. 3: 17.
Siye Wakristo hatutosheke tu na mafundisho ya musingi ya Biblia. Kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu tunapenda sana kujifunza “hata mambo mazito ya Mungu.” (1 Ko. 2:9, 10) Juu ya nini usijiwekee programu ya kujifunza habari zenye zitakusaidia umukaribie Yehova zaidi? Kwa mufano, unaweza kuchunguza namna alionyesha upendo watumishi wake wa zamani na namna ile inaonyesha kama anakupenda na weye. Unaweza kuchunguza mipango yenye Yehova aliweka kwa ajili ya ibada mu Israeli na kuona namna inalingana na vile Yehova anapenda Wakristo wamuabudu leo. Ao pengine unaweza kujifunza kwa undani maunabii yenye Yesu alitimiza mu maisha na utumishi wake hapa ku dunia. Tutafurahi sana kama tunajifunza zile habari kwa kutumia Index ao Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Kujifunza Biblia kwa undani kunaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako, na kukusaidia “upate ujuzi juu ya Mungu.”—Mez. 2:4, 5. w23.10 18-19 fu. 3-5
Siku ya Tano, 24 Mwezi wa 10
Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.—1 Pe. 4:8.
Neno yenye mutume Neno “mwingi” yenye Petro alitumia inamaanisha neno kwa neno “kupanuka.” Sehemu ya pili ya ile andiko inaonyesha matokeo ya upendo mwingi: unafunika zambi za ndugu zetu. Ni sawa vile upendo ulikuwa nguo yenye inaweza kupanuka yenye tunakamata na mikono mbili na tunaanza kuikokota na inapanuka mupaka inafunika hapana zambi moya ao mbili, lakini “zambi nyingi.” ‘Kufunika’ ni namna ingine ya kusema kusamehe. Sawa tu vile nguo inaweza kufunika kasoro, upendo unaweza kufunika uzaifu na makosa ya wengine. Upendo wetu unapaswa kuwa nguvu sana juu tuweze kusamehe makosa ya waamini wenzetu, hata kama wakati fulani ile inaomba kujikaza sana. (Kol. 3:13) Wakati tunasamehe wengine tunaonyesha kama upendo wetu uko nguvu na kama tunapenda kumufurahisha Yehova. w23.11 11-12 fu. 13-15
Siku ya Posho, 25 Mwezi wa 10
Shafani akaanza kukisoma mbele ya mufalme.—2 Ny. 34:18.
Wakati Mufalme Yosia alikuwa na miaka 26 alianza kutengeneza hekalu. Wakati ile kazi ilikuwa inafanywa, “kitabu cha Sheria ya Yehova yenye ilipewa kupitia Musa” kilipatikana. Kisha kusikia maneno yenye ilikuwa imeandikwa mu ile kitabu, mufalme alichochewa kutenda kupatana na ile maneno. (2 Ny. 34:14, 19-21) Na weye ungependa kuwa nasoma Biblia kila siku? Kama uko najikaza kufanya vile, usomaji wako uko naendelea muzuri? Unaandikaka maandiko yenye inaweza kukusaidia? Wakati Yosia alikuwa na miaka karibu 39 alifanya kosa yenye ilifanya apoteze uzima wake. Alijitumainia kuliko kutafuta muongozo wa Yehova. (2 Ny. 35:20-25) Tunajifunza nini? Ikuwe tuko na miaka ngapi, ao tumejifunza Biblia kwa muda gani, tunapaswa kuendelea kumutafuta Yehova, ni kusema, tunapaswa kusali kwa ukawaida, kutafuta muongozo wake, kujifunza Neno yake, na kutafuta mashauri ya Wakristo wenye kukomaa kiroho. Kama tunafanya vile, inawezekana tusifanye makosa makubwa-makubwa na tukuwe na furaha zaidi.—Yak. 1:25. w23.09 12 fu. 15-16
Siku ya Yenga, 26 Mwezi wa 10
Mungu anapinga wenye majivuno, lakini anapatia wanyenyekevu fazili zenye hazistahiliwe.—Yak. 4:6.
Biblia inazungumuzia mifano mingi ya wanamuke wa pekee wenye walimupenda na kumutumikia Yehova. Kama vile andiko yetu ya musingi inaonyesha, walikuwa “na kiasi katika tabia zao, na waaminifu katika mambo yote.”(1 Ti. 3:11) Zaidi ya ile, dada vijana wanaweza kupata mu kutaniko yao dada Wakristo wenye kukomaa kiroho wenye kuwa mifano mizuri ya kuiga. Dada vijana, hamuone kama itakua muzuri mutafute mu kutaniko yenu dada fulani wenye kukomaa kiroho wenye munaweza kuiga? Mutambue sifa zao za muzuri, kisha muone namna munaweza pia kuzionyesha. Moya kati ya sifa za maana ili kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho ni unyenyekevu. Kama dada iko munyenyekevu, atakuwa na uhusiano muzuri pamoya na Yehova na pamoya na wengine. Kwa mufano, mwanamuke mwenye anamupenda Yehova anategemeza kwa unyenyekevu mupango wa ukichwa wenye Baba yake wa mbinguni aliweka. (1 Ko. 11:3) Kuko mambo yenye anaweza kufanya juu ya kuonyesha kama anategemeza ule mupango wa ukichwa mu kutaniko, na mambo ingine yenye anaweza kufanya juu ya kuonyesha kama anategemeza ule mupango mu familia. w23.12 18-19 fu. 3-5
Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 10
Bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe.—Efe. 5:28.
