Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Wafalme

      • Hoshea, mufalme wa Israeli (1-4)

      • Kuanguka kwa Israeli (5, 6)

      • Waisraeli wanahamishwa kwa sababu ya uasi-imani (7-23)

      • Wageni wanaletwa katika miji ya Samaria (24-26)

      • Muchanganyiko wa dini katika Samaria (27-41)

2 Wafalme 17:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 15:30

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,”

    uku. 148-149

2 Wafalme 17:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 18:9; Isa 10:5, 6; Ho 10:14, 15
  • +2 Fal. 18:14

2 Wafalme 17:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 31:1

2 Wafalme 17:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ho 13:16
  • +Law. 26:32, 33; Kum 4:27; 28:64; 1 Fal. 14:15
  • +1Nya 5:26
  • +2 Fal. 18:9-11

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,”

    uku. 145, 156

2 Wafalme 17:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Waliogopa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:2
  • +Kut 20:5

2 Wafalme 17:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, katika kila mahali, ikuwe panaikaliwa na watu kidogo ao wengi.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ho 12:11

2 Wafalme 17:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 34:13; Kum 16:21, 22
  • +Kum 12:2; Isa 57:5

2 Wafalme 17:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 20:23

2 Wafalme 17:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:28-30; 21:25, 26
  • +Kut 20:3-5; Law. 26:1; Kum 4:23

2 Wafalme 17:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 24:18, 19; 36:15, 16; Yer 25:4
  • +Isa 55:7

2 Wafalme 17:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wakafanya shingo zao kuwa ngumu kama shingo za.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 1:32; 31:27

2 Wafalme 17:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 5:2; 29:12
  • +Ho 4:6
  • +Kum 32:21; 1 Sa. 12:21
  • +Zab 115:4-8; Isa 44:9
  • +Kum 12:30

2 Wafalme 17:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “sanamu za kuyeyushwa.”

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:28-30
  • +1 Fal. 14:15; 16:33
  • +Kum 4:19; Yer 8:2
  • +1 Fal. 16:30, 31; 22:51, 53; 2 Fal. 10:21; 23:4, 5

2 Wafalme 17:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kujiuzisha.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 16:1, 3
  • +Kum 18:10; Mik 5:12

2 Wafalme 17:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 23:12, 13; Isa 42:24

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 145

2 Wafalme 17:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 14:22; Yer 3:8
  • +Eze 23:4, 11

2 Wafalme 17:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:20

2 Wafalme 17:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:28-30

2 Wafalme 17:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:45, 63; 1 Fal. 14:16; Ho 1:4; Amo 5:27; Mik 1:6
  • +2 Fal. 18:11

2 Wafalme 17:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 19:11, 13

2 Wafalme 17:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “hawakumuabudu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 23:29

2 Wafalme 17:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “desturi za dini.”

2 Wafalme 17:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kumuabudu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 28:18, 19; Yosh. 16:1; 1 Fal. 12:28, 29
  • +Yoh 4:20-22

2 Wafalme 17:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “miungu yake.”

2 Wafalme 17:30

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 17:24

2 Wafalme 17:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 18:34

2 Wafalme 17:32

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:31, 32; 13:33

2 Wafalme 17:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “desturi za dini.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 17:24, 41

2 Wafalme 17:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “desturi za dini.”

  • *

    Tnn., “anamuogopa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 32:28

2 Wafalme 17:35

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 19:5; 24:7; Kum 29:1
  • +Kut 20:3-5; 23:24; 34:14; Kum 5:9

2 Wafalme 17:36

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 6:6
  • +Kum 6:12, 13

2 Wafalme 17:37

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 31:9

2 Wafalme 17:38

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 4:23

2 Wafalme 17:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “desturi za dini.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 17:34

