Zaburi
Kwa kiongozi; imepatanishwa na “Usiharibu.” Ya Daudi. Miktamu.* Wakati Sauli alituma watu wachunguze nyumba ya Daudi* ili wamuue.+
59 Uniokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Mungu wangu;+
Unilinde kutoka kwa wale wenye kusimama ili kunishambulia.+
2 Uniokoe kutoka kwa wale wenye kutenda uovu,
Na uniokoe kutoka kwa watu wenye jeuri.*
Wanaume wenye nguvu wananishambulia
Lakini haiko kwa sababu nimeasi ao kutenda zambi,+ Ee Yehova.
4 Hata kama sikutenda kosa lolote, wanakimbia na kujitayarisha ili kushambulia.
Simama wakati ninakuita na uone.
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ni Mungu wa Israeli.+
Amuka ili ukazie uangalifu wako mataifa yote.
Usionyeshe rehema wasaliti wowote wenye nia mubaya.+ (Sela)
7 Angalia kile kinamwangika* kutoka katika kinywa chao;
Midomo yao ni kama panga,+
Kwa maana wanasema: “Ni nani anasikiliza?”+
10 Mungu mwenye ananitendea kwa upendo mushikamanifu atanisaidia;+
Mungu ataniwezesha niangalie kwa furaha kushindwa kwa maadui wangu.+
11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.
Kwa nguvu zako uwafanye watange-tange;
Uwaangushe, Ee Yehova, ngao yetu.+
12 Kwa sababu ya zambi ya kinywa chao, neno la midomo yao,
Acha kiburi chao kiwanase,+
Kwa sababu ya laana na udanganyifu wenye wanasema.
13 Uwamalize kwa kasirani yako kali;+
Uwamalize, ili wasikuwe tena;
Uwafanye wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo na mupaka kwenye miisho ya dunia.+ (Sela)
15 Acha watange-tange wakitafuta chakula;+
Usiwaruhusu washibe wala kupata makao.
16 Lakini mimi, nitaimba kuhusu nguvu zako;+
Asubui nitatangaza kwa shangwe kuhusu upendo wako mushikamanifu.