Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Sauli anashinda Waamoni (1-11)

      • Sauli anahakikishwa tena kuwa mufalme (12-15)

1 Samweli 11:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mapatano.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 2:19
  • +Amu 21:8; 1 Sa. 31:11, 12

1 Samweli 11:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 10:26; 14:2

1 Samweli 11:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 3:9, 10; 6:34; 11:29; 14:5, 6; 1 Sa. 10:10, 11; 16:13

1 Samweli 11:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kama mutu mumoja.”

1 Samweli 11:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 11:3

1 Samweli 11:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, karibu saa 8 ya usiku (2:00) mupaka saa 12 ya asubui (6:00).

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 11:1

1 Samweli 11:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 10:26, 27

1 Samweli 11:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 19:22

1 Samweli 11:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 7:15, 16
  • +1 Sa. 10:17, 24

1 Samweli 11:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 7:11
  • +1 Fal. 1:39, 40; 2 Fal. 11:12, 14; 1Nya 12:39, 40

Maandiko ingine

1 Sam. 11:1Kum 2:19
1 Sam. 11:1Amu 21:8; 1 Sa. 31:11, 12
1 Sam. 11:41 Sa. 10:26; 14:2
1 Sam. 11:6Amu 3:9, 10; 6:34; 11:29; 14:5, 6; 1 Sa. 10:10, 11; 16:13
1 Sam. 11:101 Sa. 11:3
1 Sam. 11:111 Sa. 11:1
1 Sam. 11:121 Sa. 10:26, 27
1 Sam. 11:132 Sa. 19:22
1 Sam. 11:141 Sa. 7:15, 16
1 Sam. 11:141 Sa. 10:17, 24
1 Sam. 11:15Law. 7:11
1 Sam. 11:151 Fal. 1:39, 40; 2 Fal. 11:12, 14; 1Nya 12:39, 40
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 11:1-15

Cha Kwanza cha Samweli

11 Basi Nahashi Mwamoni+ akapanda na kupiga kambi ili kushambulia Yabeshi+ kule Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamuambia Nahashi: “Fanya agano* pamoja na sisi, na tutakutumikia.” 2 Nahashi Mwamoni akawaambia: “Nitafanya agano pamoja na ninyi kama tu munakubali jambo hili: macho yenu yote ya kuume yatobolewe. Nitafanya vile ili kuletea haya Israeli wote.” 3 Wazee wa Yabeshi wakamujibu: “Utupatie muda wa siku saba (7) ili tutume wajumbe katika eneo lote la Israeli. Kisha, kama hakuna mutu wa kutuokoa, tutajitia katika mukono wako.” 4 Kisha wakati fulani wajumbe hao wakafika Gibea+ ya Sauli na wakasema maneno hayo katika masikio ya watu, na watu wote wakalia kwa sauti kubwa sana.

5 Lakini Sauli alikuwa anatoka katika eneo la mashamba akiwa nyuma ya mifugo, na Sauli akasema: “Watu wako na shida gani? Sababu gani wanalia?” Kwa hiyo wakamuelezea maneno ya watu wa Yabeshi. 6 Roho ya Mungu ikamutia Sauli nguvu+ wakati alisikia maneno hayo, na akawaka kasirani. 7 Kwa hiyo akakamata ngombe-dume wawili na kuwakata vipande-vipande, na akatuma vipande hivyo katika eneo lote la Israeli kwa mukono wa wajumbe, wenye walisema: “Kila mutu mwenye hafuate Sauli na Samweli ajue kwamba ngombe zake watafanyiwa hivi!” Na woga wa Yehova ukaanguka juu ya watu, na hivyo wakatoka wote pamoja.* 8 Kisha akawahesabu kule Bezeki, na kulikuwa Waisraeli elfu mia tatu (300 000) na watu elfu makumi tatu (30 000) wa Yuda. 9 Sasa wakaambia wajumbe wenye walikuwa wamekuja: “Ni hivi munapaswa kuambia watu wa Yabeshi kule Gileadi, ‘Kesho wakati wa jua kali, mutaokolewa.’” Basi wale wajumbe wakakuja na kuambia watu wa Yabeshi, nao wakashangilia sana. 10 Kwa hiyo watu wa Yabeshi wakasema: “Kesho tutajitia katika mukono wenu, na munaweza kututendea jambo lolote lenye linaonekana kuwa muzuri kwenu.”+

11 Siku yenye ilifuata, Sauli aliwagawa watu katika vikundi tatu (3), na wakaingia katikati ya kambi wakati wa kesha la asubui* na wakapiga na kuua Waamoni+ mupaka wakati jua lilikuwa kali. Watu wenye waliokoka walisambazwa, na hivyo hakuna watu wawili kati yao wenye walibakia pamoja. 12 Kisha watu wakamuambia Samweli: “Ni nani alikuwa anasema, ‘Je, Sauli atakuwa mufalme juu yetu?’+ Mulete watu hao, na sisi tutawaua.” 13 Lakini, Sauli akasema: “Hakuna mutu mwenye atauawa leo,+ kwa maana leo Yehova ameokoa Israeli.”

14 Kisha wakati fulani Samweli akaambia watu: “Mukuje na tuende Gilgali+ ili kuhakikisha tena ufalme.”+ 15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali, na kule Gilgali wakamuweka Sauli kuwa mufalme mbele ya Yehova. Kisha wakatoa kule zabihu za ushirika mbele ya Yehova,+ na Sauli na watu wote wa Israeli wakasherehekea kwa shangwe kubwa.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine