Hosea
5 “Musikie jambo hili, ninyi makuhani,+
Mukaze uangalifu, Ee nyumba ya Israeli,
Musikilize, Ee nyumba ya mufalme,
Kwa maana hukumu hii inawahusu ninyi pia;
Kwa sababu ninyi ni mutego kwa Mispa
3 Ninajua Efraimu,
Na Israeli haijifiche kwangu.
4 Matendo yao hayawaruhusu wamurudilie Mungu wao,
Kwa sababu kuko roho ya ukahaba* kati yao;+
Na hawamutambue Yehova.
5 Kiburi cha Israeli kimeshuhudia juu yake;*+
Israeli na pia Efraimu wamejikwaa katika kosa lao,
Na Yuda imejikwaa pamoja nao.+
6 Walienda kumutafuta Yehova wakiwa na makundi yao na mifugo yao,
Lakini hawakumupata.
Alikuwa amejitenga nao.+
7 Wamemusaliti Yehova,+
Kwa maana wamekuwa baba za wana wa kigeni.
Sasa mwezi mumoja utawameza* pamoja na mafungu* yao.
8 Mupige baragumu+ katika Gibea, tarumbeta katika Rama!+
Mufanye makelele ya vita katika Bet-aveni+—nyuma yako, Ee Benyamini!
9 Ee Efraimu, utakuwa kitu cha kuogopesha sana katika siku ya azabu.+
Nimejulisha jambo lenye litatendeka hakika kati ya makabila ya Israeli.
10 Wakubwa wa Yuda ni kama watu wenye wanasogeza mupaka.+
Nitawamwangia kasirani yangu kali kama maji.
11 Efraimu amekandamizwa, amepondwa kwa hukumu,
Kwa maana alikusudia kufuata adui yake.+
12 Basi nilikuwa kama nondo* kwa Efraimu
Na kama kuoza kwa ajili ya nyumba ya Yuda.
13 Wakati Efraimu aliona ugonjwa wake, na Yuda kidonda chake,
Efraimu alienda Ashuru+ na kutuma ujumbe kwa mufalme mukubwa.
Lakini hakuweza kuwaponyesha ninyi,
Na hakuweza kuponyesha kidonda chenu.
14 Kwa maana nitakuwa kama mwana-simba kwa ajili ya Efraimu,
Na kama simba mwenye nguvu* kwa ajili ya nyumba ya Yuda.
15 Nitaenda na kurudia mahali pangu mupaka wakati watabeba matokeo ya hatia yao,
Wakati watakuwa katika taabu, watanitafuta.”+