Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Kwanza, 15 Mwezi wa 9

Ndugu, kuhusu kuvumulia uovu na kuwa wavumilivu, mufuate mufano wa wale manabii wenye walisema katika jina la Yehova.​—Yak. 5:10.

Biblia iko na mifano mingi ya watu wenye walikuwaka na uvumilivu. Hauone kama ni jambo ya muzuri kama unajiwekea muradi wa kujifunza ile mifano? Kwa mufano, hata kama Daudi alitiwa mafuta wakati alikuwa angali kijana sana ili akuwe mufalme wa Israeli, alipaswa kungoya miaka mingi mbele akuwe mufalme. Simeoni na Ana walimuabudu Yehova kwa uaminifu wakati walikuwa nangoya Masiya mwenye aliahidiwa. (Lu. 2:25, 36-38) Wakati utakuwa najifunza ile mifano, tafuta majibu ya hii maulizo: Pengine ni nini ilisaidia huyu mutu aonyeshe uvumilivu? Alipata faida gani juu alikuwa na uvumilivu? Namna gani naweza kumuiga? Unaweza pia kupata faida kwa kujifunza kuhusu wale wenye hawakuonyesha uvumilivu. (1 Sa. 13:8-14) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Nini njo ilifanya wale watu washindwe kuonyesha uvumilivu? Ni matokeo gani ya mubaya yenye walipata juu hawakukuwa na uvumilivu?’ w23.08 25 fu. 15

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Pili, 16 Mwezi wa 9

Tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mutakatifu wa Mungu.​—Yoh. 6:69.

Mutume Petro alikuwa mushikamanifu; hakuacha kitu yoyote imufanye aache kabisa kumufuata Yesu. Kwa mufano, alionyesha ushikamanifu wake wakati Yesu alisema jambo fulani yenye wanafunzi wake hawakuelewa. (Yoh. 6:68) Kuliko kungoya ao kumuomba Yesu awafasirie, wengi waliacha kumufuata. Lakini Petro hakufanya vile, alijua kama Yesu tu njo alikuwa na “maneno ya uzima wa milele.” Yesu alijua kama Petro na mitume wengine wangemuacha. Hata vile, Yesu alionyesha kama alikuwa hakika kama Petro angemurudilia na kuendelea kuwa muaminifu. (Lu. 22:31, 32) Yesu alielewa kama “roho inataka, lakini mwili ni muzaifu.” (Mk. 14:38) Njo maana hata kisha Petro kumukana, Yesu hakuacha ule mutume wake. Kisha Yesu kufufuliwa. alimutokea Petro. Ni wazi kama alifanya vile wakati Petro alikuwa peke yake. (Mk. 16:7; Lu. 24:34; 1 Ko. 15:5) Bila shaka ile ilimutia moyo sana Petro! w23.09 22 fu. 9-10

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Tatu, 17 Mwezi wa 9

Wenye furaha ni wale wenye matendo yao ya kuvunja sheria yamesamehewa na wenye zambi zao zimefunikwa.​—Ro. 4:7.

Mungu anasamehe ao anafunika zambi za wale wenye kuwa na imani kwake. Anawasamehe kabisa-kabisa na haendelee kuhesabia zambi zao. (Zb. 32:1, 2) Kwa musingi ya imani yao, anawaona kuwa wenye hawana kosa na wenye haki. Hata kama Abrahamu, Daudi, na watumishi wengine waaminifu wa Mungu walionwa kuwa wenye haki, walikuwa wangali watu wenye hawakamilike na wenye wanaweza kufanya zambi. Lakini kwa sababu ya imani yao, Mungu aliwaona kuwa wenye hawana kosa, zaidi sana wakati alikuwa anawalinganisha na watu wengine wenye hawakumutumikia. (Efe. 2:12) Sawa vile mutume Paulo alionyesha mu barua yake, imani ni ya maana sana juu mutu akuwe rafiki ya Mungu. Abrahamu na Daudi walikuwa marafiki wa Mungu juu walikuwa na imani kwake. Siye pia tunaweza kuwa marafiki wa Mungu kama tuko na imani. w23.12 3 fu. 6-7

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine