Mezali
30 Ujumbe muzito wenye kuwa katika maneno ya Aguri mwana wa Yake, wenye alimuambia Itieli, ndiyo, Itieli na Ukali.
2 Mimi ni mujinga kuliko mutu mwingine yeyote,+
Na sina uelewaji wenye mwanadamu anapaswa kuwa nao.
3 Sijajifunza hekima,
Na sina ujuzi kuhusu Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.
4 Ni nani amepanda mbinguni na kisha akashuka?+
Ni nani amekusanya upepo katika viganja vya mikono mbili?
Ni nani amefunga maji katika nguo yake?+
Ni nani amefanya miisho yote ya dunia kuwa imara?*+
Jina lake ni nani na jina la mwana wake ni nani—kama unajua?
5 Kila neno la Mungu ni safi.+
Yeye ni ngao kwa wale wenye kumukimbilia.+
7 Ninakuomba mambo mbili.
Usiniime mambo hayo mbele nikufe.
8 Ondolea mbali na mimi mambo yenye hayako ya kweli na ya uongo.+
Usinipatie umaskini wala utajiri.
Wala usiruhusu nikuwe maskini, niibe na kuletea haya* jina la Mungu wangu.
10 Usimuchongee mutumishi kwa bwana wake,
Ukifanya vile anaweza kukulaani na utapatikana na hatia.+
11 Kuko kizazi cha watu wenye wanamulaani baba yao
Na hawamubariki mama yao.+
13 Kuko kizazi cha watu wenye macho yenye kujaa kiburi
Na wenye macho yao yanaangalia kwa majivuno mengi!+
14 Kuko kizazi cha watu wenye meno yao ni panga
Na wenye mataya* yao ni visu vya kuchinjia;
Wanameza watu wa hali ya chini wa dunia
Na maskini kutoka kati ya wanadamu.+
15 Vidudu-ruba viko na mabinti wawili wenye kulia, “Nipatie! Nipatie!”
Kuko vitu tatu (3) vyenye havishibake,
Vitu ine (4) vyenye havisemake, “Inaenea!”
17 Jicho lenye linamuchekelea baba na kuzarau kumutii mama+
—Kunguru wa bonde* watalingoa,
Na tai wadogo watalikula.+
18 Kuko mambo tatu (3) yenye kunipita uelewaji,*
Na mambo ine (4) yenye sielewe:
19 Njia ya tai katika mbingu,
Njia ya nyoka juu ya mwamba,
Njia ya mashua* katika bahari kubwa,
Na njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke.
20 Hii ndiyo njia ya mwanamuke muzinifu:
Anakula, anapangusa kinywa chake;
Kisha anasema, “Sikufanya kosa lolote.”+
21 Kuko mambo tatu (3) yenye kutetemesha dunia
Na mambo ine (4) yenye dunia haiwezi kuvumilia:
22 Wakati mutumwa anatawala akiwa mufalme,+
Wakati mupumbavu anashiba sana,
23 Wakati mwanamuke mwenye kuchukiwa* anaolewa,
Na wakati mutumishi mwanamuke anachukua nafasi ya bimukubwa wake.+
24 Kuko vitu ine (4) katika dunia vyenye kuwa kati ya vitu vidogo zaidi,
29 Kuko vitu tatu (3) vyenye mwendo wa kuvutia,
Vitu ine (4) vyenye kuvutia wakati vinatembea:
30 Simba, munyama mwenye nguvu zaidi kuliko wanyama wote,
Mwenye hamukimbie mutu yeyote;+
31 Imbwa-muwindaji; mbuzi-dume;
Na mufalme mwenye kuwa pamoja na jeshi lake.