Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, wakati nabii Natani alikuja kwa Daudi kisha yeye kulala na Bat-sheba.+
51 Unionyeshe wema, Ee Mungu, kulingana na upendo wako mushikamanifu.+
Futa makosa yangu kulingana na rehema yako kubwa.+
4 Kukuelekea wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda zambi;+
Nimetenda mambo ya mubaya mbele ya macho yako.+
Kwa hiyo, uko mwenye haki wakati unasema,
Uko mwenye haki katika hukumu yako.+
6 Angalia! Unapendezwa na kweli katika mutu wa ndani;+
Fundisha mutu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.
7 Unisafishe kutokana na zambi yangu kwa hisopo, ili nikuwe safi;+
8 Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,
Ili mifupa yenye uliponda ishangilie.+
11 Usinitupe kutoka mbele yako;
Wala usiondoe roho yako takatifu juu yangu.
13 Nitafundisha wakosaji njia zako,+
Ili watenda-zambi warudie kwako.
14 Uniokoe kutokana na hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+
Ili ulimi wangu utangaze kwa shangwe haki yako.+
15 Ee Yehova, fungua midomo yangu,
Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+
17 Zabihu zenye zinamupendeza Mungu ni roho yenye kuvunjika;
18 Kwa nia yako njema tendea Sayuni mambo mema;
Jenga kuta za Yerusalemu.
19 Halafu utafurahia zabihu za haki,
Zabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;
Kisha ngombe-dume watatolewa kwenye mazabahu yako.+