Waamuzi
18 Katika siku hizo hapakukuwa mufalme katika Israeli.+ Na katika siku hizo watu wa kabila la Dani+ walikuwa wanatafuta mahali pa kukaa, kwa sababu kufikia wakati huo hawakukuwa wamepata uriti kati ya makabila ya Israeli.+
2 Watu wa kabila la Dani wakatuma watu tano (5) wa familia yao, wanaume wenye uwezo kutoka Sora na Eshtaoli,+ ili wapeleleze inchi na kuichunguza. Wakawaambia: “Muende, muchunguze inchi.” Wakati walifika kwenye eneo lenye milima la Efraimu, kwenye nyumba ya Mika,+ wakalala pale usiku. 3 Wakati walikuwa karibu na nyumba ya Mika, wakatambua sauti* ya ule kijana Mulawi, basi wakamuendea na kumuuliza: “Ni nani alikuleta hapa? Uko unafanya nini hapa? Ni nini inakufanya ubakie hapa?” 4 Akawajibu: “Mika alinitendea hivi na hivi, na alinipatia kazi ya kuwa kuhani wake.”+ 5 Kisha wakamuambia: “Tafazali, uliza Mungu kama safari yetu itakuwa na matokeo ya muzuri.” 6 Kuhani huyo akawaambia: “Muende kwa amani. Yehova iko* pamoja na ninyi katika safari yenu.”
7 Basi watu hao tano (5) wakaendelea na wakafika Laishi.+ Wakaona namna watu wa kule walikuwa wanaishi bila kutegemea mutu yeyote kama vile Wasidoni. Walikuwa watulivu na hawakukuwa na wasiwasi,+ na hapakukuwa mushindi yeyote mwenye aliwakandamiza wala kuwasumbua. Walikuwa mbali sana na Wasidoni, na hawakukuwa na mambo ya kufanya na watu wengine.
8 Wakati walirudia kwa ndugu zao kule Sora na Eshtaoli,+ ndugu zao wakawauliza: “Mambo yalikuwa namna gani?” 9 Wakajibu: “Tupande kupigana nao, kwa maana tumeona kwamba inchi hiyo ni ya muzuri sana. Sababu gani munasita-sita? Musikawie kuingia ili kukamata inchi hiyo. 10 Wakati mutafika, mutakuta watu wenye hawana wasiwasi,+ na inchi yao ni kubwa. Mungu ameitia katika mukono wenu, mahali kwenye hakukose kitu katika dunia.”+
11 Basi watu mia sita (600) wenye kubeba silaha za vita wa familia ya Wadani wakaondoka Sora na Eshtaoli.+ 12 Wakapanda na kupiga kambi kule Kiriat-yearimu+ katika Yuda. Ndiyo sababu eneo hilo, lenye kuwa upande wa mangaribi wa Kiriat-yearimu, linaitwa Mahane-dani*+ mupaka leo. 13 Wakatoka kule na kuenda kwenye eneo lenye milima la Efraimu, wakafika kwenye nyumba ya Mika.+
14 Kisha wale watu tano (5) wenye walikuwa wameenda kupeleleza inchi ya Laishi+ wakaambia ndugu zao: “Je, mulijua kwamba nyumba hizi ziko na efodi, sanamu za terafimu,* sanamu ya kuchongwa, na sanamu ya metali?*+ Mufikirie kile munapaswa kufanya.” 15 Basi wakasimama pale na kuenda kwenye nyumba ya ule kijana Mulawi,+ kwenye nyumba ya Mika na wakauliza hali yake. 16 Na wakati huo, wale wanaume mia sita (600) wa Dani+ wenye kubeba silaha za vita, walikuwa wamesimama kwenye muingilio wa mulango mukubwa. 17 Wale watu tano (5) wenye walikuwa wameenda kupeleleza inchi+ wakaingia ndani ili kukamata ile sanamu ya kuchongwa, ile efodi,+ zile sanamu za terafimu,*+ na ile sanamu ya metali.*+ (Ule kuhani+ alikuwa anasimama kwenye muingilio wa mulango mukubwa pamoja na wale watu mia sita [600] wenye kubeba silaha za vita.) 18 Wakaingia katika nyumba ya Mika na kukamata ile sanamu ya kuchongwa, ile efodi, zile sanamu za terafimu,* na ile sanamu ya metali.* Ule kuhani akawauliza: “Muko munafanya nini?” 19 Lakini wakamuambia: “Nyamaza. Tia mukono wako kwenye kinywa chako, na utufuate ili ukuwe baba* na kuhani wetu. Ni jambo gani lenye kuwa muzuri zaidi kwako—kuwa kuhani wa nyumba ya mutu mumoja+ ao kuwa kuhani wa kabila na familia katika Israeli?”+ 20 Basi kuhani huyo akatosheka, na akakamata ile efodi, zile sanamu za terafimu,* na ile sanamu ya kuchongwa+ na akaenda pamoja na watu hao.
21 Kisha wakageuka na kuendelea na safari yao, wakapitisha watoto, mifugo, na vitu vya maana sana mbele yao. 22 Wakati walikuwa wamefika mbali kidogo na nyumba ya Mika, wanaume wenye waliishi katika nyumba zenye zilikuwa karibu na nyumba ya Mika wakakusanyika pamoja na kufikia wale Wadani. 23 Wakati walilalamikia Wadani, wakageuka ili kuwaangalia na wakamuuliza Mika: “Kuko shida gani? Sababu gani mumekusanyika pamoja?” 24 Basi akasema: “Mumekamata miungu yangu yenye nilitengeneza, na mumeenda na kuhani pia. Nimebakia na nini? Namna gani basi munaweza kuniuliza, ‘Uko na shida gani?’” 25 Wale Wadani wakajibu: “Usiseme na sisi kwa sauti ya juu; ukifanya vile, watu wenye kasirani* wanaweza kukushambulia, na unaweza kupoteza uzima wako* na uzima wa* watu wa nyumba yako.” 26 Basi Wadani wakaendelea na safari yao; na Mika, wakati aliona kwamba wako na nguvu kuliko yeye, akageuka na kurudia kwenye nyumba yake.
27 Kisha wao kukamata vitu vyenye Mika alikuwa ametengeneza, pamoja na kuhani wake, wakaenda Laishi,+ kwa kikundi cha watu watulivu na wenye hawana wasiwasi.+ Wakawapiga na kuwaua kwa upanga na kuteketeza muji huo kwa moto. 28 Hapakukuwa mutu wa kuokoa muji huo, kwa maana ulikuwa mbali na Sidoni na hawakukuwa na mambo ya kufanya pamoja na watu wengine na muji huo ulikuwa katika bonde tambarare* la Bet-rehobu.+ Kisha wakajenga tena muji huo na kukaa ndani yake. 29 Zaidi ya hiyo, wakaita muji huo Dani+ sawa na jina la baba yao, Dani, muzao wa Israeli.+ Lakini zamani muji huo uliitwa Laishi.+ 30 Kisha Wadani wakajisimamishia ile sanamu ya kuchongwa,+ na Yonatani+ mwana wa Gershomu,+ mwana wa Musa, na wana wake wakakuwa makuhani wa kabila la Dani mupaka siku wakaaji wa inchi walipelekwa katika uhamisho. 31 Na wakasimamisha ile sanamu ya kuchongwa yenye Mika alikuwa ametengeneza, na ikabakia kule siku zote zenye nyumba ya Mungu wa kweli ilikuwa katika Shilo.+