Yeremia
22 Yehova anasema hivi: “Shuka kwenye nyumba ya mufalme wa Yuda, na utoe ujumbe huu. 2 Unapaswa kusema, ‘Sikia neno la Yehova, Ee mufalme wa Yuda mwenye kukaa juu ya kiti cha ufalme cha Daudi, wewe pamoja na watumishi wako na watu wako, wale wenye wanaingia kupitia milango hii mikubwa. 3 Yehova anasema hivi: “Mutende haki na uadilifu.* Mukomboe mwenye kunyanganywa kutoka katika mukono wa mupunjaji. Musitendee mubaya mukaaji yeyote mugeni, na musiumize mutoto yeyote mwenye hana baba* ao mujane.+ Na musimwange damu yoyote yenye haina hatia mahali hapa.+ 4 Kwa maana kama munakuwa waangalifu ili kutimiza neno hili, basi wafalme wenye kukaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ wataingia kupitia milango mikubwa ya nyumba hii, wakiwa wamepanda katika magari na juu ya farasi, wao pamoja na watumishi wao na watu wao.”’+
5 “‘Lakini kama hamutatii maneno haya, mimi ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwamba nyumba hii itakuwa mahali kwenye kuliharibiwa.’+
6 “Kwa maana Yehova anasema hivi juu ya nyumba ya mufalme wa Yuda:
‘Wewe ni kama Gileadi kwangu,
Kama kichwa cha Lebanoni.
Lakini nitakufanya kuwa jangwa;
Hakuna muji wako hata mumoja wenye utaikaliwa.+
Watakata miti yako ya mierezi ya muzuri zaidi
Na kuiangusha ndani ya moto.+
8 Na mataifa mengi yatapita pembeni ya muji huu na kuambiana: “Sababu gani Yehova alitendea hivi muji huu mukubwa?”+ 9 Na watajibu: “Kwa sababu waliacha agano la Yehova Mungu wao na wakainamia miungu mingine na kuitumikia.”’+
10 Musilie kwa sababu ya mutu mwenye alikufa,
Na musisikitike kwa sababu yake.
Tofauti na hilo, mulie sana kwa sababu ya ule mwenye anaenda zake mbali,
Kwa maana hatarudia tena ili kuona inchi yenye alizaliwa ndani.
11 “Kwa maana Yehova anasema hivi juu ya Shalumu*+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda mwenye anatawala pa nafasi ya Yosia baba yake+ na mwenye ameondoka mahali hapa: ‘Hatarudia pale tena. 12 Kwa maana atakufa mahali kwenye wamemupeleka katika uhamisho, na hataona tena inchi hii.’+
13 Ole wake mutu mwenye anajenga nyumba yake bila uadilifu*
Na vyumba vyake vya juu bila haki,
Mwenye anafanya mwanadamu mwenzake amutumikie bure,
Na mwenye anakataa kumulipa malipo yake;+
14 Ule mwenye anasema, ‘Nitajijengea nyumba yenye nafasi kubwa
Yenye vyumba vya juu vyenye nafasi kubwa.
Nitaiwekea madirisha
Na nitaifunika kwa mbao za mierezi na nitaipakaa rangi nyekundu sana.’
15 Je, utaendelea kutawala kwa sababu unapita wengine kwa kutumia miti ya mierezi?
16 Alitetea haki ya mwenye kuteseka na maskini,
Basi mambo yakakuwa muzuri.
‘Je, haiko hiyo ndiyo maana ya kunijua?’ ni vile Yehova anasema.
17 ‘Lakini macho yako na moyo wako vinakazia tu faida yako yenye haiko ya haki,
Kumwanga damu yenye haina kosa,
Na kufanya upunjaji na unyanganyi.’
18 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:
‘Hawatamuombolezea:
“Aa! ndugu yangu! Aa! dada yangu!”
Hawatamuombolezea:
“Aa! Ee bwana! Aa! muheshimiwa mufalme!”
20 Panda mupaka Lebanoni na useme kwa sauti kubwa,
Pandisha sauti yako katika Bashani,
Na useme kwa sauti kubwa kutoka Abarimu,+
Kwa maana wote wenye wanakupenda kwa tamaa wamepondwa.+
21 Nilisema na wewe wakati ulijisikia kuwa salama.
Lakini ulisema, ‘Sitatii.’+
Hii imekuwa njia yako tangu ujana,
Kwa maana haukutii sauti yangu.+
22 Upepo utachunga wachungaji wako wote,+
Na wale wenye wanakupenda kwa tamaa wataenda katika utekwa.
Kisha utapatishwa haya na kufezeheshwa kwa sababu ya musiba wako wote.
23 Ee wewe mwenye kukaa katika Lebanoni,+
Mwenye kuwa na chicha* kati ya miti ya mierezi,+
Namna utalia kwa maumivu wakati uchungu utakuja juu yako,
24 “‘Kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Yehova anasema, ‘hata kama Konia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mufalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri kwenye mukono wangu wa kuume, ningekungoa kutoka pale! 25 Nitakutia katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wako,* katika mukono wa wale wenye unaogopa, katika mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni, na katika mukono wa Wakaldayo.+ 26 Na wewe pamoja na mama yako mwenye alikuzaa nitawatupa katika inchi ingine kwenye hamukuzaliwa, na mutakufa kule. 27 Na hawatarudia hata kidogo katika inchi yenye wanatamani.*+
28 Je, mutu huyu Konia ni chungu tu chenye kuzarauliwa, chenye kuvunjika,
Chombo chenye hakuna mutu mwenye anataka?
Sababu gani yeye na wazao wake wametupwa chini
Na kutupwa katika inchi yenye hawajue?’+
29 Ee dunia,* dunia, dunia, sikia neno la Yehova.
30 Yehova anasema hivi: