Siku ya Pili, 16 Mwezi wa 9
Tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mutakatifu wa Mungu.—Yoh. 6:69.
Mutume Petro alikuwa mushikamanifu; hakuacha kitu yoyote imufanye aache kabisa kumufuata Yesu. Kwa mufano, alionyesha ushikamanifu wake wakati Yesu alisema jambo fulani yenye wanafunzi wake hawakuelewa. (Yoh. 6:68) Kuliko kungoya ao kumuomba Yesu awafasirie, wengi waliacha kumufuata. Lakini Petro hakufanya vile, alijua kama Yesu tu njo alikuwa na “maneno ya uzima wa milele.” Yesu alijua kama Petro na mitume wengine wangemuacha. Hata vile, Yesu alionyesha kama alikuwa hakika kama Petro angemurudilia na kuendelea kuwa muaminifu. (Lu. 22:31, 32) Yesu alielewa kama “roho inataka, lakini mwili ni muzaifu.” (Mk. 14:38) Njo maana hata kisha Petro kumukana, Yesu hakuacha ule mutume wake. Kisha Yesu kufufuliwa. alimutokea Petro. Ni wazi kama alifanya vile wakati Petro alikuwa peke yake. (Mk. 16:7; Lu. 24:34; 1 Ko. 15:5) Bila shaka ile ilimutia moyo sana Petro! w23.09 22 fu. 9-10
Siku ya Tatu, 17 Mwezi wa 9
Wenye furaha ni wale wenye matendo yao ya kuvunja sheria yamesamehewa na wenye zambi zao zimefunikwa.—Ro. 4:7.
Mungu anasamehe ao anafunika zambi za wale wenye kuwa na imani kwake. Anawasamehe kabisa-kabisa na haendelee kuhesabia zambi zao. (Zb. 32:1, 2) Kwa musingi ya imani yao, anawaona kuwa wenye hawana kosa na wenye haki. Hata kama Abrahamu, Daudi, na watumishi wengine waaminifu wa Mungu walionwa kuwa wenye haki, walikuwa wangali watu wenye hawakamilike na wenye wanaweza kufanya zambi. Lakini kwa sababu ya imani yao, Mungu aliwaona kuwa wenye hawana kosa, zaidi sana wakati alikuwa anawalinganisha na watu wengine wenye hawakumutumikia. (Efe. 2:12) Sawa vile mutume Paulo alionyesha mu barua yake, imani ni ya maana sana juu mutu akuwe rafiki ya Mungu. Abrahamu na Daudi walikuwa marafiki wa Mungu juu walikuwa na imani kwake. Siye pia tunaweza kuwa marafiki wa Mungu kama tuko na imani. w23.12 3 fu. 6-7
Siku ya Ine, 18 Mwezi wa 9
Sikuzote tumutolee Mungu zabihu ya sifa, ni kusema, tunda la midomo yetu yenye inatangaza jina lake mbele ya watu wote.—Ebr. 13:15.
Leo, Wakristo wote wako na pendeleo ya kumutolea Yehova zabihu kwa kutumia wakati wao, nguvu yao, na vitu vyenye wako navyo ili kusaidia kazi ya Ufalme iendelee mbele. Tunaweza kuonyesha kama tunafurahia pendeleo yenye tuko nayo ya kumuabudu Yehova kwa kumutolea zabihu kwa uwezo wetu wote. Mutume Paulo alizungumuzia sehemu mbalimbali za ibada yetu zenye hatupaswe kupuuza. (Ebr. 10:22-25) Ile inatia ndani kumukaribia Yehova katika sala, kufanya tangazo ya mbele ya watu wote ya tumaini yetu, kukusanyika pamoya mu kutaniko, na kutiana moyo “na kufanya vile zaidi sana kwa kadiri tunaona siku ya Yehova kuwa inakaribia.” Ku mwisho wa kitabu ya Ufunuo, malaika wa Yehova anasema hivi mara mbili: “Abudu Mungu!” (Ufu. 19:10; 22:9) Tusisahau hata siku moya hii mafundisho mazito kuhusu hekalu kubwa ya kiroho ya Yehova, na pendeleo ya muzuri sana yenye tuko nayo ya kumuabubu Mungu wetu mukubwa! w23.10 29 fu. 17-18