Yeremia
45 Hili ndilo neno lenye Yeremia nabii alimuambia Baruku+ mwana wa Neria wakati aliandika katika kitabu maneno haya yenye yalisemwa na Yeremia+ katika mwaka wa ine (4) wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:
2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi juu yako wewe, Baruku: 3 ‘Umesema: “Ole wangu, kwa maana Yehova ameongeza huzuni kwenye maumivu yangu! Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu, na sikupata mahali pa kupumuzikia.”’
4 “Umuambie, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia! Kile chenye nimejenga ninakibomoa, na kile chenye nimepanda ninakingoa—inchi yote.+ 5 Lakini unajitafutia* mambo makubwa. Acha kutafuta mambo hayo.”’
“‘Kwa maana, niko karibu kuleta musiba juu ya miili yote,’*+ ni vile Yehova anasema, ‘na kila mahali kwenye unaweza kuenda, nitakupatia uzima wako* kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita.’”*+