Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 3
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Samweli anaitwa ili akuwe nabii (1-21)

1 Samweli 3:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 2:11, 18
  • +Hes 12:6; 1Nya 17:15

1 Samweli 3:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 4:15

1 Samweli 3:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, tabenakulo.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 24:2
  • +1 Sa. 1:9; 3:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2005, uku. 21-22

1 Samweli 3:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Tuige Imani Yao, uku. 64

    Munara wa Mulinzi,

    1/10/2010, uku. 16-17

1 Samweli 3:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amo 3:7

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/12/2002, uku. 8-9

1 Samweli 3:10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Tuige Imani Yao, uku. 64

    Munara wa Mulinzi,

    1/10/2010, uku. 16-17

1 Samweli 3:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 4:17

1 Samweli 3:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 23:19; 1 Sa. 2:31-34; Isa 55:10, 11

1 Samweli 3:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 2:22, 23; Yoh 15:22; Yak 4:17
  • +Hes 15:30; 1 Sa. 2:12, 17
  • +Mhu. 8:11

1 Samweli 3:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 4:11; 22:21; 1 Fal. 2:27

1 Samweli 3:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “lianguke kwenye dunia.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 2:21

1 Samweli 3:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 3:1, 4; Zab 99:6

Maandiko ingine

1 Sam. 3:11 Sa. 2:11, 18
1 Sam. 3:1Hes 12:6; 1Nya 17:15
1 Sam. 3:21 Sa. 4:15
1 Sam. 3:3Law. 24:2
1 Sam. 3:31 Sa. 1:9; 3:15
1 Sam. 3:7Amo 3:7
1 Sam. 3:111 Sa. 4:17
1 Sam. 3:12Hes 23:19; 1 Sa. 2:31-34; Isa 55:10, 11
1 Sam. 3:131 Sa. 2:22, 23; Yoh 15:22; Yak 4:17
1 Sam. 3:13Hes 15:30; 1 Sa. 2:12, 17
1 Sam. 3:13Mhu. 8:11
1 Sam. 3:141 Sa. 4:11; 22:21; 1 Fal. 2:27
1 Sam. 3:191 Sa. 2:21
1 Sam. 3:211 Sa. 3:1, 4; Zab 99:6
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 3:1-21

Cha Kwanza cha Samweli

3 Wakati huo, kijana Samweli alikuwa anamutumikia+ Yehova mbele ya Eli, lakini neno la Yehova halikupatikana sana katika siku hizo; maono+ hayakukuwa mengi.

2 Siku moja Eli alikuwa amelala mahali alizoea kulala, na macho yake yalikuwa yamefifia; hangeweza kuona.+ 3 Taa ya Mungu+ haikukuwa imezimwa, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu*+ la Yehova, mahali kwenye Sanduku la Mungu lilikuwa. 4 Kisha Yehova akamuita Samweli. Samweli akajibu: “Mimi huyu.” 5 Akakimbia kwa Eli na kusema: “Mimi huyu, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema: “Sikukuita. Lala tena.” Basi akaenda na kulala. 6 Yehova akaita tena: “Samweli!” Basi Samweli akaamuka na kuenda kwa Eli na kusema: “Mimi huyu, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli akasema: “Sikukuita, mwana wangu. Lala tena.” 7 (Wakati huo Samweli alikuwa bado hajamujua Yehova, na neno la Yehova lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.)+ 8 Kwa hiyo Yehova akaita tena, mara ya tatu (3): “Samweli!” Basi akaamuka na kuenda kwa Eli na kusema: “Mimi huyu, kwa kuwa umeniita.”

Basi Eli akatambua kwamba ni Yehova alikuwa anamuita kijana huyo. 9 Kwa hiyo Eli akamuambia Samweli: “Uende, ulale, na kama anakuita, umuambie, ‘Sema, Yehova, kwa maana mutumishi wako anasikiliza.’” Na Samweli akaenda na kulala mahali pake.

10 Yehova akakuja na kusimama pale, na akaita kama vile alifanya nyakati zingine: “Samweli, Samweli!” Basi Samweli akasema: “Sema, kwa maana mutumishi wako anasikiliza.” 11 Yehova akamuambia Samweli: “Angalia! Ninafanya jambo fulani katika Israeli lenye litafanya masikio yote mbili ya mutu yeyote mwenye atalisikia yawashe.+ 12 Siku hiyo nitamutendea Eli mambo yote yenye nilisema kuhusu nyumba yake, kuanzia mwanzo mupaka mwisho.+ 13 Unapaswa kumuambia kwamba ninaleta hukumu ya kudumu juu ya nyumba yake kwa sababu ya kosa lenye amejua kulihusu,+ kwa maana wana wake wanamulaani Mungu,+ lakini hakuwakemea.+ 14 Ndiyo sababu nimeapia nyumba ya Eli kwamba kosa la nyumba ya Eli halitafunikwa hata kidogo kupitia zabihu ao kupitia matoleo.”+

15 Samweli akaendelea kulala mupaka asubui; kisha akafungua milango ya nyumba ya Yehova. Samweli akaogopa kumuambia Eli kuhusu maono hayo. 16 Lakini Eli akamuita Samweli: “Samweli, mwana wangu!” Naye akasema: “Mimi huyu.” 17 Eli akauliza: “Alikuambia ujumbe gani? Tafazali, usinifiche. Mungu akufanyie vile na aongeze juu ya hilo kama unanificha hata neno moja kati ya maneno yote yenye alikuambia.” 18 Kwa hiyo Samweli akamuambia kila jambo, na hakumuficha kitu. Eli akasema: “Ni Yehova. Acha afanye mambo ya muzuri mbele ya macho yake.”

19 Samweli akaendelea kukomaa, na Yehova mwenyewe alikuwa pamoja naye+ na hakuruhusu neno lolote kati ya maneno yake yote likose kutimia.* 20 Israeli wote kuanzia Dani mupaka Beer-sheba wakapata habari kwamba Samweli alikuwa amehakikishwa kuwa nabii wa Yehova. 21 Na Yehova akaendelea kutokea kule Shilo, kwa maana Yehova alijifunua kwa Samweli kule Shilo kupitia neno la Yehova.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine