Cha Kwanza cha Samweli
14 Siku moja Yonatani+ mwana wa Sauli alimuambia mutumishi mwenye alimubebea silaha zake: “Kuja na tuvuke tuende kwenye kambi ya mbele ya Wafilisti upande mwingine.” Lakini hakumuambia baba yake. 2 Sauli alikuwa anakaa sehemu za pembeni-pembeni ya Gibea+ chini ya muti wa mukomamanga kule Migroni, na wanaume karibu mia sita (600) walikuwa pamoja naye.+ 3 (Na Ahiya mwana wa Ahitubu,+ ndugu ya Ikabodi,+ mwana wa Finehasi,+ mwana wa Eli,+ kuhani wa Yehova kule Shilo,+ alikuwa amebeba efodi.)+ Na watu hawakujua kwamba Yonatani alikuwa ameenda. 4 Sasa katikati ya njia zenye Yonatani alijaribu kutumia kuvuka ili afike kwenye kambi ya mbele ya Wafilisti, kulikuwa mwamba wenye ulikuwa na umbo ya jino upande huu na mwamba wenye ulikuwa na umbo ya jino upande mwingine; jina la mwamba mumoja lilikuwa Bosesi, na jina la mwamba mwingine lilikuwa Sene. 5 Mwamba mumoja ulikuwa nguzo upande wa kaskazini wenye unaangaliana na Mikmashi, na mwamba mwingine ulikuwa upande wa kusini wenye unaangaliana na Geba.+
6 Kwa hiyo Yonatani akamuambia mubeba-silaha wake: “Kuja na tuvuke tuende kwenye kambi ya mbele ya wanaume hawa wenye hawatahiriwe.+ Pengine Yehova atatenda kwa ajili yetu, kwa maana hakuna kitu chenye kinaweza kumuzuia Yehova kuokoa kwa kutumia watu wengi ao kidogo.”+ 7 Basi mubeba-silaha wake akamuambia: “Fanya jambo lolote lenye moyo wako unakusukuma kufanya. Geukia mahali popote penye unataka, na mimi nitakufuata mahali popote penye moyo wako unakusukuma kuenda.” 8 Halafu Yonatani akasema: “Tutavuka kuenda kwa wanaume hao na kujionyesha kwao. 9 Kama wanatuambia, ‘Musimame mupaka tufike mahali kwenye muko!’ tutasimama mahali tuko na hatutapanda kuenda mahali kwenye wako. 10 Lakini kama wanasema, ‘Mupande kutushambulia!’ tutapanda, kwa sababu Yehova atawatia katika mukono wetu. Hiyo ndiyo itakuwa alama yetu.”+
11 Basi wote wawili wakajionyesha kwa kambi ya mbele ya Wafilisti. Wafilisti wakasema: “Muangalie! Waebrania wanatoka katika mashimo kwenye walikuwa wamejificha.”+ 12 Kwa hiyo watu wa kambi ya mbele wakamuambia Yonatani na mubeba-silaha wake: “Mupande mahali kwenye tuko, na tutawafundisha somo!”+ Mara moja Yonatani akamuambia mubeba-silaha wake: “Unifuate, kwa maana Yehova atawatia katika mukono wa Israeli.”+ 13 Na Yonatani akapanda kwa mikono na miguu yake, na mubeba-silaha wake alikuwa nyuma yake; na Wafilisti wakaanza kuanguka mbele ya Yonatani, na mubeba-silaha wake alikuwa anawaua nyuma ya Yonatani. 14 Katika shambulizi la kwanza lenye Yonatani na mubeba-silaha wake walifanya, walipiga na kuua watu karibu makumi mbili (20) katika karibu nusu ya nafasi yenye inaweza kulimwa kwa jembe katika ekari ya shamba.*
15 Basi woga mukubwa ukaenea katika kambi yenye kuwa katika eneo la mashamba na kati ya watu wote wa kambi ya mbele, na hata vikundi vya washambuliaji+ vikaogopa sana. Dunia ikaanza kutetemeka, na kukakuwa woga mukubwa kutoka kwa Mungu. 16 Walinzi wa Sauli katika muji wa Gibea+ wa Benyamini wakaona kwamba muvurugo ulikuwa unaenea kila upande.+
