Siku ya Tatu, 10 Mwezi wa 9
Hata kama ninafanya vile bila kupenda, bado nimepewa usimamizi-nyumba.—1 Ko. 9:17.
Utafanya nini ikiwa unaona kama sala zako hazitoke tena ku moyo ao haufurahie tena mahubiri sawa zamani? Usiwaze kama umepoteza roho ya Yehova. Juu haukamilike, hisia zako zinaweza kubadilika-badilika. Kama bidii yako inaanza kupunguka, fikiria mufano wa mutume Paulo. Hata kama alijikaza kumuiga Yesu, alijua kama wakati fulani hatajisikia kuwa mwenye bidii. Paulo aliazimia kutimiza utumishi wake hata ajisikie namna gani. Vilevile, usiache hisia zikamate uamuzi pa nafasi yako. Azimia kufanya mambo ya muzuri hata kama unajisikia namna gani. Kama unaendelea kufanya mambo ya muzuri, kisha wakati fulani hisia zako zinaweza kubadilika.—1 Ko. 9:16. w24.03 11-12 fu. 12-13
Siku ya Ine, 11 Mwezi wa 9
Muwahakikishie upendo wenu.—2 Ko. 8:24.
Tunaweza kuonyesha upendo ndugu na dada zetu kwa kufanya urafiki pamoja nao. (2 Ko. 6:11-13) Wengi kati yetu wako mu makutaniko mwenye muko ndugu na dada wa desturi na hali tofauti ya maisha na wenye kuwa na utu mbalimbali. Tunaweza kuwapenda zaidi kwa kukazia uangalifu sifa zao za muzuri. Wakati tunajifunza kuona wengine kama vile Yehova anawaona, tunaonyesha kama tunawapenda. Upendo utakuwa wa maana sana wakati wa taabu kubwa. Wakati ile taabu kubwa itaanza, wapi njo tutapata ulinzi? Fikiria mambo yenye Yehova aliomba watu wake wafanye wakati Babiloni ya zamani ilishambuliwa. Aliwaambia hivi: “Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani, na mufunge milango nyuma yenu. Mujifiche kwa wakati mufupi mupaka kasirani kali ipite.” (Isa. 26:20) Inaonekana ile maneno inatuhusu siye pia wenye tutapambana na taabu kubwa. w23.07 6-7 fu. 14-16
Siku ya Tano, 12 Mwezi wa 9
Tamasha ya ulimwengu huu inabadilika.—1 Ko. 7:31.
Ujiendeshe mu njia yenye itafanya wengine waone kama uko mutu mwenye usawaziko. Ujiulize hivi: ‘Watu wananionaka kuwa mutu mwenye usawaziko, mwenye kujipatanisha na hali, na mwenye kuachilia mambo kwa kupenda? Ao wananionaka kuwa mutu mugumu, mukali, ao wa kichwa nguvu? Ao nasikilizaka wengine na kufuata mawazo yao kama ni lazima?’ Kama tunaendelea kuwa na usawaziko, tutaonyesha kama tuko namuiga Yehova na Yesu. Tunapaswa kuwa na usawaziko wakati hali inabadilika mu maisha yetu. Ile mabadiliko inaweza kufanya tupate magumu yenye hatuyawaziaka hata kidogo. Kwa mufano tunaweza kugonjwa sana bila kutazamia, ao mabadiliko ya kiuchumi ao ya serikali yenye haitazamiwe fasi kwenye tunaishi, inaweza kufanya maisha yetu ikuwe nguvu sana. (Muh. 9:11) Inaweza pia kuwa nguvu kwetu wakati tengenezo inabadilisha mugao wetu wa utumishi. Hata hali ibadilike namna gani, unaweza kujipatanisha nayo kwa kufanya hii mambo ine: (1) Ukubali mabadiliko, (2) ufikirie mambo ya sasa hapana ya zamani, (3) ujikaze kuona mambo ya muzuri mu maisha yako na (4) usaidie wengine. w23.07 21-22 fu. 7-8