2 Wafalme 17:41

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ezr 4:1, 2

Maandiko ingine

2 Fa. 17:12 Fal. 15:30
2 Fa. 17:32 Fal. 18:9; Isa 10:5, 6; Ho 10:14, 15
2 Fa. 17:32 Fal. 18:14
2 Fa. 17:4Isa 31:1
2 Fa. 17:6Ho 13:16
2 Fa. 17:6Law. 26:32, 33; Kum 4:27; 28:64; 1 Fal. 14:15
2 Fa. 17:61Nya 5:26
2 Fa. 17:62 Fal. 18:9-11
2 Fa. 17:7Kut 20:2
2 Fa. 17:7Kut 20:5
2 Fa. 17:9Ho 12:11
2 Fa. 17:10Kut 34:13; Kum 16:21, 22
2 Fa. 17:10Kum 12:2; Isa 57:5
2 Fa. 17:11Law. 20:23
2 Fa. 17:121 Fal. 12:28-30; 21:25, 26
2 Fa. 17:12Kut 20:3-5; Law. 26:1; Kum 4:23
2 Fa. 17:132Nya 24:18, 19; 36:15, 16; Yer 25:4
2 Fa. 17:13Isa 55:7
2 Fa. 17:14Kum 1:32; 31:27
2 Fa. 17:15Kum 5:2; 29:12
2 Fa. 17:15Ho 4:6
2 Fa. 17:15Kum 32:21; 1 Sa. 12:21
2 Fa. 17:15Zab 115:4-8; Isa 44:9
2 Fa. 17:15Kum 12:30
2 Fa. 17:161 Fal. 12:28-30
2 Fa. 17:161 Fal. 14:15; 16:33
2 Fa. 17:16Kum 4:19; Yer 8:2
2 Fa. 17:161 Fal. 16:30, 31; 22:51, 53; 2 Fal. 10:21; 23:4, 5
2 Fa. 17:172 Fal. 16:1, 3
2 Fa. 17:17Kum 18:10; Mik 5:12
2 Fa. 17:18Yosh. 23:12, 13; Isa 42:24
2 Fa. 17:191 Fal. 14:22; Yer 3:8
2 Fa. 17:19Eze 23:4, 11
2 Fa. 17:211 Fal. 12:20
2 Fa. 17:221 Fal. 12:28-30
2 Fa. 17:23Kum 28:45, 63; 1 Fal. 14:16; Ho 1:4; Amo 5:27; Mik 1:6
2 Fa. 17:232 Fal. 18:11
2 Fa. 17:242 Fal. 19:11, 13
2 Fa. 17:25Kut 23:29
2 Fa. 17:28Mwa 28:18, 19; Yosh. 16:1; 1 Fal. 12:28, 29
2 Fa. 17:28Yoh 4:20-22
2 Fa. 17:302 Fal. 17:24
2 Fa. 17:312 Fal. 18:34
2 Fa. 17:321 Fal. 12:31, 32; 13:33
2 Fa. 17:332 Fal. 17:24, 41
2 Fa. 17:34Mwa 32:28
2 Fa. 17:35Kut 19:5; 24:7; Kum 29:1
2 Fa. 17:35Kut 20:3-5; 23:24; 34:14; Kum 5:9
2 Fa. 17:36Kut 6:6
2 Fa. 17:36Kum 6:12, 13
2 Fa. 17:37Kum 31:9
2 Fa. 17:38Kum 4:23
2 Fa. 17:402 Fal. 17:34
2 Fa. 17:41Ezr 4:1, 2
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Wafalme 17:1-41

Cha Pili cha Wafalme

17 Katika mwaka wa kumi na mbili (12) wa Mufalme Ahazi wa Yuda, Hoshea+ mwana wa Ela akakuwa mufalme juu ya Israeli katika Samaria; alitawala kwa miaka kenda (9). 2 Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, lakini hapana kwa kadiri yenye wafalme wa Israeli wenye walimutangulia walitenda. 3 Mufalme Shalmanesa wa Ashuru akapanda kuja kumushambulia,+ na Hoshea akakuwa mutumishi wake na akaanza kumulipa ushuru.+ 4 Lakini, mufalme wa Ashuru akapata habari kwamba Hoshea alishiriki katika mupango fulani mubaya, kwa maana alikuwa ametuma wajumbe kwa Mufalme So wa Misri+ na hakuleta ushuru kwa mufalme wa Ashuru kama vile alifanya miaka yenye ilitangulia. Kwa hiyo, mufalme wa Ashuru akamufunga na kumutia katika gereza.