17 Sauli akaambia watu wenye walikuwa pamoja naye: “Tafazali, muhesabie watu na muone ni nani ametuacha.” Wakati walihesabia, wakaona kwamba Yonatani na mubeba-silaha wake hawakukuwa pale. 18 Basi Sauli akamuambia Ahiya:+ “Leta karibu Sanduku la Mungu wa kweli!” (Kwa maana wakati huo* Sanduku la Mungu wa kweli lilikuwa pamoja na Waisraeli.) 19 Na wakati Sauli alikuwa anaongea na kuhani, muvurugo katika kambi ya Wafilisti ukazidi kuongezeka. Basi Sauli akamuambia kuhani: “Acha kile chenye unafanya.”* 20 Kwa hiyo Sauli na watu wote wenye walikuwa pamoja naye wakakusanyika na kuenda katika pigano, na kule wakavumbua kwamba Wafilisti walikuwa wamegeuza panga zao mumoja kuelekea mwenzake, na muvurugo ulikuwa mukubwa sana. 21 Pia, Waebrania wenye zamani walikuwa upande wa Wafilisti na wenye walikuwa wamepanda pamoja nao na kuingia katika kambi walikuwa wanaenda kujiunga na Israeli chini ya usimamizi wa Sauli na Yonatani. 22 Wanaume wote wa Israeli wenye walikuwa wamejificha+ katika eneo lenye milima la Efraimu wakasikia kwamba Wafilisti walikuwa wamekimbia, nao pia wakaingia katika pigano ili kuwafuatilia. 23 Kwa hiyo Yehova akaokoa Israeli siku hiyo,+ na pigano likafika mupaka Bet-aveni.+
24 Lakini watu wa Israeli walikuwa wamebanwa sana siku hiyo, kwa sababu Sauli alikuwa ametia watu chini ya kiapo hiki: “Alaaniwe mutu mwenye atakula chakula chochote* mbele ya mangaribi na mbele nilipize kisasi juu ya maadui wangu!” Kwa hiyo hakuna mutu kati ya watu mwenye alikula chakula chochote.+
25 Na watu wote wakaingia* katika pori, na asali ilikuwa kwenye udongo. 26 Wakati watu waliingia katika pori, waliona asali ikianguka matone-matone, lakini hakuna mwenye alikuwa anatia mukono wake kwenye kinywa chake, kwa sababu waliogopa kile kiapo. 27 Lakini Yonatani hakusikia wakati baba yake alitia watu chini ya kiapo,+ kwa hiyo akanyoosha chongo ya fimbo yenye ilikuwa katika mukono wake na kuiingiza katika sega la asali. Wakati alirudisha mukono wake katika kinywa chake, macho yake yakangaa. 28 Basi mumoja kati ya watu akasema: “Baba yako alitia watu chini ya kiapo cha nguvu, na kusema, ‘Alaaniwe mutu mwenye atakula chakula leo!’+ Ndiyo sababu watu wamechoka sana. 29 Lakini, Yonatani akasema: “Baba yangu ameleta shida kubwa* katika inchi. Muone namna macho yangu yalingaa kwa sababu nilionja asali hii kidogo. 30 Je, hali haingekuwa muzuri zaidi kama watu wangekula leo kwa uhuru+ sehemu ya vitu vyenye walichukua kutoka kwa maadui wao vyenye walipata? Kwa maana mauaji ya Wafilisti yangekuwa makubwa hata zaidi.”
31 Siku hiyo, wakaendelea kupiga na kuua Wafilisti kuanzia Mikmashi mupaka Aiyaloni,+ na watu wakachoka sana. 32 Kwa hiyo watu wakaanza kukimbilia kwa pupa vitu vyenye vinachukuliwa katika vita, na wakakamata kondoo na ngombe na vitoto-dume vya ngombe na kuwachinjia kwenye udongo, na wakakula nyama pamoja na damu.+ 33 Kwa hiyo Sauli akaambiwa hivi: “Angalia! Watu wanamutendea Yehova zambi kwa kula nyama pamoja na damu.”+ Basi akasema: “Mumetenda kwa ukosefu wa imani. Muviringishe mara moja jiwe kubwa kunielekea.” 34 Kisha Sauli akasema: “Muende kila mahali kati ya watu na muwaambie, ‘Kila mumoja wenu anapaswa kuleta ngombe-dume wake na kondoo wake na muwachinjie hapa na kisha muwakule. Musimutendee Yehova zambi kwa kula nyama pamoja na damu.’”+ Kwa hiyo kila mumoja wao akakuja na ngombe-dume wake usiku huo na kumuchinjia pale. 35 Na Sauli akamujengea Yehova mazabahu.+ Hiyo ndiyo ilikuwa mazabahu ya kwanza yenye alimujengea Yehova.
