Siku ya Tatu, 15 Mwezi wa 10
Mimi ndiye Alfa na Omega.—Ufu. 1:8.
Alfa njo herufi ya kwanza mu alfabeti ya Kigiriki na omega njo herufi ya mwisho. Kwa kutumia maneno “Alfa na Omega,” Yehova anaonyesha kama wakati anaanza jambo fulani anaendelea nayo mupaka ifikie mwisho kabisa. Kisha Yehova kuumba Adamu na Eva akawaambia: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.” (Mwa. 1:28) Ile wakati ni sawa vile Yehova alisema “Alfa.” Alionyesha waziwazi kusudi yake: Kutakuwa wakati wenye wazao wa Adamu na Eva wenye kuwa wakamilifu na watiifu watajaza dunia na kuifanya kuwa Paradiso. Wakati ile itatimia ni sawa vile atasema “Omega.” Kisha kumaliza kuumba “mbingu na dunia pamoja na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake,” Yehova alisema jambo fulani yenye ilihakikisha kama kusudi yake itatimia kabisa. Yehova alitoa uhakikisho kama bila shaka angetimiza kusudi yake kwa wanadamu na dunia. Ingetimia kabisa ku mwisho wa siku ya saba.—Mwa. 2:1-3. w23.11 5 fu. 13-14
Siku ya Ine, 16 Mwezi wa 10
Mufungue njia ya Yehova! Mufanye njia kubwa yenye kunyooka katika jangwa kwa ajili ya Mungu wetu.—Isa. 40:3.
Safari ya kutoka Babiloni kuenda Israeli haikukuwa mwepesi, na ingekamata karibu miezi ine. Lakini, Yehova aliahidi kama atatosha vizuizi vyote vyenye vingefanya Waisraeli wasirudie muzuri. Wayahudi waaminifu walijua kama ikiwa wanajikaza kabisa kurudia mu Israeli wangepata baraka mingi sana. Baraka kubwa sana yenye wangepata ni kurudisha ibada safi. Hamukukuwa hata hekalu moya ya Yehova mu Babiloni. Na hamukukuwa hata mazabahu kwenye Waisraeli wangetolea zabihu zenye Sheria ya Musa iliomba na hamukukuwa makuhani wenye walipaswa kutoa zile zabihu. Zaidi ya ile, mu ule muji, watu wenye walikuwa naabudu miungu ya uongo walikuwa wengi sana kuliko wale wenye walitii Yehova ao kanuni zake. Kwa hiyo, maelfu ya Wayahudi wenye walikuwa namuogopa Mungu walikuwa natazamia kwa hamu kurudia mu inchi yao ili warudishe ibada safi. w23.05 14-15 fu. 3-4
Siku ya Tano, 17 Mwezi wa 10
Muendelee kutembea kama watoto wa mwangaza.—Efe. 5:8.
Tuko na lazima ya roho takatifu ya Mungu ili tuendelea kujiendesha “kama watoto wa mwangaza.” Juu ya nini? Juu ni nguvu sana kuendelea kuwa safi mu huu ulimwengu wenye kujaa mwenendo muchafu. (1 Te. 4:3-5, 7, 8) Roho takatifu inaweza kutusaidia tupiganishe mawazo ya ulimwengu, ni kusema filozofia ya ulimwengu na mawazo yenye kupingana na mawazo ya Mungu. Roho takatifu inaweza pia kutusaidia tuonyeshe “kila namna ya wema, na haki.” (Efe. 5:9) Njia moya ya kupata roho takatifu ni kuomba Yehova atupatie ile roho. Yesu alisema kama Yehova anawapatia “roho yake takatifu wale wenye kumuomba.” (Lu. 11:13) Pia wakati tunamusifu Yehova pamoya ku mikutano, tunapata roho takatifu. (Efe. 5:19, 20) Utendaji wa roho takatifu mu maisha yetu utatusaidia kuishi mu njia yenye inamufurahisha Mungu. w24.03 23-24 fu. 13-15