Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
11 Kisha wakati fulani Waisraeli wote wakakusanyika kwa Daudi kule Hebroni+ na kusema: “Angalia! Sisi ni mufupa wako na nyama yako mwenyewe.*+ 2 Zamani wakati Sauli alikuwa mufalme, wewe ndiye ulikuwa unaongoza Israeli katika mapambano yao ya kijeshi.*+ Na Yehova Mungu wako alikuambia: ‘Utachunga watu wangu Israeli, na utakuwa kiongozi juu ya watu wangu Israeli.’”+ 3 Basi wazee wote wa Israeli wakakuja kwa mufalme kule Hebroni, na Daudi akafanya agano pamoja nao katika Hebroni mbele ya Yehova. Kisha wakamutia Daudi mafuta ili akuwe mufalme juu ya Israeli,+ kulingana na neno la Yehova kupitia Samweli.+
4 Kisha wakati fulani Daudi na Israeli wote wakaondoka na kuenda Yerusalemu, ni kusema, Yebusi,+ kwenye Wayebusi+ walikuwa wanaishi katika inchi hiyo. 5 Wakaaji wa Yebusi walimuchokoza Daudi: “Hautaingia humu hata kidogo!+ Hata hivyo, Daudi alikamata ngome ya Sayuni,+ yenye sasa ni Muji wa Daudi.+ 6 Kwa hiyo Daudi akasema: “Mutu yeyote mwenye atakuwa wa kwanza kupiga Wayebusi atakuwa kiongozi* na mukubwa.” Na Yoabu+ mwana wa Seruya akapanda wa kwanza, na akakuwa mukubwa. 7 Kisha Daudi akaanza kukaa katika ngome hiyo. Ndiyo sababu waliiita Muji wa Daudi. 8 Akaanza kujenga muji huo kuzunguka pande zote, kuanzia kwenye Kilima* mupaka kwenye maeneo ya pembeni-pembeni, na Yoabu akajenga upya sehemu zenye kubakia za muji huo. 9 Basi Daudi akakuwa mukubwa zaidi na zaidi,+ na Yehova wa majeshi alikuwa pamoja naye.
10 Sasa hawa ndio vichwa vya wapiganaji-vita wenye nguvu wa Daudi, wenye walimuunga mukono kabisa katika ufalme wake, pamoja na Israeli wote, ili wamufanye kuwa mufalme kulingana na neno la Yehova juu ya Israeli.+ 11 Hii ndiyo oroza ya wapiganaji-vita wenye nguvu wa Daudi: Yashobeamu+ mwana wa Muhakmoni, kichwa cha wale watatu (3).+ Aliinua mukuki wake juu ya watu mia tatu (300) na kuwaua kwa wakati mumoja.+ 12 Mwenye kumufuata alikuwa Eleazari+ mwana wa Dodo mwana wa Ahohi.+ Alikuwa kati ya wale wapiganaji-vita watatu (3) wenye nguvu. 13 Alikuwa pamoja na Daudi kule Pas-damimu,+ kwenye Wafilisti walikuwa wamekusanyika pamoja kwa ajili ya vita. Sasa kulikuwa shamba lenye kujaa shayiri, na watu walikuwa wamekimbia kwa sababu ya Wafilisti. 14 Lakini alisimama katikati ya shamba hilo na kulilinda na aliendelea kupiga na kuua Wafilisti, na hivyo Yehova akaleta ushindi* mukubwa.+
15 Watatu (3) kati ya wale vichwa makumi tatu (30) walishuka kuenda kwenye mwamba, kwa Daudi katika pango la Adulamu,+ wakati jeshi la Wafilisti lilikuwa limepiga kambi katika Bonde* la Refaimu.+ 16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ile ngome, na kambi ya kijeshi ya Wafilisti ilikuwa katika Betlehemu. 17 Kisha Daudi akaonyesha tamaa yake kwa kusema: “Kama tu ningekunywa maji ya tangi lenye kuwa karibu na mulango mukubwa wa Betlehemu!”+ 18 Halafu wale watatu (3) wakaingia kwa nguvu katika kambi ya Wafilisti na wakashota maji katika tangi hilo lenye kuwa karibu na mulango mukubwa wa Betlehemu na wakayaletea Daudi; lakini Daudi akakataa kuyakunywa na akayamwanga mbele ya Yehova. 19 Akasema: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwa upande wangu kwa maoni ya Mungu wangu kufanya jambo hilo! Je, nikunywe damu ya wanaume hawa wenye walitia uzima wao* katika hatari?”+ Kwa maana walitia uzima wao* katika hatari kwa kuenda kuyaleta. Basi akakataa kuyakunywa. Hayo ndiyo mambo yenye wale wapiganaji-vita watatu (3) wenye nguvu walifanya.
20 Abishai+ ndugu ya Yoabu+ akakuwa kichwa cha wengine watatu (3); aliinua mukuki wake juu ya watu mia tatu (300) na kuwaua, na alikuwa na sifa kama wale watatu.+ 21 Kati ya wale wengine watatu (3), alikuwa na sifa kuliko wale wengine wawili kati yao, na alikuwa mukubwa juu yao; lakini hakufikia wale watatu wa kwanza.
22 Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa mwanaume hodari* mwenye alifanya matendo mengi ya uhodari katika Kabzeeli.+ Alipiga na kuua wana wawili wa Arieli wa Moabu, na alishuka ndani ya shimo la maji siku ya teluji* na kumuua simba.+ 23 Alimupiga na kumuua pia mwanaume Mumisri mwenye alikuwa na ukubwa wa ajabu—mwenye urefu wa mikono tano (5).*+ Hata kama Mumisri huyo alikuwa na mukuki katika mukono wake kama muti wa wasukaji wa nguo,+ alienda kupambana naye akiwa na fimbo na akanyanganya Mumisri huyo mukuki kutoka katika mukono wake na akamuua kwa mukuki wake mwenyewe.+ 24 Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, na alikuwa na sifa kama ya wale wapiganaji-vita watatu (3) wenye nguvu. 25 Ijapokuwa alikuwa na sifa hata kuliko wale makumi tatu (30), hakufikia wale watatu (3).+ Lakini Daudi alimuweka juu ya walinzi wake mwenyewe.
26 Wapiganaji-vita wenye nguvu wa majeshi walikuwa Asaheli+ ndugu ya Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Betlehemu,+ 27 Shamoti Muharori, Helezi Mupeloni, 28 Ira+ mwana wa Ikeshi Mutekoa, Abiezeri+ Mwanatoti, 29 Sibekai + Muhusha, Ilai Mwahohi, 30 Maharai+ Munetofa, Heledi+ mwana wa Baana Munetofa, 31 Itai mwana wa Ribai wa Gibea ya Wabenyamini,+ Benaya Mupiratoni, 32 Hurai wa mabonde ya muto* ya Gaashi,+ Abieli Mwarbati, 33 Azmaveti Mubaharumu, Eliaba Mushaalboni, 34 wana wa Hashemu Mugizoni, Yonatani mwana wa Shagee Muharari, 35 Ahiamu mwana wa Sakari Muharari, Elifali mwana wa Uru, 36 Heferi Mumekerati, Ahiya Mupeloni, 37 Hezro Mukarmeli, Naarai mwana wa Ezbai, 38 Yoeli ndugu ya Natani, Mibhari mwana wa Hagri, 39 Seleki Mwamoni, Naharai Muberoti, mubeba-silaha wa Yoabu mwana wa Seruya; 40 Ira Mwitri, Garebu Mwitri, 41 Uria+ Muhiti, Zabadi mwana wa Alai, 42 Adina mwana wa Shiza Murubeni, kichwa cha Warubeni, na makumi tatu (30) pamoja naye; 43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mumitini, 44 Uziya Mwashtaroti, Shama na Yeieli, wana wa Hotamu Mwaroeri; 45 Yediaeli mwana wa Shimri, na Yoha ndugu yake Mutisi; 46 Elieli Mumahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, na Itma Mumoabu; 47 Elieli, Obedi, na Yaasieli Mumesoba.