36 Kisha wakati fulani Sauli akasema: “Tushuke ili kufuatilia Wafilisti usiku na kunyanganya vitu vyao mupaka wakati mwangaza wa asubui utatokea. Hatutaacha hata mutu mumoja aponyoke.” Basi wakasema: “Fanya jambo lolote lenye linaonekana kuwa la muzuri mbele ya macho yako.” Kisha kuhani akasema: “Tumukaribie Mungu wa kweli hapa.”+ 37 Na Sauli akamuuliza Mungu: “Je, nishuke ili kufuatilia Wafilisti?+ Je, utawatia katika mukono wa Israeli?” Lakini Mungu hakumujibu siku hiyo. 38 Kwa hiyo Sauli akasema: “Mukuje hapa, ninyi wakubwa wote wa watu, na mutafute ni zambi gani imefanywa leo. 39 Kwa maana kama vile hakika Yehova anaishi, mwenye aliokoa Israeli, hata kama ni Yonatani mwana wangu, anapaswa kufa.” Lakini hakuna mumoja kati ya watu mwenye alimujibu. 40 Kisha akaambia Israeli wote: “Mutakuwa upande mumoja, na mwana wangu Yonatani na mimi tutakuwa upande mwingine.” Basi watu wakamuambia Sauli: “Fanya jambo lolote lenye linaonekana kuwa la muzuri mbele ya macho yako.”
41 Kisha Sauli akamuambia Yehova: “Ee Mungu wa Israeli, jibu kwa Tumimu!”+ Halafu Yonatani na Sauli wakachaguliwa, na watu wakakuwa huru. 42 Basi Sauli akasema: “Mupige kura+ ili kuamua kati yangu na mwana wangu Yonatani.” Na Yonatani akachaguliwa. 43 Kisha Sauli akamuuliza Yonatani: “Uniambie, umefanya nini?” Kwa hiyo Yonatani akamuambia: “Nilionja tu asali kidogo kwa chongo ya fimbo yenye kuwa katika mukono wangu.+ Mimi huyu! Niko tayari kufa!”
44 Basi Sauli akasema: “Mungu afanye vile na aongeze juu ya hilo kama haukufe, Yonatani.”+ 45 Lakini watu wakamuambia Sauli: “Je, Yonatani anapaswa kufa—yeye mwenye aliletea Israeli ushindi* huu mukubwa?+ Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa! Kama vile hakika Yehova anaishi, hakuna unywele hata mumoja wa kichwa chake wenye utaanguka chini, kwa maana alitenda pamoja na Mungu leo.”+ Kwa hiyo watu wakamuokoa* Yonatani, na hakukufa.
46 Kwa hiyo Sauli akaacha kufuatilia Wafilisti, na Wafilisti wakaenda katika eneo lao.
47 Sauli akafanya ufalme wake kuwa imara juu ya Israeli na akapigana na maadui wake wenye walikuwa kila upande, akapigana na Wamoabu,+ Waamoni,+ Waedomu,+ wafalme wa Soba,+ na Wafilisti;+ na kila mahali kwenye alienda aliwashinda. 48 Na alipigana kwa uhodari na kushinda Waamaleki+ na kuokoa Israeli katika mukono wa wanyanganyi wao.
49 Watoto wanaume wa Sauli walikuwa Yonatani, Ishvi, na Malki-shua.+ Na alikuwa na watoto wanamuke wawili; jina la mukubwa lilikuwa Merabu,+ na jina la mudogo lilikuwa Mikali.+ 50 Jina la bibi ya Sauli lilikuwa Ahinoamu binti ya Ahimaazi. Jina la mukubwa wa jeshi lake lilikuwa Abneri+ mwana wa Neri, ndugu ya baba ya Sauli. 51 Kishi+ alikuwa baba ya Sauli, na Neri+ baba ya Abneri alikuwa mwana wa Abieli.
52 Kulikuwa vita kali pamoja na Wafilisti siku zote za Sauli.+ Wakati Sauli alimuona mwanaume yeyote mwenye nguvu ao hodari, alikuwa anamuandikisha katika utumishi wake.+