5 Mufalme wa Ashuru akashambulia inchi yote, na akakuja Samaria na kwa miaka tatu (3) aliizunguka kwa ajili ya vita. 6 Katika mwaka wa kenda (9) wa Hoshea, mufalme wa Ashuru akakamata Samaria.+ Kisha akakamata na kupeleka watu wa Israeli katika uhamisho+ kule Ashuru na akawakalisha katika Hala na Habori kwenye muto Gozani+ na katika miji ya Wamedi.+

7 Jambo hilo lilitendeka kwa sababu watu wa Israeli walikuwa wamemutendea zambi Yehova Mungu wao, mwenye aliwapandisha kutoka katika inchi ya Misri kutoka katika mukono wa Farao mufalme wa Misri.+ Waliabudu* miungu mingine,+ 8 walifuata desturi za mataifa yenye Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya Waisraeli, na walifuata desturi zenye wafalme wa Israeli walikuwa wameanzisha.

9 Waisraeli walikuwa wanafuatilia mambo yenye hayakukuwa sawa kulingana na Yehova Mungu wao. Waliendelea kujenga mahali pa juu katika miji yao yote,+ kuanzia munara wa mulinzi mupaka kwenye muji wenye ngome.* 10 Waliendelea kujisimamishia nguzo takatifu na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wenye majani mengi;+ 11 na walikuwa wanachoma zabihu ili zitoe moshi mahali pote pa juu kama vile mataifa yenye Yehova alikuwa amepeleka katika uhamisho kutoka mbele yao yalifanya.+ Waliendelea kufanya mambo maovu ili kumukasirisha Yehova.

12 Waliendelea kutumikia sanamu zenye kuchukiza,*+ zenye Yehova alikuwa amewaambia kuzihusu: “Hamupaswe kufanya jambo hili!”+ 13 Yehova aliendelea kuonya Israeli na Yuda kupitia manabii wake wote na kupitia kila muonaji,+ kwa kusema: “Mugeuke na kuacha njia zenu zenye uovu!+ Mushike amri zangu na sheria zangu kulingana na sheria yote yenye niliamuru mababu zenu na yenye nilituma kwenu kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, na wakaendelea kuwa kichwa-nguvu kama* mababu zao wenye hawakuonyesha imani katika Yehova Mungu wao.+ 15 Waliendelea kukataa masharti yake na agano lake+ lenye alikuwa amefanya pamoja na mababu zao na vikumbusho vyake vyenye alikuwa ametoa ili kuwaonya,+ na wakaendelea kufuata sanamu zenye hazina mafaa yoyote+ na wao wenyewe wakakuwa wenye hawana mafaa yoyote,+ kwa kuiga mataifa yenye kuwazunguka pande zote yenye Yehova alikuwa amewaamuru wasiige.+

16 Waliendelea kuacha amri zote za Yehova Mungu wao, na wakatengeneza sanamu za metali* za vitoto-dume mbili vya ngombe,+ na muti mutakatifu,*+ na wakainamia jeshi lote la mbinguni+ na kutumikia Baali.+ 17 Pia walipitisha watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto,+ walifanya uaguzi na walitafuta alama za mambo yenye yatatokea,+ na waliendelea kujitoa* wenyewe ili kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, ili kumukasirisha.

18 Basi Yehova akakasirikia sana Israeli, na hivyo akawaondoa mbele ya macho yake.+ Hakuacha mutu yeyote abakie isipokuwa kabila la Yuda tu.

19 Hata Yuda hawakushika amri za Yehova Mungu wao;+ walitembea pia katika desturi zenye Israeli walifuata.+ 20 Yehova alikataa wazao wote wa Israeli na akawapatisha haya na kuwatia katika mukono wa wanyanganyi, mupaka wakati alikuwa amewatupilia mbali kutoka mbele yake. 21 Alimuondoa Israeli kwa nguvu kutoka kwenye nyumba ya Daudi, na wakafanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mufalme.+ Lakini Yeroboamu akafanya Israeli wakose kumufuata Yehova, na akafanya watende zambi kubwa. 22 Na watu wa Israeli wakaendelea kutembea katika zambi zote zenye Yeroboamu alikuwa ametenda.+ Hawakuziacha 23 mupaka wakati Yehova alitosha Israeli mbele ya macho yake, kama vile alikuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii.+ Basi Israeli wakaondolewa katika inchi yao na wakapelekwa katika uhamisho kule Ashuru,+ wanakaa kule mupaka leo.

