Zaburi
KITABU CHA PILI
(Zaburi 42-72)
2 Niko na kiu kwa ajili ya Mungu, kwa ajili ya Mungu mwenye kuishi.+
Nikuje wakati gani na kuonekana mbele ya Mungu?+
3 Machozi yangu ni chakula changu muchana na usiku;
4 Ninakumbuka mambo haya, na ninamwanga nafsi* yangu,
Kwa maana wakati fulani nilitembea pamoja na kikundi cha watu;
Nilizoea kutembea kwa huzuni* mbele yao mupaka kwenye nyumba ya Mungu,
Kwa sauti za shangwe na shukrani,
Za watu wengi wenye kufanya sikukuu.+
5 Sababu gani nimepoteza tumaini?*+
Sababu gani musukosuko huu uko ndani yangu?
6 Mungu wangu, nimepoteza* tumaini.+
Ndiyo sababu ninakukumbuka,+
Kutoka katika inchi ya Yordani na vichwa vya Hermoni,
Kutoka kwenye Mulima Mizari.*
7 Maji yenye kuenda chini sana yanaita maji yenye kuenda chini sana
Kwa sauti ya maporomoko yako ya maji.
Mawimbi yako yote makubwa yamenilemea.+
8 Wakati wa muchana Yehova atanipatia upendo wake mushikamanifu,
Na usiku wimbo wake utakuwa pamoja na mimi—sala kwa Mungu wa uzima wangu.+
9 Nitamuambia Mungu, mwamba wangu:
“Sababu gani umenisahau?+
Sababu gani nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?”+
10 Maadui wangu wananichokoza kwa chuki kali sana;*
11 Sababu gani nimepoteza* tumaini?
Sababu gani musukosuko huu uko ndani yangu?