Siku ya Pili, 9 Mwezi wa 9
Mwanamuke mujinga ni mwenye fujo. Yeye ni mujinga.—Mez. 9:13.
Wale wenye wanasikia mualiko wa “mwanamuke mujinga” wanapaswa kuamua ikiwa wataukubali ao hapana. Kuko sababu mingi za muzuri zenye zinapaswa kutuchochea kuepuka uasherati. “Mwanamuke mujinga” iko nasema hivi: “Maji yenye yaliibwa ni matamu.” (Mez. 9:17) Ile “maji yenye yaliibwa” njo nini? Biblia inafananisha ngono kati ya bibi na bwana na maji yenye kuburudisha. (Mez. 5:15-18) Mwanaume na mwanamuke wenye kuoana kulingana na sheria wanaruhusiwa kufanya ngono. Lakini, ile iko tofauti kabisa na “maji yenye yaliibwa.” Ile maji inaweza kumaanisha uasherati. Kwa kawaida, watu wenye wanafanyaka uasherati wanajifichikaka juu wengine wasiwaone, sawa vile tu mwizi mwenye iko naiba. Zaidi ya ile, “maji yenye yaliibwa” inaweza kuonekana kuwa butamu kama wale wenye kuikunywa wanawaza kama hakuna mutu mwenye atajua mambo yenye walifanya. Ile ni kujidanganya kabisa juu Yehova anaonaka mambo yote. Hakuna jambo ya kuhuzunisha zaidi sawa vile kupoteza kibali ya Yehova. Kwa hiyo, haiko jambo ya “butamu” ao ya kufurahisha.—1 Ko. 6:9, 10. w23.06 22 fu. 7-9
Siku ya Tatu, 10 Mwezi wa 9
Hata kama ninafanya vile bila kupenda, bado nimepewa usimamizi-nyumba.—1 Ko. 9:17.
Utafanya nini ikiwa unaona kama sala zako hazitoke tena ku moyo ao haufurahie tena mahubiri sawa zamani? Usiwaze kama umepoteza roho ya Yehova. Juu haukamilike, hisia zako zinaweza kubadilika-badilika. Kama bidii yako inaanza kupunguka, fikiria mufano wa mutume Paulo. Hata kama alijikaza kumuiga Yesu, alijua kama wakati fulani hatajisikia kuwa mwenye bidii. Paulo aliazimia kutimiza utumishi wake hata ajisikie namna gani. Vilevile, usiache hisia zikamate uamuzi pa nafasi yako. Azimia kufanya mambo ya muzuri hata kama unajisikia namna gani. Kama unaendelea kufanya mambo ya muzuri, kisha wakati fulani hisia zako zinaweza kubadilika.—1 Ko. 9:16. w24.03 11-12 fu. 12-13
Siku ya Ine, 11 Mwezi wa 9
Muwahakikishie upendo wenu.—2 Ko. 8:24.
Tunaweza kuonyesha upendo ndugu na dada zetu kwa kufanya urafiki pamoja nao. (2 Ko. 6:11-13) Wengi kati yetu wako mu makutaniko mwenye muko ndugu na dada wa desturi na hali tofauti ya maisha na wenye kuwa na utu mbalimbali. Tunaweza kuwapenda zaidi kwa kukazia uangalifu sifa zao za muzuri. Wakati tunajifunza kuona wengine kama vile Yehova anawaona, tunaonyesha kama tunawapenda. Upendo utakuwa wa maana sana wakati wa taabu kubwa. Wakati ile taabu kubwa itaanza, wapi njo tutapata ulinzi? Fikiria mambo yenye Yehova aliomba watu wake wafanye wakati Babiloni ya zamani ilishambuliwa. Aliwaambia hivi: “Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani, na mufunge milango nyuma yenu. Mujifiche kwa wakati mufupi mupaka kasirani kali ipite.” (Isa. 26:20) Inaonekana ile maneno inatuhusu siye pia wenye tutapambana na taabu kubwa. w23.07 6-7 fu. 14-16