Cha Pili cha Wafalme
14 Katika mwaka wa pili wa Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mufalme wa Israeli, Amazia mwana wa Mufalme Yehoashi wa Yuda akakuwa mufalme. 2 Alikuwa na miaka makumi mbili na tano (25) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka makumi mbili na kenda (29) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yehoadini wa Yerusalemu.+ 3 Aliendelea kufanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova, lakini hapana kama Daudi+ babu yake. Alifanya mambo yote kama vile Yehoashi baba yake alikuwa amefanya.+ 4 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa,+ na watu walikuwa wangali wanatoa zabihu na kuchoma zabihu ili zitoe moshi mahali pa juu.+ 5 Wakati tu ufalme ulikuwa imara chini ya uongozi wake, alipiga na kuua watumishi wake wenye walikuwa wamemupiga na kumuua mufalme, baba yake.+ 6 Lakini hakuua wana wa wauaji hao, kulingana na amri ya Yehova yenye imeandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa: “Baba hawapaswe kuuawa kwa sababu ya wana wao, na wana hawapaswe kuuawa kwa sababu ya baba zao; lakini kila mutu anapaswa kuuawa kwa sababu ya zambi yake mwenyewe.”+ 7 Akapiga na kuua Waedomu+ katika Bonde la Chumvi,+ wanaume elfu kumi (10 000), na akakamata Sela katika vita,+ na jina la mahali pale likakuwa Yokteeli mupaka leo.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mufalme wa Israeli, akisema: “Kuja, tupambane katika pigano.”*+ 9 Mufalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mufalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba katika Lebanoni lilituma ujumbe kwa mwerezi katika Lebanoni, ‘Patia mwana wangu binti yako akuwe bibi yake.’ Hata hivyo, munyama wa pori wa Lebanoni akapita karibu na akakanyanga-kanyanga gugu hilo lenye miiba. 10 Ni kweli, umepiga Edomu,+ basi moyo wako umekuwa na majivuno. Furahia utukufu wako, lakini bakia katika nyumba yako mwenyewe.* Sababu gani ulete musiba na uanguke, na kuangusha Yuda pamoja na wewe?” 11 Lakini Amazia hakusikiliza.+
Basi Mufalme Yehoashi wa Israeli akapanda, naye pamoja na Mufalme Amazia wa Yuda wakapambana katika pigano kule Bet-shemeshi,+ ya Yuda.+ 12 Yuda wakashindwa mbele ya Israeli, basi kila mumoja akakimbilia kwenye nyumba yake.* 13 Mufalme Yehoashi wa Israeli akamukamata Mufalme Amazia wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Ahazia, kule Bet-shemeshi. Kisha wakakuja Yerusalemu, na akatoboa tundu katika ukuta wa Yerusalemu kuanzia Mulango Mukubwa wa Efraimu+ mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Pembe,+ urefu wa mikono mia ine (400).* 14 Akakamata zahabu yote na feza na vyombo vyote vyenye vilikuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mufalme, na pia watu wenye walikamatwa. Kisha akarudia Samaria.
15 Na mambo mengine ya historia ya Yehoashi, mambo yenye alifanya, na nguvu zake na namna alipigana na Mufalme Amazia wa Yuda, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 16 Kisha Yehoashi akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake na akazikwa katika Samaria+ pamoja na wafalme wa Israeli; na Yeroboamu*+ mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.
17 Amazia+ mwana wa Yehoashi mufalme wa Yuda aliishi miaka kumi na tano (15) kisha kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mufalme wa Israeli.+ 18 Na mambo mengine ya historia ya Amazia, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 19 Kisha wakati fulani mupango mubaya ukafanywa juu yake+ kule Yerusalemu, na akakimbilia Lakishi, lakini wakatuma watu wamufuatilie kule Lakishi na wakamuua kule. 20 Basi wakamubeba juu ya farasi na kumurudisha, na akazikwa katika Yerusalemu pamoja na mababu zake katika Muji wa Daudi.+ 21 Kisha watu wote wa Yuda wakamuchukua Azaria,*+ mwenye alikuwa na miaka kumi na sita (16),+ na wakamufanya kuwa mufalme pa nafasi ya Amazia baba yake.+ 22 Alijenga upya Elati+ na kuirudisha kwa Yuda kisha mufalme* kulalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake.+
23 Katika mwaka wa kumi na tano (15) wa Amazia mwana wa Yehoashi mufalme wa Yuda, Yeroboamu+ mwana wa Mufalme Yehoashi wa Israeli akakuwa mufalme katika Samaria, na alitawala kwa miaka makumi ine na moja (41). 24 Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova. Hakuacha zambi zote zenye Yeroboamu mwana wa Nebati alikuwa amefanya Israeli watende.+ 25 Alirudisha mupaka wa Israeli kuanzia Lebo-hamati*+ mupaka kwenye Bahari ya Araba,*+ kulingana na neno lenye Yehova Mungu wa Israeli alisema kupitia Yona mutumishi wake+ mwana wa Amitai, nabii kutoka Gat-heferi.+ 26 Kwa maana Yehova alikuwa ameona mateso machungu sana ya Israeli.+ Hapakukuwa mutu yeyote mwenye kubakia wa kusaidia Israeli, hapakukuwa hata mutu mwenye hana uwezo ao mwenye kuwa muzaifu. 27 Lakini Yehova alikuwa ameahidi kwamba hatafuta jina la Israeli kutoka chini ya mbingu.+ Basi akawaokoa kwa mukono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.+
28 Na mambo mengine ya historia ya Yeroboamu, mambo yote yenye alifanya, na nguvu zake, namna alipigana na namna alirudisha Damasko+ na Hamati+ kwa Yuda katika Israeli, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 29 Kisha Yeroboamu akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake, pamoja na wafalme wa Israeli; na Zekaria mwana wake+ akakuwa mufalme pa nafasi yake.