Zaburi
Kwa kiongozi. Maskili.* Ya Daudi, wakati Doegi Mwedomu alikuja na kumuambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+
52 Sababu gani unajisifu kuhusu matendo yako maovu, wewe mwenye nguvu?+
Upendo mushikamanifu wa Mungu unadumu muchana wote.+
3 Unapenda uovu kuliko mema,
Kusema uongo kuliko kusema mambo yenye kuwa sawa. (Sela)
4 Unapenda kila neno lenye kuumiza,
Ee ulimi mudanganyifu!
5 Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+
Atakukamata haraka na kukupasua kutoka katika hema yako;+
Atakungoa kutoka katika inchi ya wazima.+ (Sela)
7 “Huyu ndiye mwanaume mwenye hakumufanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+
Lakini alitumainia utajiri wake mwingi+