24 Kisha mufalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babiloni, Kuta, Ava, Hamati, na Sefarvaimu+ na akawakalisha katika miji ya Samaria pa nafasi ya Waisraeli; wakakamata Samaria na kuishi katika miji yake. 25 Wakati walianza kukaa kule, hawakumuogopa* Yehova. Basi Yehova akatuma simba katikati yao,+ na wakaua wamoja kati ya watu. 26 Mufalme wa Ashuru akapata habari hii: “Mataifa yenye ulipeleka katika uhamisho na kukalisha katika miji ya Samaria hawajue dini* ya Mungu wa inchi hiyo. Basi anaendelea kutuma simba katikati yao; na simba hao wanawaua, kwa sababu hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anajua dini ya Mungu wa inchi hiyo.”

27 Halafu mufalme wa Ashuru akaamuru: “Murudishe mumoja wa makuhani wenye mulipeleka katika uhamisho arudie na aishi kule na awafundishe dini ya Mungu wa inchi hiyo.” 28 Basi mumoja wa makuhani wenye walikuwa wamepelekwa katika uhamisho kutoka Samaria akarudia na kuishi Beteli,+ na akaanza kuwafundisha namna wanapaswa kumuogopa* Yehova.+

29 Hata hivyo, kila taifa tofauti likajitengenezea mungu wake* mwenyewe na kumuweka katika nyumba za ibada mahali pa juu penye Wasamaria walikuwa wamejenga; kila taifa tofauti lilifanya vile katika miji yenye walikuwa wanaishi ndani. 30 Basi watu wa Babiloni wakatengeneza Sukot-benoti, watu wa Kuti wakatengeneza Nergali, watu wa Hamati+ wakatengeneza Ashima, 31 na Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki. Wasefarvaimu walikuwa wanateketeza wana wao katika moto kwa ajili ya Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.+ 32 Hata kama walimuogopa Yehova, waliweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kawaida, na makuhani hao walitumika kwa ajili yao katika nyumba za ibada mahali pa juu.+ 33 Kwa hiyo, walimuogopa Yehova, lakini waliabudu miungu yao wenyewe kulingana na dini* ya mataifa yenye walikuwa wameletwa kutoka ndani.+

34 Mupaka leo wanafuata dini* zao za zamani. Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anamuabudu* Yehova, na hakuna mutu yeyote mwenye anafuata sheria zake, hukumu zake, Sheria, na amri yenye Yehova alipatia wana wa Yakobo, mwenye jina lake alilibadilisha kuwa Israeli.+ 35 Wakati Yehova alifanya agano pamoja nao,+ aliwaamuru: “Hamupaswe kuogopa miungu mingine, na hamupaswe kuiinamia ao kuitumikia ao kuitolea zabihu.+ 36 Lakini Yehova, mwenye aliwapandisha ninyi kutoka katika inchi ya Misri kwa nguvu nyingi na kwa mukono wenye kunyooshwa,+ Yeye ndiye munapaswa kuogopa,+ na munapaswa kumuinamia yeye, na munapaswa kumutolea yeye zabihu. 37 Na masharti, hukumu, Sheria, na amri yenye aliandika kwa ajili yenu,+ munapaswa kuzifuata kwa uangalifu, na hamupaswe kuogopa miungu mingine. 38 Na hamupaswe kusahau agano lenye nilifanya pamoja na ninyi,+ na hamupaswe kuogopa miungu mingine. 39 Lakini Yehova Mungu wenu ndiye munapaswa kuogopa, kwa kuwa yeye ndiye atawaokoa ninyi kutoka katika mukono wa maadui wenu wote.”

40 Lakini hawakutii, na wakafuata dini* yao ya zamani.+ 41 Basi mataifa hayo yakamuogopa Yehova,+ lakini yalikuwa pia yanatumikia sanamu zao wenyewe za kuchongwa. Wana wao na pia wajukuu wao wamekuwa wakitenda kama vile mababu zao walitenda, mupaka leo.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine