Siku ya Yenga, 14 Mwezi wa 9
Elewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini.—Efe. 3:18.
Wakati unataka kuamua ikiwa utauza nyumba fulani ao hapana. Itakuwa lazima uchunguze kila sehemu ya nyumba yenye unapenda kuuza. Hapana kupitia video lakini kwa kufika mahali kwenye kuko ile nyumba. Tunaweza pia kufanya vile wakati tuko nasoma na kujifunza Biblia. Kama unaisoma mbiombio pengine utajifunza tu kweli za musingi, ni kusema “mambo ya musingi ya maneno matakatifu ya Mungu.” (Ebr. 5:12) Kuliko kufanya vile, sawa vile mutu anaweza kufanya kuhusu nyumba, ingia “ndani” ili uchunguze mambo yote ya maana. Njia ya muzuri ya kujifunza Biblia ni kuona namna sehemu zake mbalimbali zinapatana. Usitafute tu kujua ni kweli gani unaamini, lakini pia juu ya nini unaziamini. Ili kuelewa Neno ya Mungu kwa undani kabisa, unapaswa kujifunza mafundisho mazito ya Biblia. Mutume Paulo alitia moyo ndugu na dada zake wajifunze Neno ya Mungu kwa uangalifu ili waweze “kuelewa kwa ukamili upana na urefu na urefu kuenda juu na urefu kuenda chini” wa kweli. Na ile ingefanya wafikie kuwa “na mizizi na kufanywa imara” katika imani yao. (Efe. 3:14-19) Siye pia tunapaswa kufanya vile. w23.10 18 fu. 1-3
Siku ya Kwanza, 15 Mwezi wa 9
Ndugu, kuhusu kuvumulia uovu na kuwa wavumilivu, mufuate mufano wa wale manabii wenye walisema katika jina la Yehova.—Yak. 5:10.
Biblia iko na mifano mingi ya watu wenye walikuwaka na uvumilivu. Hauone kama ni jambo ya muzuri kama unajiwekea muradi wa kujifunza ile mifano? Kwa mufano, hata kama Daudi alitiwa mafuta wakati alikuwa angali kijana sana ili akuwe mufalme wa Israeli, alipaswa kungoya miaka mingi mbele akuwe mufalme. Simeoni na Ana walimuabudu Yehova kwa uaminifu wakati walikuwa nangoya Masiya mwenye aliahidiwa. (Lu. 2:25, 36-38) Wakati utakuwa najifunza ile mifano, tafuta majibu ya hii maulizo: Pengine ni nini ilisaidia huyu mutu aonyeshe uvumilivu? Alipata faida gani juu alikuwa na uvumilivu? Namna gani naweza kumuiga? Unaweza pia kupata faida kwa kujifunza kuhusu wale wenye hawakuonyesha uvumilivu. (1 Sa. 13:8-14) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Nini njo ilifanya wale watu washindwe kuonyesha uvumilivu? Ni matokeo gani ya mubaya yenye walipata juu hawakukuwa na uvumilivu?’ w23.08 25 fu. 15
Siku ya Pili, 16 Mwezi wa 9
Tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mutakatifu wa Mungu.—Yoh. 6:69.
Mutume Petro alikuwa mushikamanifu; hakuacha kitu yoyote imufanye aache kabisa kumufuata Yesu. Kwa mufano, alionyesha ushikamanifu wake wakati Yesu alisema jambo fulani yenye wanafunzi wake hawakuelewa. (Yoh. 6:68) Kuliko kungoya ao kumuomba Yesu awafasirie, wengi waliacha kumufuata. Lakini Petro hakufanya vile, alijua kama Yesu tu njo alikuwa na “maneno ya uzima wa milele.” Yesu alijua kama Petro na mitume wengine wangemuacha. Hata vile, Yesu alionyesha kama alikuwa hakika kama Petro angemurudilia na kuendelea kuwa muaminifu. (Lu. 22:31, 32) Yesu alielewa kama “roho inataka, lakini mwili ni muzaifu.” (Mk. 14:38) Njo maana hata kisha Petro kumukana, Yesu hakuacha ule mutume wake. Kisha Yesu kufufuliwa. alimutokea Petro. Ni wazi kama alifanya vile wakati Petro alikuwa peke yake. (Mk. 16:7; Lu. 24:34; 1 Ko. 15:5) Bila shaka ile ilimutia moyo sana Petro! w23.09 22 fu. 9-10