Yehova anatazamia kwamba bwana amupende bibi yake na ahangaikie mahitaji yake ya kiroho, ya kimwili, na akuwe rafiki muzuri kwake. Kuwa na uwezo wa kufikiri, kuheshimia wanamuke, na kuwa mwenye kutegemeka, zitakusaidia kuwa bwana muzuri. Kisha kuoa, munaweza kuwa na watoto. Mufano wa Yehova unaweza kukufundisha nini kuhusu kuwa baba muzuri? (Efe. 6:4) Yehova aliambia waziwazi Yesu, mwana wake, kama anamupenda na anamukubali. (Mt. 3:17) Kama unakuwa baba, uhakikishie watoto wako kwa ukawaida kama unawapenda. Ukuwe na zoea ya kuwapongeza juu ya mambo ya muzuri yenye wanafanya. Baba wenye wanamuiga Yehova wanasaidia watoto wao wakuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho. Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya ile daraka kwa kupenda na kuhangaikia watu wa familia yako na wa mu kutaniko, na kwa kujifunza kuwaonyesha kama unawapenda na kama unawaona kuwa wa maana.—Yoh. 15:9. w23.12 28-29 fu. 17-18
Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 10
[Yehova] ndiye anafanya nyakati zako kuwa imara.—Isa. 33:6.
Siye watumishi waaminifu wa Yehova tunapambana na magumu yenye watu wote wanapataka. Tunaweza pia kupambana na upinzani ao mateso kutoka kwa wale wenye wanachukia watu wa Mungu. Hata kama Yehova hazuie ile magumu isitupate, anatuahidi kama atatusaidia. (Isa. 41:10) Kwa musaada wake tunaweza kuendelea kuwa na furaha, kukamata maamuzi ya muzuri, na kuendelea kuwa washikamanifu, hata mu hali za nguvu sana. Yehova anaahidi kutupatia jambo yenye Biblia inaita “amani ya Mungu.” (Flp. 4:6, 7) Ile amani ni utulivu wa akili na wa moyo wenye mutu anakuwaka nao kwa sababu ya uhusiano muzuri wenye iko nao pamoja naye. Ile amani “inapita uelewaji wote”; inapita jambo yoyote yenye tunaweza kuwazia. Ulishakasikia utulivu wa ajabu kisha kusali kwa Yehova? Ile yenye ulisikiaka njo “amani ya Mungu.” w24.01 20 fu. 2; 21 fu. 4
Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 10
Acha nimusifu Yehova; Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.—Zb. 103:1.
Watu waaminifu wanamupenda Mungu, na ile inawachochea wasifu jina yake kwa moyo wote. Mufalme Daudi alielewa kama kusifu jina ya Mungu ni kumusifu Mungu mwenyewe. Jina ya Mungu, Yehova, inamaanisha mambo mingi, inatukumbusha sifa zake za muzuri, na matendo yake ya ajabu. Daudi aliona jina ya Baba yake kuwa takatifu na aliisifu. Alipenda kufanya vile kwa “kila kitu chenye kuwa ndani” yake, ni kusema, kwa moyo wote. Kuhusu kumusifu Yehova, Walawi njo walikuwa ku mustari wa mbele. Kwa unyenyekevu, walikubali kama maneno yao haingeweza kusifu jina ya Yehova kwa ukamili vile inastahili. (Ne. 9:5) Bila shaka, ile sifa yenye kutoka ku moyo na yenye kufanywa kwa unyenyekevu, ilifurahisha moyo wa Yehova. w24.02 9 fu. 6
Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 10
Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.—Flp. 3:16.
Kama haufikie muradi wenye haupatane na uwezo wako, usiwaze kama Yehova ataona kuwa unashindwa. (2 Ko. 8:12) Ujifunze mambo fulani kupitia kizuizi yenye unakutana nayo.Usisahau miradi yenye ulishakafikia. Biblia inasema kama “Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu.” (Ebr. 6:10) Na weye usisahau miradi yenye ulishakafikia, sawa vile kukomalisha urafiki wako pamoya na Yehova, kuambia wengine juu yake, ao kubatizwa. Sawa vile tu ulijikazaka kufikia miradi yako ya kiroho zamani, unaweza pia kujikaza kufikia miradi yako ya sasa.Kwa musaada wa Yehova, unaweza kuwa na furaha ya kufikia muradi wako Kila mara ujikaze kuona namna Yehova iko nakusaidia, na ile itafanya ukuwe na furaha wakati uko najikaza kufikia miradi yako. (2 Ko. 4:7) Kama hauvunjike moyo, utapata baraka mingi hata zaidi.—Gal. 6:9. w23.05 31 fu. 16-18
Siku ya Tano, 31 Mwezi wa 10
Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mumenipenda na mumeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.—Yoh. 16:27.
Yehova anapenda kuonyesha kama anakubali wale wenye anapenda. Maandiko inazungumuzia mara mbili zenye Yehova aliambia Yesu kama alikuwa Mwana wake mupendwa mwenye alikubali. (Mt. 3:17; 17:5) Unapenda kumusikia Yehova anasema kama anakukubali? Hatuwezi kusikia sauti ya Yehova, lakini anazungumuza na siye kupitia Neno yake. Tunaweza “kumusikia” Yehova anasema kuwa anatukubali wakati tunasoma maneno ya Yesu yenye kuwa mu Injili. Yesu alionyesha kwa ukamili utu wa Baba yake. Wakati tunasoma namna Yesu aliambia wafuasi wake waaminifu kama anawakubali hata kama hawakukuwa wakamilifu, tunaweza kuwazia kama ni Yehova njo iko natuambia ile maneno. (Yoh. 15:9, 15) Kama tunapata magumu, ile magumu haimaanishe kama Yehova hatukubali tena. Lakini inatupatia nafasi ya kuonyesha ni kwa kadiri gani tunamupenda na kumutumainia.—Yak. 1:12. w24.03 28 fu. 10-11