Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
8 Benyamini+ akamuzaa Bela+ muzaliwa wake wa kwanza, wa pili Ashbeli,+ wa tatu (3) Ahara, 2 wa ine (4) Noha, na wa tano (5) Rafa. 3 Wana wa Bela walikuwa Adari, Gera,+ Abihudi, 4 Abishua, Naamani, Ahoa, 5 Gera, Shefufani, na Huramu. 6 Hawa ndio walikuwa wana wa Ehudi, vichwa vya jamaa za upande wa baba za wakaaji wa Geba,+ wenye walikamatwa na kupelekwa katika uhamisho kule Manahati: 7 Naamani, Ahiya, na Gera—yeye ndiye aliwakamata na kuwapeleka katika uhamisho na akazaa Uza na Ahihudi. 8 Shaharaimu akazaa watoto katika eneo* la Moabu kisha kuwafukuza. Hushimu na Baara walikuwa bibi zake.* 9 Na kupitia Hodeshi bibi yake, akamuzaa Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu, 10 Yeuzi, Sakia, na Mirma. Hao walikuwa wana wake, vichwa vya jamaa za upande wa baba.
11 Kupitia Hushimu akazaa Abitubu na Elpaali. 12 Na wana wa Elpaali walikuwa Eberi, Mishamu, Shemedi (mwenye alijenga Ono+ na Lodi+ na miji yake ya pembeni-pembeni*), 13 Beria, na Shema. Hao walikuwa vichwa vya jamaa za upande wa baba za wakaaji wa Aiyaloni.+ Hao walifukuza wakaaji wa Gati. 14 Na kulikuwa Ahio, Shashaki, Yeremoti, 15 Zebadia, Aradi, Ederi, 16 Mikaeli, Ishpa, Yoha, wana wa Beria; 17 na Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi, 18 Ishmerai, Izlia, Yobabu, wana wa Elpaali; 19 na Yakimu, Zikri, Zabdi, 20 Elienai, Ziletai, Elieli, 21 Adaya, Beraya, Shimrati, wana wa Shimei; 22 na Ishpani, Eberi, Elieli, 23 Abdoni, Zikri, Hanani, 24 Hanania, Elamu, Antotiya, 25 Ifdeya, Penueli, wana wa Shashaki; 26 na Shamsherai, Sheharia, Atalia, 27 Yaareshia, Eliya, Zikri, wana wa Yerohamu. 28 Hao ndio walikuwa vichwa vya jamaa za upande wa baba kulingana na wazao wao. Vichwa hao waliishi katika Yerusalemu.
29 Yeieli, baba ya Gibeoni, aliishi katika Gibeoni.+ Jina la bibi yake lilikuwa Maaka.+ 30 Na mwana wake muzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, kisha Suri, Kishi, Baali, Nadabu, 31 Gedori, Ahio, na Zekeri. 32 Mikloti akamuzaa Shimea. Na wote waliishi karibu na ndugu zao katika Yerusalemu, pamoja na ndugu zao wengine.
33 Neri+ akamuzaa Kishi; Kishi akamuzaa Sauli;+ Sauli akamuzaa Yonatani,+ Malki-shua,+ Abinadabu,+ na Eshbaali.*+ 34 Na mwana wa Yonatani alikuwa Merib-baali.*+ Merib-baali akamuzaa Mika.+ 35 Na wana wa Mika walikuwa Pitoni, Meleki, Tarea, na Ahazi. 36 Ahazi akamuzaa Yehoada; Yehoada akamuzaa Alemeti, Azmaveti, na Zimri. Zimri akamuzaa Mosa. 37 Mosa akamuzaa Binea, Rafa mwana wake, Eleasa mwana wake, Aseli mwana wake. 38 Aseli alikuwa na wana sita (6), na majina yao yalikuwa Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia, na Hanani. Hao wote ndio walikuwa wana wa Aseli. 39 Na wana wa Esheki ndugu yake walikuwa Ulamu muzaliwa wake wa kwanza, wa pili Yeushi, na wa tatu (3) Elifeleti. 40 Na wana wa Ulamu walikuwa wapiganaji-vita wenye nguvu wenye wanaweza kushika* upinde, na walikuwa na wana wengi na wajukuu wengi, hesabu yao ilikuwa mia moja makumi tano (150). Hao wote walikuwa wazao wa Benyamini.