Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 3
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Wafalme

      • Sulemani anamuoa binti ya Farao (1-3)

      • Yehova anamutokea Sulemani katika ndoto (4-15)

        • Sulemani anaomba hekima (7-9)

      • Sulemani anaamua kesi ya mama wawili (16-28)

1 Wafalme 3:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Alichukua.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 7:3, 4; 1 Fal. 7:8; 9:24; 11:1; Ne 13:25-27
  • +2 Sa. 5:7; 1Nya 11:7
  • +1 Fal. 7:1
  • +1 Fal. 8:17-19
  • +1 Fal. 9:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/12/2011, uku. 10

1 Wafalme 3:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 33:17
  • +Kum 12:5, 6; 1 Fal. 5:3; 1Nya 28:6

1 Wafalme 3:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 7:9; 10:8; 1Nya 21:26

1 Wafalme 3:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “pakubwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 16:39, 40; 21:29
  • +2Nya 1:3-6

1 Wafalme 3:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 1:7-10

1 Wafalme 3:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 2:1, 4

1 Wafalme 3:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mutoto mudogo.”

  • *

    Tnn., “na sijue kutoka inje na kuingia ndani.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 29:1; Yer 1:6

1 Wafalme 3:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 19:5, 6

1 Wafalme 3:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “wagumu.” Tnn., “wazito.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 72:1; 119:34
  • +Ebr 5:14

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/6/2007, uku. 27

1 Wafalme 3:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mez. 15:8

1 Wafalme 3:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “siku nyingi.”

  • *

    Ao “nafsi za.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 22:12; 29:19; 2Nya 1:11, 12; Mez. 16:16

1 Wafalme 3:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mhu. 1:16; 1 Yo. 5:14
  • +1 Fal. 4:29; Mez. 2:3-5; Yak 1:5
  • +Mt 12:42

1 Wafalme 3:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “siku zako zote.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 84:11; Mt 6:33; Efe 3:20
  • +1 Fal. 4:21; Mhu. 7:11
  • +1 Fal. 10:23

1 Wafalme 3:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitarefusha siku zako.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 15:5
  • +Zab 21:4; 91:14, 16; Mez. 3:13, 16

1 Wafalme 3:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 7:11

1 Wafalme 3:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kwenye kifua chake.”

1 Wafalme 3:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 29:23-25; Zab 72:5
  • +1 Fal. 3:9, 10

Maandiko ingine

1 Fa. 3:1Kum 7:3, 4; 1 Fal. 7:8; 9:24; 11:1; Ne 13:25-27
1 Fa. 3:12 Sa. 5:7; 1Nya 11:7
1 Fa. 3:11 Fal. 7:1
1 Fa. 3:11 Fal. 8:17-19
1 Fa. 3:11 Fal. 9:15
1 Fa. 3:22Nya 33:17
1 Fa. 3:2Kum 12:5, 6; 1 Fal. 5:3; 1Nya 28:6
1 Fa. 3:31 Sa. 7:9; 10:8; 1Nya 21:26
1 Fa. 3:41Nya 16:39, 40; 21:29
1 Fa. 3:42Nya 1:3-6
1 Fa. 3:52Nya 1:7-10
1 Fa. 3:61 Fal. 2:1, 4
1 Fa. 3:71Nya 29:1; Yer 1:6
1 Fa. 3:8Kut 19:5, 6
1 Fa. 3:9Zab 72:1; 119:34
1 Fa. 3:9Ebr 5:14
1 Fa. 3:10Mez. 15:8
1 Fa. 3:111Nya 22:12; 29:19; 2Nya 1:11, 12; Mez. 16:16
1 Fa. 3:12Mhu. 1:16; 1 Yo. 5:14
1 Fa. 3:121 Fal. 4:29; Mez. 2:3-5; Yak 1:5
1 Fa. 3:12Mt 12:42
1 Fa. 3:13Zab 84:11; Mt 6:33; Efe 3:20
1 Fa. 3:131 Fal. 4:21; Mhu. 7:11
1 Fa. 3:131 Fal. 10:23
1 Fa. 3:141 Fal. 15:5
1 Fa. 3:14Zab 21:4; 91:14, 16; Mez. 3:13, 16
1 Fa. 3:15Law. 7:11
1 Fa. 3:281Nya 29:23-25; Zab 72:5
1 Fa. 3:281 Fal. 3:9, 10
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Wafalme 3:1-28

Cha Kwanza cha Wafalme

3 Sulemani alifanya mapatano ya ndoa pamoja na Farao mufalme wa Misri. Alimuoa* binti ya Farao+ na akamuleta katika Muji wa Daudi+ mupaka wakati alimaliza kujenga nyumba yake mwenyewe,+ na nyumba ya Yehova,+ na ukuta kuzunguka Yerusalemu.+ 2 Lakini watu walikuwa wangali wanatoa zabihu mahali pa juu,+ kwa sababu kufikia wakati huo nyumba kwa ajili ya jina la Yehova ilikuwa bado haijajengwa.+ 3 Sulemani akaendelea kumupenda Yehova kwa kutembea katika sheria za Daudi baba yake, isipokuwa tu alikuwa anatoa zabihu na kuchoma matoleo ili yatoe moshi mahali pa juu.+

4 Mufalme alienda Gibeoni ili kutoa zabihu kule, kwa maana ni pale kulikuwa mahali pa juu penye kujulikana zaidi.*+ Sulemani alitoa zabihu elfu moja (1 000) za kuteketezwa juu ya mazabahu hiyo.+ 5 Katika Gibeoni Yehova alimutokea Sulemani katika ndoto usiku, na Mungu akasema: “Omba kile unataka nikupatie.”+ 6 Basi Sulemani akasema: “Umemuonyesha mutumishi wako Daudi baba yangu upendo mwingi mushikamanifu wakati alikuwa anatembea mbele yako kwa uaminifu na haki na kwa unyoofu wa moyo. Umeendelea kumuonyesha upendo huu mushikamanifu mukubwa mupaka leo kwa kumupatia mwana wa kukaa kwenye kiti chake cha ufalme.+ 7 Na sasa, Yehova Mungu wangu, umemufanya mutumishi wako kuwa mufalme pa nafasi ya Daudi baba yangu, hata kama mimi ni kijana* tu na sina uzoefu.*+ 8 Mutumishi wako iko* kati ya watu wako wenye umechagua,+ watu wengi sana hivi kwamba hawawezi kuhesabiwa ao kujulikana hesabu. 9 Basi patia mutumishi wako moyo mutiifu ili kuhukumu watu wako,+ kufanya tofauti kati ya mambo ya muzuri na mambo ya mubaya,+ kwa maana ni nani mwenye anaweza kuhukumu watu wako hawa wenye ni wengi?”*

10 Lilikuwa jambo lenye kumupendeza Yehova kwamba Sulemani aliomba hilo.+ 11 Basi Mungu akamuambia: “Kwa sababu uliomba jambo hili na haukujiombea maisha ya murefu* ao utajiri ao kifo cha* maadui wako, lakini uliomba uelewaji wa kusikia kesi za hukumu,+ 12 nitafanya mambo yenye uliomba.+ Nitakupatia moyo wenye hekima na uelewaji,+ hivi kwamba kama vile hakujakuwa hata siku moja mutu mwenye kuwa kama wewe, hakutakuwa tena hata siku moja mutu kama wewe.+ 13 Zaidi ya hayo, nitakupatia vitu vyenye haukuomba,+ utajiri na pia utukufu,+ na hivyo hakutakuwa mufalme mwingine kama wewe wakati wa maisha yako yote.*+ 14 Na kama unatembea katika njia zangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile Daudi baba yako alitembea,+ nitakupatia pia maisha ya murefu.”*+

15 Wakati Sulemani aliamuka, akatambua kwamba ilikuwa ndoto. Kisha akaenda Yerusalemu na kusimama mbele ya sanduku la agano la Yehova na akatoa zabihu za kuteketezwa na matoleo ya ushirika+ na akafanya karamu kwa ajili ya watumishi wake wote.

16 Wakati huo makahaba wawili wakaingia kwa mufalme na kusimama mbele yake. 17 Mwanamuke wa kwanza akasema: “Tafazali, bwana wangu, mwanamuke huyu na mimi tunaishi katika nyumba moja, na nilizaa wakati alikuwa katika nyumba. 18 Siku ya tatu (3) kisha mimi kuzaa, mwanamuke huyu pia alizaa. Tulikuwa pamoja, sisi wawili tu; hakuna mutu mwingine mwenye alikuwa pamoja na sisi katika nyumba. 19 Usiku, mwana wa mwanamuke huyu alikufa, kwa sababu alimulalia. 20 Basi akaamuka katikati ya usiku, akachukua mwana wangu kutoka pembeni yangu wakati mutumishi wako mwanamuke alikuwa analala na akamulalisha katika mikono yake,* na akalalisha mwana wake mwenye kufa katika mikono yangu. 21 Wakati niliamuka asubui ili kunyonyesha mwana wangu, nikaona amekufa. Kwa hiyo nikamuchunguza kwa uangalifu asubui na nikaona kwamba haiko mwana wangu mwenye nilikuwa nimezaa.” 22 Lakini ule mwanamuke mwingine akasema: “Hapana, mwana wangu ni ule mwenye kuwa muzima, na mwana wako ni ule mwenye kufa!” Lakini ule mwanamuke wa kwanza alikuwa anasema: “Hapana, mwana wako ni ule mwenye kufa, na mwana wangu ni ule mwenye kuwa muzima.” Ni vile walikuwa wanabishana mbele ya mufalme.

23 Mwishowe mufalme akasema: “Huyu anasema, ‘Huyu ni mwana wangu, mwenye kuwa muzima, na mwana wako ni ule mwenye kufa!’ na ule mwingine anasema, ‘Hapana, mwana wako ni ule mwenye kufa, na mwana wangu ni ule mwenye kuwa muzima!’” 24 Mufalme akasema: “Muniletee upanga.” Basi wakamuletea mufalme upanga. 25 Kisha mufalme akasema: “Mukate ule mutoto mwenye kuwa muzima vipande mbili, na mupatie mwanamuke mumoja nusu moja na mwingine nusu ingine.” 26 Mara moja ule mwanamuke mwenye ule mwana wake alikuwa muzima akamuomba mufalme, kwa maana alisikilia mwana wake huruma. Akasema: “Tafazali, bwana wangu! Umupatie ule mutoto mwenye kuwa muzima! Usimuue hata kidogo!” Lakini ule mwanamuke mwingine alikuwa anasema: “Hatakuwa wangu na hatakuwa wako! Acha wamukate vipande mbili!” 27 Halafu mufalme akajibu: “Mupatie ule mwanamuke wa kwanza ule mutoto mwenye kuwa muzima! Musimuue hata kidogo, kwa maana yeye ndiye mama yake.”

28 Kwa hiyo Israeli wote wakasikia kuhusu uamuzi wenye mufalme alikuwa amefanya, na wakamuogopa mufalme,+ kwa maana waliona kwamba hekima ya Mungu ilikuwa pamoja naye ili kutenda haki.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine